mwalimu mkweli
Member
- Dec 23, 2017
- 35
- 69
Zao la nanasi ni zao ambalo kiasili ni zao linalovumilia ukame na ni zao ambalo la kibiashara lenye faida kubwa.
Kwa hapa Tanzania yapo maeneo mengi ambapo zao hili la nanasi linastawi ila katika mji wa KIWANGWA-BAGAMOYO zao hili linastawi zaidi kutokana na hali ya mwinuko wake kutoka usawa wa bahari pia ardhi nzuri yenye rutuba ya kutosha.
Maeneo mengine yanayolima zao hili ni pamoja na Geita, Kigoma, Shinyanga, Lindi na Mtwara. Kwa baadhi ya maeneo ya Pwani ni Mkuranga, Kibiti na Kibaha.
Sasa leo nitakupa faida ya jinsi ya kulilima nanasi na jinsi ya kujipatia kipato twende wote mpaka mwisho....
NANASI LA KIWANGWA LIPOJE
Katika maeneo yote zao hili linapolimwa KIWANGWA ndiyo sehemu pekee unakutana na mbegu aina ya mpigo nanasi ambalo halistawi kwengine isipokuwa kiwangwa tu.
Pia nanasi la Kiwangwa kiasili ni tamu na ndiyo lenye msimu mzuri wa kilimo. Pamoja na yote rahisi kulifanyia usafirishaji kutokana na ukaribu na miji yote ya kibiashara kulizunguka eneo hili.
NB: Ni kawaida sana kumkuta mkulima wa nanasi wa KIWANGWA anamiliki magari majumba na mali za kutosha ilihali elimu yake ni darasa la saba.
JINSI YA KULIMA NANASI (MAHITAJI)
1. ENEO
Hapa kuna aina mbili za maeneo ya kuanzishia kilimo cha nanasi
i-Shamba jipya, hili ni lile jipya ambalo utaanza kukata miti n.k
ii-Shamba la zamani ambalo hili lilishalimwa limwa
Mashamba yote haya yanapatikana kwa namna mbili
i-Kukodi (laki tano kwa miaka mitano)
ii-Kununua (inategemea ubora wa ardhi, na umbali kutoka kwenye lami)
Kwanini tunaangalia umbali?
Tunaangalia umbali ili isije kusumbua wakati wa kuuza kulileta sokoni. Hivyo umbali ni kitu cha msingi na kujua miundombinu kunafikika kipindi cha mvua.
NB: Tunashauri kama unaanza na hauna hela anza kukodi ila ukinunua ni nzuri zaidi..
2. MBEGU
Kwa kawaida mbegu moja inauzwa wastani wa Tsh 20- 35 inategeemea na wakati kuna muda huwa chini kuna muda hupanda ila haizidi hapo.
Ni bora ukachukua mbegu za wastani na siyo ndogo sana au kubwa sana siyo nzuri kabisa kuzitumia...
Kwa shamba la hekari moja huitaji miche elfu 18 kwa upandaji wa kisasa au hata elfu 16. Tunapanda hivi ili isaidie kupata mananasi makubwa.
GHARAMA ZA KUPANDA
Mbegu tsh 35 × 18000
Kuvunja mbegu baada ya kununua tsh 10 × 18000
Kupakia kwenye gari na kushusha tsh 4 × 18000
Kupanda baada mbegu kufika shamba tsh 50 × 18000
MAANDALIZI YA SHAMBA
Kukodi laki tano
Kusafisha Tsh 80000
Trekta Tsh 50000
NB: Gharama za mbegu ni za mara moja tu mwanzoni unapoanza baada ya hapo zitakuwa zinajizalisha zenye kwahiyo utakuwa nyingine unauza na wewe pia utatumia za kukutosha..
PALIZI
Mpaka unavuna nanasi linahitaji si chini ya pali saba mpaka kumi
CHANGAMOTO ZA KILIMO
Hakuna jambo linalokosa changamoto ila kwa bahati nzuri zao hili halina changamoto ya wadudu wala sijui mvua hakuna nanasi hata iweje lazima liote tu hata kama utakisusa changamoto kubwa ni mbili au tatu...
