Vidumu ni vitu gani hasa?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,997
Nimekuwa nikisikia mara kwa mara "nina kidumu" au mdada anajisifia "kidumu chake" kiko hivi au vile. Mwanzoni nilifikiria wanazungumzia vile ambavyo si "galoni". Lakini siku za karibuni vidumu vimezidi kupata nafasi kubwa katika maisha ya baadhi ya kina dada na naambiwa vinalingana na kile ambacho wanaume wanakiita "nyumba ndogo".




Je kuna ulingano katika upatikanaji, matumizi na matunzo? Kidumu chaweza kufanywa kuwa galoni kama vile nyumba ndogo yaweza kuwa "big house"? Au vidumu kwa kawaida hubakia kuwa vidumu. Hili ni swali kwa wale ambao "rafiki" zao wana vigumu, wamewahi kuwa na vidumu au wana mpango wa kuwa na vidumu kwa matumizi ya "dharura".

Vidumu huwa vinadumu kweli au ni vigumu kudumu?
 
Honestly vidumu vina manufaa sana!Ndo ikianza kuvuja unaipeleka kuchomewa huku unaendelea na kidumu chako...kwa vile maji ni uhai wa maisha inabidi uwe na chombo kingine chakuyapatia just incase kile kikubwa kikiwa hakipo either kwasababu kimeazimwa...hukitaki tena au kimeharibika.

Kuhusu matumizi na matunzo kuna unafuu tofauti na nyumba ndogo kwa wanaume au “ndoo“ kwa wanawake.Imagine ukubwa wa ndoo...ukiweka maji nusu itapepesuka kichwani...ukijaza italemea!Ila kidumu hata wa mkono unabeba!!
 
Honestly vidumu vina manufaa sana!Ndo ikianza kuvuja unaipeleka kuchomewa huku unaendelea na kidumu chako...kwa vile maji ni uhai wa maisha inabidi uwe na chombo kingine chakuyapatia just incase kile kikubwa kikiwa hakipo either kwasababu kimeazimwa...hukitaki tena au kimeharibika.

Kuhusu matumizi na matunzo kuna unafuu tofauti na nyumba ndogo kwa wanaume au "ndoo" kwa wanawake.Imagine ukubwa wa ndoo...ukiweka maji nusu itapepesuka kichwani...ukijaza italemea!Ila kidumu hata wa mkono unabeba!!
Umeelezea vizuri sana sina haja ya kuongezea
 
Kidumu kina raha na karaha yake hasa pale unapoenda bafuni kuoga kinakuwa hakitoshi unatoka bafuni na mapovu kichwani ila ukiwa na ndoo yako kubwa akuuuu unaoga kwa raha zako

kidumu kinafanya kazi ndoo inaposhindwa kukamilisha kazi iliyoianza. mfano unaoga kwa bahati mbaya maji ya ndoo yakamwagika; kidumu kitasaidia kuondoa povu.
ndoo inabebwa kichwani kidumu mkononi kwa hiyo uwezekano wa maji ya ndoo kumwagika ni mkubwa kuliko kidumu.
 
ukimwi utatuua wengi. coz nyumba nyummba ndogo plus kidumu on the other side afu fikiria chain yake inakuwaje. unaweza shangaa inafika mpka kwa binamu yako then inarudi mpaka kwa mamdogo wako. tumekwishaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
mhh, wadada mna mambo....kwa bahat mbaya mm ndo mto wenyewe, tena siyo seasonal. wangu hahtaj kidum wala kijiko anaogelea atakavyo na hana haja ya kuhfadh maji pemben
hahahahahahaha duh we umefunika kabisa, anaoga anaoogelea na asipofanya yote atakuja kuvuka tu kwendaa upande wa pili
 
:biggrin1::biggrin1: yaani kuna vikopo, vidumu , Ndoo na Pipa mpaka tanki.....we mdada jiangalie wapi panafaa....:biggrin1::biggrin1: angalia usijeota matuta kwenye misuli ya shingo na mikono ukawa kama baunsa hutamaniki :biggrin1::biggrin1: wakati wenzako wanatumia matanki full kimiminika walaaaiiiniiii :biggrin1::A S-rose::tonguez:
 
ukimwi utatuua wengi. coz nyumba nyummba ndogo plus kidumu on the other side afu fikiria chain yake inakuwaje. unaweza shangaa inafika mpka kwa binamu yako then inarudi mpaka kwa mamdogo wako. tumekwishaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

mkuu ukifikiria hizi cheni inatisha!huwa sipendi hata kutafakari juu ya hilo sana,ukweli wanawake nao kwa sasa wanatamba na vidumu! Iwe ana stress au hana ili mradi ni hulka ya mtu,lkn kama si hulka yake mwanamke mpaka awe na kidumu ujue kuna pengo anaziba ambalo yule alie nae hajafanikisha,vidumu huwa si sawa na nyumba ndogo za wanaume kny matumizi labda ikute mwanamke mwenyewe ni sugar mamy ndo kidumu kitahudumiwa kama small house za wanaume
 
mhh, wadada mna mambo....kwa bahat mbaya mm ndo mto wenyewe, tena siyo seasonal. wangu hahtaj kidum wala kijiko anaogelea atakavyo na hana haja ya kuhfadh maji pemben

kaka usiusemee Moyo.......!ukiona mwenzio ananyolewa tia maji.......
 
Hivi ili kiwe kidumu, je ni lazima kiwe na rangi ya blue, njano, nyeupe, ama nyeusi??
Hivi ili kiwe kidumu, je ni lazima kiwe na ujazo mdogo kuliko ule wa ndoo??
Hivi ili kiwe kidumu, je ni lazima kiwe cha plastic na si cha udongo wala chuma??
 
Vidumu ni mipango ya pembeni.
Huwa vinadumu kutegemea na namna mnavyoishi hasa pale kidumu anapojijua yeye ni kidumu.
Ubaya ni kwamba vidumu vingi havitaki kujikubali vinataka wao ndio wamiliki hivyo kujifanya wana kauli kuliko wenye mali.
Vinasaidia pale mdada anapokuwa hayupo katika situation nzuri ya kimahusiano na mpenzi wake na ni katika kipindi hicho hicho kidumu ana nafasi kubwa ya kumiliki jumla.
Nafikiri ni vizuri kuridhika na mpnzi mmoja maana ukianza na kidumu kimoja utataka kingine mwishoni uwe na msururu wa vidumu hata ndoo uisahau.
 
kidumu kinafanya kazi ndoo inaposhindwa kukamilisha kazi iliyoianza. mfano unaoga kwa bahati mbaya maji ya ndoo yakamwagika; kidumu kitasaidia kuondoa povu.
ndoo inabebwa kichwani kidumu mkononi kwa hiyo uwezekano wa maji ya ndoo kumwagika ni mkubwa kuliko kidumu.

Halafu nadhani ni jambo rahisi kubeba vidumu viwili kila mkono kwa wakati mmoja kuliko ndoo mbili, well, unless wewe ni Power Mabula!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom