X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Siyo siri kuwa Kanisa la Kirumi la Kikatoliki linaanza kuuona mwanga na ukweli. Kama mizengwe na unyanyasaji na urushi havitarudiwa, kuna haja ya kulipa shime na heko kwa kuachana na unafiki na ukale visivyo na ulazima.
Kanisa la Vatikan chini ya Rais wake, Papa Benedicto XVI linafanya mashauriano na baadhi ya wanamapinduzi ya kiroho juu ya sakramenti takatifu ya ndoa. Harakati hizi kwa upande mwingine zinaongozwa na Askofu mwenye mke, Emmanuel Milingo toka Zambia.
Ulimwengu unakumbuka jinsi gwiji huyu wa theolojia na uponyaji alivyolitia kanisa msambweni pale alipoamua kuachana na ukapela na kumuoa Daktari Maria Sung (48), toka Korea ya Kusini. Ndoa hii iliyofana ilibarikiwa na Mchungaji Sung Myung Moon wa kanisa la Unification mwaka 2001.
Kanisa kwa nguvu zake zote lilifanikiwa kumrubuni na kumrejesha Milingo kwenye kundi. Katika hatua hii mwezi Augusti 2001 alimkana mkewe na kurejea Vatikan alikofanya maombi na kufunga kabla ya kupelekwa uhamishoni nchini Argentina.
Kwa mara ya kwanza wakati huo, kanisa na Bi Milingo waliingia mvutano usio wa kawaida hasa pale Mke wa Miliongo Daktari Maria Milingo alipodai kuwa kanisa lilikuwa limemteka mumewe.
Kwa kitambo kidogo kanisa liliona kama limeshinda kumbe wapi. Maana baadaye Milingo alimrudia mkewe na kuendelea na kazi yake ya uponyaji na kuishi maisha ya ndoa.
Mlingo mwanamapinduzi na mwanatheolojia asiyeshindwa na anayejua anachofanya, ameibuka upya jijini New-York akiwa na mkewe. Amekwenda maili moja mbele kwa kuanzisha jumuia inayoitwa "Married Priests Now".
Kanisa limemtimua tena mwezi Oktoba baada ya kuwapa daraja la uaskofu mapadre wanne waliooa nchini Marekani.
Anatarajia kuitangaza jumuia yake atakapokutana na mapadre wapatao 1,000.
Jambo hili limelifanya kanisa la Roma kuanza harakati za kujadili suala zima la useja na ukasisi.
Wale wanaopinga useja kwa makasisi wanadai kuwa hata Papa wa Kwanza kama kanisa linavyotuaminisha, Petro alikuwa ni mtu aliyeoa. Vile vile ukisoma Biblia hakuna sehemu hata moja Mungu anapozuia Mapadre kuoa wala Masista kutoolewa.
Kitu kingine kinachofanya wanaopinga useja wa kulazimishwa kwenye kanisa la Roma ambao umekuwapo kwa takribani miaka 1,000, ni kuongezeka kwa kashfa za uzinzi na ulawiti miongoni mwa Mapadre na uzinzi kwa Masista.
Soma 1 Timotheo 3:1-12 anasema ukiitaka kazi ya uaskofu umetaka kazi njema.
Askofu awe mume wa mke mmoja,mtu wa makamo,asiwe mpenda mvinyo na pesa na mtu anayeweza kuitiisha familia yake. Je maaskofu wa Kikatoliki wanazo sifa hizo?
1 Timotheo 4:1-4 roho asema wazi kuwa kutakuja wakati wengi wataanguka wakizitii roho chafu na itikadi za kishetani.
Kwa kutumia unafiki wa waongo tena kwa ugumu wa chuma. Wanaozuia ndoa na kutetea kuacha kula baadhi ya vyakula....
1 Timotheo 5: 9-11 kwa watawa au masista awe na umri si chini ya miaka 60 kwani chini ya hapo bado anahitaji kuolewa na kuzaa watoto.
Historia.
Papa Paulo V (1605-1621) Alipotaka madanguro yote ya Roma iliyokuwa na watu 100,000 na madanguro 6,000, waumini walikuja juu wakisema kuwa kufanya hivyo kutafanya mapadri wawatongoze wake zao.
Papa Grigori XV (1621-1623) Alipoamru kisima karibu na nyumba ya watawa kikaushwe, alishtuka kukuta mafuvu ya vichanga zaidi ya 6,000.
Kardinali Peter D'Ailly aliwahi kusema kuwa kuvaa joho la usista ni sawa na kutangaza kuwa u kahaba wa jamii.
Albert The Magnificient wa Humburg Ujerumani, mnamo mwaka 1477 alipigwa na butwaa baada ya kugundua kuwa wanawake wapatao 11,000 kwenye jimbo lake walikuwa wamewekwa kinyumba na watawa. Msemo kuwa Padre ni kuwa mume wa wanawake wote.
Akiwaonya Mapadre wake Albert alisema "Si non caste,tamen caute" yaani kama huuwezi utaua basi uwe mwangalifu. Yaani ufanye mambo yako kwa usiri.
Hivyo basi ni wakati muafaka wa kulirudisha kanisa kwenye ukweli kwa kuruhusu Mapadri waoe na Masista waolewe. Tena itakuwa rahisi maana wawili hawa wanajuana vilivyo ni suala la kutangaza kuachana na usiri na unafiki vinginevyo tendo lipo na halina ubishi.
