Machepele
JF-Expert Member
- Jun 28, 2019
- 289
- 420
MASHAIRI YA SHAGALABAGALA
NCHI YA AZMA
*******
Nchi ya AZMA wasomi wake wanauza elimu kwa teuzi na mishahara, sina shaka na uelekeo unapoenda, Shaka ninalo namna utakavyofika unakoenda.
Nguvu kazi imejenga ufalme kwenye social media,
Nchi ya AZMA umepiga bomu kwenye sheria umewaharibia, Njia pekee ya kuupinga uongo ni kuuleta ukweli kwa sheria.
Nchi ya AZMA ajira hamna hata kujiajiri kwa mitaji ya bando, Napo wamezuiliwa unaenda wapi nchi ya AZMA,
Nchi ya AZMA wasomi wako ndiyo majambazi wako wa kesho.
Chagua moja kujenga ajira au gereza Kuimarisha daraja au ukuta ili tujue kama tutafika,
Nchi ya AZMA watu wako wanakosoa mpaka mema unayoyafanya.
Na watu wako wanamsema SIAZMA kwa mabaya, Mabaya yenye faida kwao vizuri wanayanena Nashindwa kuelewa maana wananichanganya.
Nchi ya AZMA wanaosema wanataka demokrasia Wanadai umejaa demogasia ila wao wanajiendesha kwa demohisia
Kimsingi kwao hakuna jema, pole sana nchi ya AZMA kwa unayopitia.
Siyajui maono yako AZMA ila japo unafanya tofauti na tulivyozowea,
Ila naamini kuna mahala unatupeleka, kazi ni kwako AZMA,
Siasa imezidi utaalam na wataalam wamezidi siasa.
AZMA, kalamu yangu wino umeniisha siku nikikuona yapo mengi nitakuambia, Siku nikibahatika kukuona yapo mengi sana nitahadithia, Kwa mola wangu muumba amani nakuombea, Wasalaamu mwana asiye haramu.
MASHAIRI YA SHAGALABAGALA
#NCHI YA AZMA.
Machepele, Tanzania.
Kahama.
NCHI YA AZMA
*******
Nchi ya AZMA wasomi wake wanauza elimu kwa teuzi na mishahara, sina shaka na uelekeo unapoenda, Shaka ninalo namna utakavyofika unakoenda.
Nguvu kazi imejenga ufalme kwenye social media,
Nchi ya AZMA umepiga bomu kwenye sheria umewaharibia, Njia pekee ya kuupinga uongo ni kuuleta ukweli kwa sheria.
Nchi ya AZMA ajira hamna hata kujiajiri kwa mitaji ya bando, Napo wamezuiliwa unaenda wapi nchi ya AZMA,
Nchi ya AZMA wasomi wako ndiyo majambazi wako wa kesho.
Chagua moja kujenga ajira au gereza Kuimarisha daraja au ukuta ili tujue kama tutafika,
Nchi ya AZMA watu wako wanakosoa mpaka mema unayoyafanya.
Na watu wako wanamsema SIAZMA kwa mabaya, Mabaya yenye faida kwao vizuri wanayanena Nashindwa kuelewa maana wananichanganya.
Nchi ya AZMA wanaosema wanataka demokrasia Wanadai umejaa demogasia ila wao wanajiendesha kwa demohisia
Kimsingi kwao hakuna jema, pole sana nchi ya AZMA kwa unayopitia.
Siyajui maono yako AZMA ila japo unafanya tofauti na tulivyozowea,
Ila naamini kuna mahala unatupeleka, kazi ni kwako AZMA,
Siasa imezidi utaalam na wataalam wamezidi siasa.
AZMA, kalamu yangu wino umeniisha siku nikikuona yapo mengi nitakuambia, Siku nikibahatika kukuona yapo mengi sana nitahadithia, Kwa mola wangu muumba amani nakuombea, Wasalaamu mwana asiye haramu.
MASHAIRI YA SHAGALABAGALA
#NCHI YA AZMA.
Machepele, Tanzania.
Kahama.