1. Ukipenda sipopendwa, adhabu wajitakia,
Moyo utapondwapondwa, maradhi wajitakia,
Utachekwa na watawa, aibu itatukia,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
2. Usilazimishe kupenda, majuto yatakujia,
Mtima utakupinda, ubovu utaingia,
Wajuzi watakuwinda, wakubeze kwenye njia
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
3. Mpende mwenye kupenda, mwache asiyekupenda,
Usishindane mshinda, dhalili itakudenda,
Ghadhabu itakuwinda, kama kamanda wa kanda,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
4. Meseji utazituma, vocha nazo hupeleka,
Utabaki uyatima, faida hutaidaka,
Utaingia gharama, ukose hata nafaka,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
5. Mtaani utabezwa, vijiweni utangazwe,
Hutakosa kubatizwa, buzi jina utawazwe,
Wataikosa na dawa, ili japo utulizwe,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
Nimeandika shairi hili kuwaonya wale wanaolazimisha kupenda/kupendwa kwani majuto, kuvunjwa moyo, kukatishwa tama na hata kudhalilishwa na kupotezewa muda na pesa ni sehemu ya adha wanazokumbana nazo siku hadi siku. Lazima ujenge utaratibu wa kutathmini mahusiano yako na mpenzi wako kama yana ufanisi na faida kwako.
Moyo utapondwapondwa, maradhi wajitakia,
Utachekwa na watawa, aibu itatukia,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
2. Usilazimishe kupenda, majuto yatakujia,
Mtima utakupinda, ubovu utaingia,
Wajuzi watakuwinda, wakubeze kwenye njia
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
3. Mpende mwenye kupenda, mwache asiyekupenda,
Usishindane mshinda, dhalili itakudenda,
Ghadhabu itakuwinda, kama kamanda wa kanda,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
4. Meseji utazituma, vocha nazo hupeleka,
Utabaki uyatima, faida hutaidaka,
Utaingia gharama, ukose hata nafaka,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
5. Mtaani utabezwa, vijiweni utangazwe,
Hutakosa kubatizwa, buzi jina utawazwe,
Wataikosa na dawa, ili japo utulizwe,
Usilazimishe penzi, hata kama umependa.
Nimeandika shairi hili kuwaonya wale wanaolazimisha kupenda/kupendwa kwani majuto, kuvunjwa moyo, kukatishwa tama na hata kudhalilishwa na kupotezewa muda na pesa ni sehemu ya adha wanazokumbana nazo siku hadi siku. Lazima ujenge utaratibu wa kutathmini mahusiano yako na mpenzi wako kama yana ufanisi na faida kwako.