mzee wa mkeka
Senior Member
- Mar 12, 2017
- 142
- 236
Habari wadau wa jf na wote mnaopita humu kupata habari; kama heading ilivyo hapo juu ninaushahidi ambao nitauambanisha hapa kudhihilisha kwamba kampuni ya vodacom tanzania inawaibia muda wa hewani wa wateja bila hata mteja kutumia simu kwa huduma yeyote ile.
Kabla sijaelezea kwanza niweke wazi kwamba mimi sina maslahi yeyote na kampuni yeyote ya mawasiliano ya simu tanzania au nje ya tanzania; sinufaiki kwa namna yeyote moja kwa moja au hata bila kuwa moja kwa moja na biashara hiyo. Turudi kwenye mada sasa.
Mimi ni mteja wa vodacom tanzania kwa zaidi ya miaka 12 sasa; pamoja na laini ya simu ya vodacom natumia pia lines za mitandao mingine kwa mawasiliano. Na kulingana na sintofahamu iliyonikuta kama miaka 4 nyuma ya kutokuelewa vyema muda wa hewani `unavyopotea` na vifurushi vyao vinavyoyoyoma binafsi niliamua kuendelea kutumia vodacom kwa kupokea simu na sms na pia huduma yao ya MPESA na karibuni kwa mobile banking. Hii imepelekea niwe naweka vocha/muda wa hewani kidogo kadri inavyowezekana kwa sababu huwa naona salio lolote linalobakia kwenye simu linaendelea kupungua tu na kwisha kabisa baada ya siku kadhaa bila kuitumia simu kwa huduma yeyote.
Hivyo kwa huduma ya mobile banking nalazimika kuweka `vocha` kiasi; sasa kimbembe ni pale airtime inayosalia inavyokata na kuisha kabisa bila hata kutumia simu kwa huduma yeyote ile na bila `kuwasha data`. Binafsi naomba TCRA na mamlaka zingine mtusaidie hii mitandao ya simu inatuibia waziwazi. Naweka ushahidi hapa chini;
Hii hapa chini ni screenshot ya salio ya tarehe 23/01/2018. Hapa niliweka vocha ya 2,000 nikaingia mobile banking ndipo likabakia hilo salio.
Picha ya chini hapa ni screenshot ya salio tarehe 23/01/2018; siku hiyohiyo baada ya kutumia huduma ya MPESA . Salio halikubadilika.
Picha inayofuata hapa chini ni screenshot ya salio jioni ya siku hiyohiyo 23/01/2018; salio halijapungua. Baada ya hapa nilizima simu.
Picha inayofuata hapa chini ni screenshot ya salio siku iliyofuata tarehe 24/01/2018; Bila kutumia huduma yeyote salio likayeyuka hadi sh. 528. Ilistaajabisha sana.
Na picha ya inayomalizia kwa sasa ni screenshot ya tarehe 28/01/2018. Wamebakiza sh. 3. Angalia hapa;
Kwa leo naomba niishie hapa; Ila nitaendelea leta ushahidi mwingine. Kwa sasa kuna salio nimeweka na nascreenshot salio kila siku asubuhi na jioni bila simu kutumika. Natunza kumbukumbu vyema nataka wakimaliza ifyeka yote niende huduma kwa wateja vodacom niwaombe waangalie kwenye mfumo wao hayo matumizi baada ya hapo nitaleta mrejesho hapa.
Niombe pia kwa yeyote aliyeibiwa muda wa hewani na mtandao wa simu aunganishe ushahidi hapa ili kilio kifike vyema. Pia natambua tabia ya waajiriwa wa kampuni husika kualikana kuja kushambulia uzi wanauona unaanika udhaifu wa kampuni yao; nawakaribisha na wao pia waje `wapoze` hapa. Pia natambua jibu lao la utakuwa uliwasha data kila mara wanavyoulizwa kuhusu kupungua kwa salio kusikoeleweka. Hilo kwangu halipo.
Kuna siku desemba mwaka jana vodacom walimeza 6000 ya muda wa hewani niliouacha kwenye simu. Nilifikiri sana kwa idadi ya wateja walionao kama wanakwapua hivi kila mwezi wanaingiza pesa kiasi gani kwa huu wizi? Tunaomba TCRA na mamlaka nyingine zinazolinda walaji zitulinde wananchi.
