ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Kwa sasa imekuwa ni tabia kwa watanzania walio wengi kuthamini sana vyakula vya "Super Markets" kuanzia matunda, mbogamboga na hata vitoweo na vitafunywa.
Pengine wengi tunaweza kuathirika baada ya muda fulani kutokana na aina hii ya maisha ambayo asili yake ni Ulaya na Marekani. Tofauti na wenzetu ambapo nchi zao zimekuwa makini kuhakikisha usalama wa raia wao kwa kila nyanja ikiwemo kuweka mifumo ya kuwabana wafanyabiashara wasiuze bidhaa feki zitakazoumiza afya za walaji kupitia sheria (Consumer protection laws) nk, kwetu imekuwa ni holela tupu.
Kwa mara kadhaa nimepitia duka la "Shoprite" la Mlimani City, cha kustaajabisha unakutana na baadhi ya bidhaa hasa matunda na mboga mboga zipo kwenye "shelves" zikiwa zimebaindikwa "label" ya kuzitangaza lakini katika hiyo "label" huwezi kuona "display date" (yaani tarehe halisi ambayo bidhaa imewekwa kwenye shelf) na wala hakuna tarehe ya kuondolewa kutoka kwenye "shelf" (Expiry date").
Leo nimekuta "ma-apple", uyoga na karoti vikiwa vina dalili zote za kuvunda ndani yake lakini bado zimetundikwa kwenye makabati ya kuuzia na hakuna dalili zozote ya kuviundoa wala kupunguza bei hivi karibuin kutokana na muda wake wa kuliwa kuwa umepita (expired)...cha kusikitisha zaidi,sidhani hata kama mle dukani kuna wataalamu wa kuthibiti ubora wa bidhaa za jinsi hiyo.
Nimejaribu kuangalia kwa jicho kali kwenye makabati na baadae kubaini kuwa kuna tag imepachikwa juu ya flamu sambamba na "ma-apple" inasoma "9/10" (sina hakika sana kama ni "Septemba, 2010" au lah)..ikiwa hii ndio tarehe halisi ambayo yalipachikwa hapo, ni hatari sana. Tuwe makini na hawa wenzetu wandugu!!, kuna maeneo mengine tumeyajengea tabia kana kwamba haya epukiki japo yanatupunguzia uahi wetu kwa mfano "kwenye zinaa wataalamu wa afya wanatuasa kwa staili ya ajabu wakisema ..".UKIMWI NI HATARI.., CHUKUA TAHADAHIRI, ...UKISHINDWA TUMIA KONDOMU"..Lakini hili la vyakula vibovu, hatuhitaji kufundishwa tukishindwa kununua huko twende wapi...tunaangamia kimya kimya!!
Cha kusikitisha, kila kukicha tunasikia Mamlaka ya Vyakula na Dawa (TFDA) ikihangaika na kuwaminya wafanyabiashara wadogo wa kizalendo kwenye maduka ya Vipodozi na Dawa Baridi..sijui kwa hawa wauzaji wa bidhaa katika Maduka makubwa kama SHOPRITE wanadhibitiwaje...
Pengine wengi tunaweza kuathirika baada ya muda fulani kutokana na aina hii ya maisha ambayo asili yake ni Ulaya na Marekani. Tofauti na wenzetu ambapo nchi zao zimekuwa makini kuhakikisha usalama wa raia wao kwa kila nyanja ikiwemo kuweka mifumo ya kuwabana wafanyabiashara wasiuze bidhaa feki zitakazoumiza afya za walaji kupitia sheria (Consumer protection laws) nk, kwetu imekuwa ni holela tupu.
Kwa mara kadhaa nimepitia duka la "Shoprite" la Mlimani City, cha kustaajabisha unakutana na baadhi ya bidhaa hasa matunda na mboga mboga zipo kwenye "shelves" zikiwa zimebaindikwa "label" ya kuzitangaza lakini katika hiyo "label" huwezi kuona "display date" (yaani tarehe halisi ambayo bidhaa imewekwa kwenye shelf) na wala hakuna tarehe ya kuondolewa kutoka kwenye "shelf" (Expiry date").
Leo nimekuta "ma-apple", uyoga na karoti vikiwa vina dalili zote za kuvunda ndani yake lakini bado zimetundikwa kwenye makabati ya kuuzia na hakuna dalili zozote ya kuviundoa wala kupunguza bei hivi karibuin kutokana na muda wake wa kuliwa kuwa umepita (expired)...cha kusikitisha zaidi,sidhani hata kama mle dukani kuna wataalamu wa kuthibiti ubora wa bidhaa za jinsi hiyo.
Nimejaribu kuangalia kwa jicho kali kwenye makabati na baadae kubaini kuwa kuna tag imepachikwa juu ya flamu sambamba na "ma-apple" inasoma "9/10" (sina hakika sana kama ni "Septemba, 2010" au lah)..ikiwa hii ndio tarehe halisi ambayo yalipachikwa hapo, ni hatari sana. Tuwe makini na hawa wenzetu wandugu!!, kuna maeneo mengine tumeyajengea tabia kana kwamba haya epukiki japo yanatupunguzia uahi wetu kwa mfano "kwenye zinaa wataalamu wa afya wanatuasa kwa staili ya ajabu wakisema ..".UKIMWI NI HATARI.., CHUKUA TAHADAHIRI, ...UKISHINDWA TUMIA KONDOMU"..Lakini hili la vyakula vibovu, hatuhitaji kufundishwa tukishindwa kununua huko twende wapi...tunaangamia kimya kimya!!
Cha kusikitisha, kila kukicha tunasikia Mamlaka ya Vyakula na Dawa (TFDA) ikihangaika na kuwaminya wafanyabiashara wadogo wa kizalendo kwenye maduka ya Vipodozi na Dawa Baridi..sijui kwa hawa wauzaji wa bidhaa katika Maduka makubwa kama SHOPRITE wanadhibitiwaje...