Utajiri wa 'ngende' (ushirikina) una masharti magumu kuliko utajiri wowote ule duniani

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,921
36,784
Mambo vipi wazee!

Aisee duniani kuna mambo sana.

Ukienda gende yenyewe original kutafuta utajiri hakika utaupata endapo tu utazingatia masharti yao.

Sharti lao kuu uwe na biashara, hili sharti halihitaji biashara kubwa. Hata biashara ya kuuza nyanya chungu poa tu, hata kuuza mishikaki ya mia mia poa tu.

Jamaa watakupa pesa either ya noti au sarafu ingawa sarafu ndio kipaumbele chao zaidi. Ile pesa utaambiwa kaiweke kwenye mkoba au chombo unachotunzia fedha za mauzo.

Jioni ukipega hesabu utakuta imeji double mara kadhaa.

Kuhusu gharama ya ndagu jamaa kwa ufupi ni Kama wanatoa bure vile maana mara nyingi wanasema utarudi kushukuru wazee ukifanikiwa.

Hapo ndipo utajiri unakujia.

Nitatoa mifano ya watu 4 ninaowafahamu walioshindwa masharti kabla au baada ya utajiri:

1. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sh. Mia moja ya sarafu kila mwaka wakati wa kiangazi. Aliweza kupeleka misimu miwili tu akadharau. Aliishia kuwa fukara.

2. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sindano ya mkono moja kila mwaka wakati wa kiangazi alipekeka mara moja tu akaona ni ujinga, atoke na gari Iringa mpaka Liwale ngende kupeleka sindano ya sh. Hamsini huku anatumia mafuta ya laki 3 . Sasa ni fukara anaomba mpaka sigara.

3. Alipewa sharti la kutokusalimiana au kupeana mkono na mtu yeyote kutoka Liwale Lindi mpaka Dar. Akaona simple. Nakuambia huyu alichemka vibaya. Akarudi kwa bibi akabadilishiwa sharti. Akatajirika ila mwishowe alichemka sharti la pili la kutokuchepuka. Unaambiwa baada ya kuwa na mipesa mastaa wa Bongo warembo unaowafahamu walimzonga kila kona akachepuka nao wawili watatu akafilisika.

4. Huyu alipewa sharti la kusafiri kwa mguu au baiskeli tu. Akafanikiwa sana mpaka alijenga hoteli za kisasa. Akiangalia meneja wa hotel zake zote mbili wana magari yeye ni mwendo wa baiskeli tu. Akanunua magari ya kutembelea. Akafulia.

Visa ni vingi takuja kusimulia vingine.
 
Acha kutapeli watu mkuu,labda Kama unazungumzia ngende ya mgodini,Ila Kama unazungumzia ngende ya liwale iliyoko Kijiji Cha mpigamiti Basi jua unataka kutapeli watu hapa.

Kiufupi huwezi nificha kitu kuhusu huyo Bibi njumwite,na vibaraka wake,wale wote ni matapeli,ukienda pale wako radhi wakupukitushe Hadi chupi uliyovaa,

Wakuu nashauri msijaribu hata kumfuata huyo bwana PM,Ila Kama mnataka kuibiwa Basi jaribuni,I speak from my experience,nimewahi kufika huko,nilichoambulia ni kutapeliwa kila kitu na hao jamaa wa ngende,hakuna jipya nililoliona.
 
Acha kutapeli watu mkuu,labda Kama unazungumzia ngende ya mgodini,Ila Kama unazungumzia ngende ya liwale iliyoko Kijiji Cha mpigamiti Basi jua unataka kutapeli watu hapa.

Kiufupi huwezi nificha kitu kuhusu huyo Bibi njumwite,na vibaraka wake,wale wote ni matapeli,ukienda pale wako radhi wakupukitushe Hadi chupi uliyovaa,

Wakuu nashauri msijaribu hata kumfuata huyo bwana PM,Ila Kama mnataka kuibiwa Basi jaribuni,I speak from my experience,nimewahi kufika huko,nilichoambulia ni kutapeliwa kila kitu na hao jamaa wa ngende,hakuna jipya nililoliona.

Na wewe una moyo sana
 
Acha kutapeli watu mkuu,labda Kama unazungumzia ngende ya mgodini,Ila Kama unazungumzia ngende ya liwale iliyoko Kijiji Cha mpigamiti Basi jua unataka kutapeli watu hapa.

Kiufupi huwezi nificha kitu kuhusu huyo Bibi njumwite,na vibaraka wake,wale wote ni matapeli,ukienda pale wako radhi wakupukitushe Hadi chupi uliyovaa,

Wakuu nashauri msijaribu hata kumfuata huyo bwana PM,Ila Kama mnataka kuibiwa Basi jaribuni,I speak from my experience,nimewahi kufika huko,nilichoambulia ni kutapeliwa kila kitu na hao jamaa wa ngende,hakuna jipya nililoliona.
Mkuu funguka kidogo tuendelee kujifunza
 
Bado nasaka ajira kwa miaka 5 sasa na GPA yangu yangu ya 4.2, na bado NO JOB hadi sasa. Huko kujiajiri wanakopigapiga kelele nako nimejaribu but wapi! Sasa nimeamua kujiajiri kwenye utapeli,nimeanza na ndugu na baada ya kupata uzoefu wa kutosha sasa natapeli kila mtu, hadi wagonjwa mahututi. Huku si kutafuta laana kweli?

Hatia iliyonijaa moyoni inaniambia niachane na udhulmati na ukanjanja wote.Sasa nifanye kipi kingine kama si kwenda huko Ngende?Hivyo visharti vidooogo wanavyotoa vitanishinda kweli na huu msoto niliokwisha pitia.Sharti pekee ambalo siwezi kulikubali ni la kugeuzwa James Delicious, ila mengine yote (hata kulala makaburini in the midnight naweza).

Kwanza nimechoshwa na matusi ya King Msukuma,mtu wa darasa la 7 mwenye jeuri ya kuwananga graduates wa vyuo vikuu kwa sababu yeye ana pesa (za kafara), wao hawana pesa (maana hawategemei utajiri wa kishirikina). Kule Geita kila mtu anajua utajiri wa Msukuma umetokana na nini? Kwanini na mimi nisimpandilie?

Nipeni ramani ya kufika huko.
 
Ngende,Liwale_Lindi..Hivi haya mambo ya uchawi wa ngende bado yapo siku hizi ?

Kuna Mzee alifuatwa na Simba kutoka ngende Hadi barazani kwake kufuata pesa Yao ambayo Mzee alishindwa kufata masharti na alifirisika

...masharti ilikuwa apeleke sh tano kila mwaka na asilale kitandani,alake kwenye kaniki maisha yake yote.Lkn alipofanikiwa kuwa tajiri akajisahau kuwa utajiri wake umetokana na uchawi wa ngende.Huo mwaka ambayo Simba alikuja nyumbani kwake ndy mwaka ambao aliacha kwenda Ngende kupeleka shilling 5 Yao,so Simba wa maajabu akatembea kutoka huko ngende liwale Hadi Lindi kuja kumkumbusha amesahau kupeleka pesa ya watu na Tyr Kwa kufanya hivyo ameshavunja masharti..wakamfirisi kichawi

Enzi nakua ndy nikawa nasimuliwa Stori za huyo Mzee enzi ya utajiri wake wa ngende na jinsi alivyotamba ukanda wote ule wa kusini Lindi na Mtwara
 
Back
Top Bottom