Nawasilisha kwa michango
Kabla sijaelezea kwanza niweke wazi kwamba mimi sina maslahi yeyote na kampuni yeyote ya mawasiliano ya simu tanzania au nje ya tanzania; sinufaiki kwa namna yeyote moja kwa moja au hata bila kuwa moja kwa moja na biashara hiyo. Turudi kwenye mada sasa.
Mimi ni mteja wa vodacom tanzania kwa zaidi ya miaka 12 sasa; pamoja na laini ya simu ya vodacom natumia pia lines za mitandao mingine kwa mawasiliano. Na kulingana na sintofahamu iliyonikuta kama miaka 4 nyuma ya kutokuelewa vyema muda wa hewani `unavyopotea` na vifurushi vyao vinavyoyoyoma binafsi niliamua kuendelea kutumia vodacom kwa kupokea simu na sms na pia huduma yao ya MPESA na karibuni kwa mobile banking. Hii imepelekea niwe naweka vocha/muda wa hewani kidogo kadri inavyowezekana kwa sababu huwa naona salio lolote linalobakia kwenye simu linaendelea kupungua tu na kwisha kabisa baada ya siku kadhaa bila kuitumia simu kwa huduma yeyote.
Hivyo kwa huduma ya mobile banking nalazimika kuweka `vocha` kiasi; sasa kimbembe ni pale airtime inayosalia inavyokata na kuisha kabisa bila hata kutumia simu kwa huduma yeyote ile na bila `kuwasha data`. Binafsi naomba TCRA na mamlaka zingine mtusaidie hii mitandao ya simu inatuibia waziwazi. Naweka ushahidi hapa chini;
Hii hapa chini ni screenshot ya salio ya tarehe 23/01/2018. Hapa niliweka vocha ya 2,000 nikaingia mobile banking ndipo likabakia hilo salio.
Picha ya chini hapa ni screenshot ya salio tarehe 23/01/2018; siku hiyohiyo baada ya kutumia huduma ya MPESA . Salio halikubadilika.
Picha inayofuata hapa chini ni screenshot ya salio jioni ya siku hiyohiyo 23/01/2018; salio halijapungua. Baada ya hapa nilizima simu.
Picha inayofuata hapa chini ni screenshot ya salio siku iliyofuata tarehe 24/01/2018; Bila kutumia huduma yeyote salio likayeyuka hadi sh. 528. Ilistaajabisha sana.
Na picha ya inayomalizia kwa sasa ni screenshot ya tarehe 28/01/2018. Wamebakiza sh. 3. Angalia hapa;
Kwa leo naomba niishie hapa; Ila nitaendelea leta ushahidi mwingine. Kwa sasa kuna salio nimeweka na nascreenshot salio kila siku asubuhi na jioni bila simu kutumika. Natunza kumbukumbu vyema nataka wakimaliza ifyeka yote niende huduma kwa wateja vodacom niwaombe waangalie kwenye mfumo wao hayo matumizi baada ya hapo nitaleta mrejesho hapa.
Niombe pia kwa yeyote aliyeibiwa muda wa hewani na mtandao wa simu aunganishe ushahidi hapa ili kilio kifike vyema. Pia natambua tabia ya waajiriwa wa kampuni husika kualikana kuja kushambulia uzi wanauona unaanika udhaifu wa kampuni yao; nawakaribisha na wao pia waje `wapoze` hapa. Pia natambua jibu lao la utakuwa uliwasha data kila mara wanavyoulizwa kuhusu kupungua kwa salio kusikoeleweka. Hilo kwangu halipo.
Kuna siku desemba mwaka jana vodacom walimeza 6000 ya muda wa hewani niliouacha kwenye simu. Nilifikiri sana kwa idadi ya wateja walionao kama wanakwapua hivi kila mwezi wanaingiza pesa kiasi gani kwa huu wizi? Tunaomba TCRA na mamlaka nyingine zinazolinda walaji zitulinde wananchi.
Nawasilisha kwa michango