Usichonge sana kwenye malavidavi

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,149
Unachonga sana!



Ndoa nzuri huanza na watu wawili lonely, wakati mwingine huanza na wawili wasiojua kuongea (communicate) na baadae wakawa wazuri zaidi.

Je kuna njia yoyote ambayo mwanamke anaweza kufanya mume wake aongee kama hataki kuongea naye?

Ukweli siku zote ukitaka kuleta mabadiliko ni wewe mwenyewe kuanza kujiangalia kwenye kioo (yaani kwa kujiangalia mwenyewe).

Na jambo la msingi ni mwanamke mwenyewe kujiuliza je unaongea sana, je unachonga sana.
Wakati mwingine tunaweza kumasaidia mtu mwingine kuongea hasa kwa sisi wenyewe kupiga zip kwenye midomo yetu.

Wapo wanawake huongea kama kasuku muda wote na hii ni mbaya sana kwa mwanaume yeyote.
Kama hujajua kama wewe ni mwongeaji kuliko kawaida ukitaka kujichunguza basi angalia ukiwa na rafiki zako au ukiwa na mumeo unaongea asilimia ngapi ya maongezi kama ni asilimia 51 basi ina maana you talk too much.

Jambo la pili ni kuangalia unaongelea topic gani au ni topic zipi huwa zinatawala maongezi yako? Na je maongezi yako ni kuhusu wewe mwenyewe tu, au maongezi yako ni nyimbo ambazo mumeo hazipendi.

Jambo la tatu je unaongea topic za wanawake tu?
Hakuna mwanaume ambaye atavumilia kusikiliza women stuff muda wote au feminine stuff all the time.
Hivyo ni muhimu kuangalia subject na muda unaotumia kuongea.
Jambo lingine la msingi ni wewe mwanamke kujifunza vitu ambavyo huweza ku turn off mwanaume na asiongee na wewe​
 
"Marriage is our last, best chance to grow up."
 
Back
Top Bottom