Uwakilishi wa wanawake bungeni Tanzania 35% USA 16.6% what is your take from this

Mazee

Senior Member
Dec 6, 2007
128
24
Country

Tanzania
United States
Leader

President: Jakaya Kikwete
President: Barack Obama
Population
40,213,200
303,825,000


GDP per capita
$1,400 US
$48,000 US

Literacy Rate
69.4%
99%

Corruption Perception Index
3
7.3

Percentage of Women in Parliament
30.4%
16.6%



Source: Country Comparisons - Examine Similarities and Differences between any two countries

percentage of women in parliament in Kenya 9.8%

Anyway this is just to point out few but what does this reflect?Ni kweli Tanzania wanawake wamesoma sana kuliko USA au Kenya?Au wana uwezo mkubwa kiuongozi/Karama/Vipaji kulikowale wa USA.
Pia in USA house representatives number is fixed at 435 with a population of about 303,825,000 against 43million of Tanzania with 357 house representatives
Angalia hapo juu na hiyo tofauti ya GDP na literacy rate .
Jamani mimi sielewi where are heading to as a Nation...
In my opinion uchaguzi wa hawa Viongozi umekaa kisiasa zaidi na si kwa kuzingatia competency zao.Nachelea kuamini kuwa hii 35% ya women inachaguliwa kisiasa zaidi basi tu kutengeza Image flani ya Taifa na pia hii inaonesha ni jinsi gani sasa hata hawa viongozi wa jinsia ya kiume ambavyo wanaweza kuwa ovyo zaidi kwani misingi ya uteuzi wao pia ni questionable Raisi anajichagulia tu ovyo ovyo kudhihirisha hili angalia Kauli zao hawa watu Sijui Werema,Simba na viazi wengine.....kama hawa na wengine ambao wamejaa bungeni kule kiasi kwamba wakianza kuongea unajisikia aibu wewe mwenyewe na kustaajabu kama kweli hao ni wawakilishi wako kweli??

Sijui hiri rinchi rimerogwa.....
 
Sababu iko wazi. Marekani muwakilishi yoyote ni lazima agombee hakuna nafasi za upendeleo. Tanzania tuna viti maalumu zinazo pendelea wakina mama na kama sikosei hata katiba yetu imeainisha kwamba uwakilishi wa wakina mama ni lazima uwe kwenye asilimia 35 kwenye Bunge. Kwa hiyo sisi kama nchi tumeona jinsia ni kipaumbele katika uongozi wakati wenzetu wao jinsia hawaoni kama hoja ya kuzingatiwa.
 
Nakumbuka JK aliwahi kusema kuwa wataongeza viti maalumu kufikia asilimia 40 ya wabunge wa kuchaguliwa sasa sijui tija ni Image au maendeleo ni aibu sana kuwa na vingozi wasiokuwa na vision hapa juzi Tena PM Pinda anasema hajui kwa nini Nchi yetu ni maskini....so pathetic..............
Lakini naamini Mungu anaipenda Tanzania na jina lake tamu kwani ujinga wa wananchi umekuwa ni mtaji mkubwa sana na kwa muda mrefu kwa hawa watawala mafisi...
 
Mimi sipendi viti maalumu kwa sababu moja. Mbunge wa kuteuliwa hana constituency maalumu kama mbunge wa kuchaguliwa kwa maana hana jimbo. Sasa hapa mbunge wa viti maalumu ana muwakilisha nani zaidi ya aliye mteua? Hivi viti ni njia moja wapo tu inayo wezesha chama ambacho kipo madarakani kuongeza wabunge na kutoa nafasi za fadhila na hilo la kutaka kuwezesha wanawake ni gelesha tu inayo tumika kufunika nia na madhumuni ya kweli.
 
Jambo muhimu siyo asilimia kubwa,bali ni uwakilishi makini toka kwa huyo mbunge. Asilimia 5 inaweza ikatikisa bunge kuliko asilimia 50. Sisi huku hatupo makini,tunajaza bungeni nyumba ndogo,mahawara,girl friends na watu wa mipasho!
 
Mkuu tofauti ya US na Tanzania ni kuwa wote wanaoingia kwenye senate na congress lazima wachaguliwe na wapiga kura tofauti na hapa kwetu ambako wengi wanapewa na rais.

