Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Tanzania imekosa mapato ambayo ingeyapata kama timu zingeukodi uwanja huo kwa ajili ya kujiandaa na mashindano ya Kombe la Dunia yatakayofanyika Afrika kusini kesho.
habari zilizotufikia kutoka vyanzo vyetu vya habari hii vinasema kuwa kuna timu imeurudisha uwanja huo na kuapa kuwa haitaukodi tena kwa maana Tz isahau kuwa uwanja huo kutatokea timu itaukodi ,maana yake watapakazia dunia nzima.
Kilichotokeaa timu hio ilikuwa imeanza mazoezi na ni siku ya mwanzo nyakati za usiku baada ya mataa kuwashwa kulitokea wadudu kibao ,yaani senene au kumbikumbi kwa kwa lugha za walaji kiasi ya kusababisha wacheza wavae mask ili kuwazuia wasiingie midomoni na puani kwa jinsi walivyokuwa wengi.
Hawajakaa vizuri mara umeme umezimwa mara umewashwa ,mara umezimwa tena ,akatafutwa anaehusika na majenereta ikajibiwa kuwa hayupo na haijulikani funguo anazo nani.
Jamaa wakaongozwa kwa tochi hadi vyumba vya kulalia na asubuhi yake wakatafuta ndege na kuelekea kusiko julikana.
habari zilizotufikia kutoka vyanzo vyetu vya habari hii vinasema kuwa kuna timu imeurudisha uwanja huo na kuapa kuwa haitaukodi tena kwa maana Tz isahau kuwa uwanja huo kutatokea timu itaukodi ,maana yake watapakazia dunia nzima.
Kilichotokeaa timu hio ilikuwa imeanza mazoezi na ni siku ya mwanzo nyakati za usiku baada ya mataa kuwashwa kulitokea wadudu kibao ,yaani senene au kumbikumbi kwa kwa lugha za walaji kiasi ya kusababisha wacheza wavae mask ili kuwazuia wasiingie midomoni na puani kwa jinsi walivyokuwa wengi.
Hawajakaa vizuri mara umeme umezimwa mara umewashwa ,mara umezimwa tena ,akatafutwa anaehusika na majenereta ikajibiwa kuwa hayupo na haijulikani funguo anazo nani.
Jamaa wakaongozwa kwa tochi hadi vyumba vya kulalia na asubuhi yake wakatafuta ndege na kuelekea kusiko julikana.