Kufanya hivyo kutarejesha hata imani ya waumini kwa watumishi wa Mungu ambao kusema ukweli kwa sasa ni hatari na uzembe kuwaamini hasa katika masuala ya ndoa.
Kanisa la Vatikan chini ya Rais wake, Papa Benedicto XVI linafanya mashauriano na baadhi ya wanamapinduzi ya kiroho juu ya sakramenti takatifu ya ndoa. Harakati hizi kwa upande mwingine zinaongozwa na Askofu mwenye mke, Emmanuel Milingo toka Zambia.
Ulimwengu unakumbuka jinsi gwiji huyu wa theolojia na uponyaji alivyolitia kanisa msambweni pale alipoamua kuachana na ukapela na kumuoa Daktari Maria Sung (48), toka Korea ya Kusini. Ndoa hii iliyofana ilibarikiwa na Mchungaji Sung Myung Moon wa kanisa la Unification mwaka 2001.
Kanisa kwa nguvu zake zote lilifanikiwa kumrubuni na kumrejesha Milingo kwenye kundi. Katika hatua hii mwezi Augusti 2001 alimkana mkewe na kurejea Vatikan alikofanya maombi na kufunga kabla ya kupelekwa uhamishoni nchini Argentina.
Kwa mara ya kwanza wakati huo, kanisa na Bi Milingo waliingia mvutano usio wa kawaida hasa pale Mke wa Miliongo Daktari Maria Milingo alipodai kuwa kanisa lilikuwa limemteka mumewe.
Kwa kitambo kidogo kanisa liliona kama limeshinda kumbe wapi. Maana baadaye Milingo alimrudia mkewe na kuendelea na kazi yake ya uponyaji na kuishi maisha ya ndoa.
Mlingo mwanamapinduzi na mwanatheolojia asiyeshindwa na anayejua anachofanya, ameibuka upya jijini New-York akiwa na mkewe. Amekwenda maili moja mbele kwa kuanzisha jumuia inayoitwa "Married Priests Now".
Kanisa limemtimua tena mwezi Oktoba baada ya kuwapa daraja la uaskofu mapadre wanne waliooa nchini Marekani.
Anatarajia kuitangaza jumuia yake atakapokutana na mapadre wapatao 1,000.
Jambo hili limelifanya kanisa la Roma kuanza harakati za kujadili suala zima la useja na ukasisi.
Wale wanaopinga useja kwa makasisi wanadai kuwa hata Papa wa Kwanza kama kanisa linavyotuaminisha, Petro alikuwa ni mtu aliyeoa. Vile vile ukisoma Biblia hakuna sehemu hata moja Mungu anapozuia Mapadre kuoa wala Masista kutoolewa.
Kitu kingine kinachofanya wanaopinga useja wa kulazimishwa kwenye kanisa la Roma ambao umekuwapo kwa takribani miaka 1,000, ni kuongezeka kwa kashfa za uzinzi na ulawiti miongoni mwa Mapadre na uzinzi kwa Masista.
Soma 1 Timotheo 3:1-12 anasema ukiitaka kazi ya uaskofu umetaka kazi njema.
Askofu awe mume wa mke mmoja,mtu wa makamo,asiwe mpenda mvinyo na pesa na mtu anayeweza kuitiisha familia yake. Je maaskofu wa Kikatoliki wanazo sifa hizo?
1 Timotheo 4:1-4 roho asema wazi kuwa kutakuja wakati wengi wataanguka wakizitii roho chafu na itikadi za kishetani.
Kwa kutumia unafiki wa waongo tena kwa ugumu wa chuma. Wanaozuia ndoa na kutetea kuacha kula baadhi ya vyakula....
1 Timotheo 5: 9-11 kwa watawa au masista awe na umri si chini ya miaka 60 kwani chini ya hapo bado anahitaji kuolewa na kuzaa watoto.
Historia.
Papa Paulo V (1605-1621) Alipotaka madanguro yote ya Roma iliyokuwa na watu 100,000 na madanguro 6,000, waumini walikuja juu wakisema kuwa kufanya hivyo kutafanya mapadri wawatongoze wake zao.
Papa Grigori XV (1621-1623) Alipoamru kisima karibu na nyumba ya watawa kikaushwe, alishtuka kukuta mafuvu ya vichanga zaidi ya 6,000.
Kardinali Peter D'Ailly aliwahi kusema kuwa kuvaa joho la usista ni sawa na kutangaza kuwa u kahaba wa jamii.
Albert The Magnificient wa Humburg Ujerumani, mnamo mwaka 1477 alipigwa na butwaa baada ya kugundua kuwa wanawake wapatao 11,000 kwenye jimbo lake walikuwa wamewekwa kinyumba na watawa. Msemo kuwa Padre ni kuwa mume wa wanawake wote.
Akiwaonya Mapadre wake Albert alisema "Si non caste,tamen caute" yaani kama huuwezi utaua basi uwe mwangalifu. Yaani ufanye mambo yako kwa usiri.
Hivyo basi ni wakati muafaka wa kulirudisha kanisa kwenye ukweli kwa kuruhusu Mapadri waoe na Masista waolewe. Tena itakuwa rahisi maana wawili hawa wanajuana vilivyo ni suala la kutangaza kuachana na usiri na unafiki vinginevyo tendo lipo na halina ubishi.
Kufanya hivyo kutarejesha hata imani ya waumini kwa watumishi wa Mungu ambao kusema ukweli kwa sasa ni hatari na uzembe kuwaamini hasa katika masuala ya ndoa.