Utapeli huu unawaharibia vodacom

Thomas Juma

Member
Nov 9, 2010
88
17
Jana nikiwa katika ofisi yangu kama wakala wa vodacom m-pesa wilaya ya Kahama nimekumbwa na utapeli ambao mpaka sasa sijaelewa huu utapeli umekaa vipi.
Kuna bwana mmoja amefika kwa ajili ya kutoa pesa kwa kuwa cash ilikuwepo nikamruhusu atoe baada ya hapo nikasubiri voda wahakiki kuingia kwa pesa hiyo baada ya muda kweli msg ikaingia kwenye Simu yangu kuwa wamehakiki na float yangu imeongezeka na kuwa kiasi flani ambacho ni kweli kulingana na salio alilotoa huyo bwana + salio lililokuwepo kwenye float pia hata muda ambao huyo bwana ametoa hiyo pesa ni sawasawa kabisa.
Cha kushangaza baada ya muda kidogo mtu mwingine amekuja kuweka pesa nilipokuwa namuwekea pesa kwenye account yake ndipo nikaambiwa salio langu halitoshi, ikabidi nihakikishe kwa kuangalia salio maana uhakika wa kuwa salio lipo nilikuwanao kwa kuwa yule mtu alitoa na nikampatia cash,katika kuangalia salio nikakuta kweli halitoshi.
Nikawapigia vodacom kwa taarifa nilichoambiwa ni kwamba hiyo pesa hawaioni kwenye transaction nilizofanya na kwamba hapo tayar nimeshatapeliwa.
Sawa sasa kuna maswali kadhaa najiuliza;
1/ Hiyo msg ya kuhakiki mbona vodacom ndio waliotuma kuingia kwenye Simu yangu?
2/ kwanini salio langu limewiana ukiongeza na salio la huyu wanaedai kuwa ni tapeli?
3/ Hata muda aliotoa pesa mbona unaendana na muda halisi?

Sasa basi Kama ni utapeli nani kafanya ni vodacom wenyewe au ni mteja?
Na je nitawezaje kutambua tapeli kati ya mteja na vodacom ikiwa msg za uhakiki wanatuma vodacom wenyewe na mwisho wanadai hazionekani kwenye computer zao ili kuweza kumsaidia wakala.
Ndugu zangu naomba kujua nani kanitapeli na je nifanye?
Msaada plz.
 
ulimsainisha kwenye logbook na alikuonyesha kitambulisho? Je wewe kama wakala huwa unawapa wateja simu yako ya uwakala? Mana kuna mtindo mtu akishika simu ya wakala anasave namba kwa jina la mpesa then ana edit sms kwako inafika kwa jina la mpesa kumbe sms ya kawaida sio ya voda
 
Kwenye kitabu kasaini na namba yake ya Simu ninayo japo inapatikana hewani lakin jamaa hapokei
 
Hakuna mtu anachukua Simu yangu isipokuwa Mimi mwenyewe pia msg iliyokuja kwenye Simu yangu ni ya uhakiki kutoka voda na sio kwa mtu kama unavyosema.
 
mkuu watembelee huduma kwa wateja na iyo sms watakupa msaada zaidi ukipiga call center watakuyeyusha tu
 
mkuu watembelee huduma kwa wateja na iyo sms watakupa msaada zaidi ukipiga call center watakuyeyusha tu


Mkuu hiyo watoto wa mjini wanaita "flush message". Mteja anakuja anakuuliza kama anaweza kutoa sh. 1,000,000/=. Ukimwambia atoe, utashtukia imeingia sms ya pesa kuingia kwenye account yako; ila ukiulizia salio lako hautaiona hiyo millioni kwani itasoma salio kabla haijawekwa (kwa maana kwamba umetumiwa sms hewa).
Wanachoghilibu nacho wawa wezi ni kwamba akikuflash msg itaonekana kuwepo na ongezeko kama efu 30 au 50 kwenye hiyo pesa hivyo wewe wakala ukiiwaza cha juu hutakumbuka hata kuangalia salio unafanya chap chap kumtoa ili uweze kufuatilia elf 30 au 50 zako ambazo ni changa la macho.
Hata hiyo sms uipeleke wapi haitambuliki maana namba ya muamala huo inakuwa haipo kwenye record za system za kampuni ya simu.
Mwanzoni mwa mwaka huu tuliwatega baada ya kutuibia mara kibao, tuliwabamba lakini baada ya kuwafikisha kunakohusika tulishangaa wako mtaani vifua mbele wakitutishia hata sisi...............................
 
Back
Top Bottom