1. Usimamizi mbovu
2. Ukosefu wa huduma kwa wakati
3. Kwenda kombo kwa soko(ila kwa ulimaji wa kisasa ni rahisi kuliepuka hili)
Muendelezo soma - Muendelezo soma hapa
Kwa hapa Tanzania yapo maeneo mengi ambapo zao hili la nanasi linastawi ila katika mji wa KIWANGWA-BAGAMOYO zao hili linastawi zaidi kutokana na hali ya mwinuko wake kutoka usawa wa bahari pia ardhi nzuri yenye rutuba ya kutosha.
Maeneo mengine yanayolima zao hili ni pamoja na Geita, Kigoma, Shinyanga, Lindi na Mtwara. Kwa baadhi ya maeneo ya Pwani ni Mkuranga, Kibiti na Kibaha.
Sasa leo nitakupa faida ya jinsi ya kulilima nanasi na jinsi ya kujipatia kipato twende wote mpaka mwisho....
NANASI LA KIWANGWA LIPOJE
Katika maeneo yote zao hili linapolimwa KIWANGWA ndiyo sehemu pekee unakutana na mbegu aina ya mpigo nanasi ambalo halistawi kwengine isipokuwa kiwangwa tu.
Pia nanasi la Kiwangwa kiasili ni tamu na ndiyo lenye msimu mzuri wa kilimo. Pamoja na yote rahisi kulifanyia usafirishaji kutokana na ukaribu na miji yote ya kibiashara kulizunguka eneo hili.
NB: Ni kawaida sana kumkuta mkulima wa nanasi wa KIWANGWA anamiliki magari majumba na mali za kutosha ilihali elimu yake ni darasa la saba.
JINSI YA KULIMA NANASI (MAHITAJI)
1. ENEO
Hapa kuna aina mbili za maeneo ya kuanzishia kilimo cha nanasi
i-Shamba jipya, hili ni lile jipya ambalo utaanza kukata miti n.k
ii-Shamba la zamani ambalo hili lilishalimwa limwa
Mashamba yote haya yanapatikana kwa namna mbili
i-Kukodi (laki tano kwa miaka mitano)
ii-Kununua (inategemea ubora wa ardhi, na umbali kutoka kwenye lami)
Kwanini tunaangalia umbali?
Tunaangalia umbali ili isije kusumbua wakati wa kuuza kulileta sokoni. Hivyo umbali ni kitu cha msingi na kujua miundombinu kunafikika kipindi cha mvua.
NB: Tunashauri kama unaanza na hauna hela anza kukodi ila ukinunua ni nzuri zaidi..
2. MBEGU
Kwa kawaida mbegu moja inauzwa wastani wa Tsh 20- 35 inategeemea na wakati kuna muda huwa chini kuna muda hupanda ila haizidi hapo.
Ni bora ukachukua mbegu za wastani na siyo ndogo sana au kubwa sana siyo nzuri kabisa kuzitumia...
Kwa shamba la hekari moja huitaji miche elfu 18 kwa upandaji wa kisasa au hata elfu 16. Tunapanda hivi ili isaidie kupata mananasi makubwa.
GHARAMA ZA KUPANDA
Mbegu tsh 35 × 18000
Kuvunja mbegu baada ya kununua tsh 10 × 18000
Kupakia kwenye gari na kushusha tsh 4 × 18000
Kupanda baada mbegu kufika shamba tsh 50 × 18000
MAANDALIZI YA SHAMBA
Kukodi laki tano
Kusafisha Tsh 80000
Trekta Tsh 50000
NB: Gharama za mbegu ni za mara moja tu mwanzoni unapoanza baada ya hapo zitakuwa zinajizalisha zenye kwahiyo utakuwa nyingine unauza na wewe pia utatumia za kukutosha..
PALIZI
Mpaka unavuna nanasi linahitaji si chini ya pali saba mpaka kumi
CHANGAMOTO ZA KILIMO
Hakuna jambo linalokosa changamoto ila kwa bahati nzuri zao hili halina changamoto ya wadudu wala sijui mvua hakuna nanasi hata iweje lazima liote tu hata kama utakisusa changamoto kubwa ni mbili au tatu...
1. Usimamizi mbovu
2. Ukosefu wa huduma kwa wakati
3. Kwenda kombo kwa soko(ila kwa ulimaji wa kisasa ni rahisi kuliepuka hili)
Muendelezo soma - Muendelezo soma hapa