Wabunge wa viti maalumu/kuteuliwa na rais wanakwenda bungeni kulinda maslahi ya huyo aliyewachagua na chama wanachowakilisha, hawana umuhimu wala manufaa yoyote zaidi ya kufuja hela za walipa kodi.
 
nilikua nikiisubiri hii topic ... naona ni mojawapo ya agenda za kujadiliwa kwenye katiba mpya

nafasi za upendeleo bungeni ziishe... kila mtu aingie kwa kuchaguliwa na wananchi ili ajibu na awe responsible kwa waliomchagua na si chama au viongozi!

kuwa na independent candidates pale watu wanapoamua kutoona chama kinachowafaa

kuwe na fixed number ya wabunge, na iwe in proportion to the population kama marekani ... maeneo yatakayokua na population kubwa yawe na wawakilishe wengi....review kila census ya miaka 10 kudetermine majimbo ya uchaguzi utakaofuatia

mawaziri na manaibu waziri wasiwe wabunge ... kama walikua wabunge, chama husika kipewe upendeleo wa kutafuta mtu wa kumalizia kipindi chake mpaka uchaguzi mwingine

.... ni hayo tu kwa sasa
 
Sababu nyingine ni kuwa kwa Tanzaia ubunge ni ajira, kwa wenzetu ni uwakilishi!
 
hivi viti viitwe viti maalum vya chama fulani kwani wanaovikalia hawawakilishi Wanawake bali vyama vya siasa . Wanawake wanahangaika hawajui nani wa kuwasemea matatizo yao nani awaonyeshe njia hawaoni halafu mnasema kuna idadi kubwa ya watu wa kuwasemea Wanawake bungeni .
Ikibidi viti vifutwe au kuwe na utaratibu ambao Wanawake wote kimkoa au kiwilaya wachague wanawake wa kuwawakilishe nadhani ndiyo tija inaweza kuonekana
 
huku tukipata taswira ya demokrasia halisi kutoka U.S.A mpaka leo hawana rais mwanamke,hawafikirii na sijuhi kama itatokea hvi karibu sisi huku tuko bize na uongozi chini ya mama ..jamaa wana akili ajabu,wanaanzisha vitu na kutulaghai tuvitumie kisha vinatuzuru wao wanatucheka..ahaa! kweli akili ni nywele,tusidanganywe sana na kutuchekea ...wazungu wako serious kwenye mambo ya msingi
 
Sijawahi kuona faida ya kuwa na viti maalum bungeni, ni bora vifutwe tuu kwenye katiba, coz hao viongozi wenyewe hawana faida na wananchi, zaidi ya kupoteza rasilimali za taifa bila sababu kwa kuwalipa watu ambao hawana faida.
 
tatizo ni kuwadharaulisha mama zetu, badala ya kwenda majimboni kupambana kikakamavu wao wanasubiri ushindi wa mezani kwa VITI MAALUM na matokeo yake wanakuwa VITU MAALUM!
 
Wengi wao wako bungeni kama mizigo tu, hawajielewi wala hawajitambui, wanjaza viti tu ili ionekane kuna watu lkn kiutendaji wengi wao bado na hata hao wanaojitahidi wengine sidhani km walipaswa kuwepo bungeni labda kwenye kuimba taarabu..mfano so*** Lion
 
Na huo upendeleo wa wanawake unawadumaza badala ya kuwasaidia.


Inasikitisha sana kuona nchi "maskini" inavyofuata mkumbo wa kuwa na viti maalum. Kuna wabunge tangia walipoingia kwenye siasa miaka ya 90 wao ni viti maalum tuu hawajui jimbo la uchaguzi. Hivi umewahi kujiuliza inakuwaje mtu anaitwa "Iron Lady" lakini anabebwa kila mara? na hata sasa ameibukia katika kapu la 3 bora la Rais kati ya 10 atakao wateua.
 
kwa USA na Kenya kinachoangaliwa ni uwezo wa mtu kielimu and how she can deliver but hapa kwetu Bongo kinachoangaliwa ni wepesi wa kuvua chupi,period.
 
tatizo ni kuwadharaulisha mama zetu, badala ya kwenda majimboni kupambana kikakamavu wao wanasubiri ushindi wa mezani kwa viti maalum na matokeo yake wanakuwa vitu maalum !

vitu maalum .......
 
Mi naona viti maalumu vingefutwa kabisa,havina maana sana.Ni bora wanawake waende kugombea majimboni.Viti maalumu ni kuongeza garama ya bunge,pia baadhi huenda kusinzia,wanawakilisha nini?Baadhi hupitishwa kulipa fadhila
 
Nchi yetu inaendeshwa kishikaji mno, tunafuata kila kitu tunachoambiwa na western countries, we have never redefined our rules and direction as a country even after the failure of Arusha Declaration, so what do you expect?
kila kiongozi anakuja na mipango yake ya maana na ya hovyo hovyo mpaka akili itakapotuingia na kuona umuhimu wa kufuata yetu badala ya nchi zingine.
 
Back
Top Bottom