OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,246
- 103,949
Binafsi najua limbwata lipo. Mtu akipigwa limbwata anafanya vitu ambavyo watu watamshangaa na yeye unawashangaa kwanini wanamshangaa. Omba sana katika harakati zako za mapenzi usipigwe limbwata.
Waambie ndugu na masela wakiona umepigwa kitu wakushtue, ukiwa mbishi wakubebe kinguvu wakupeleke kwenye maombi au kwa mtaalamu. Unakuwa hujijui.
Kuna baadhi wanasema hakuna limbwata ila ni mambo ya kufikirika. Bali unakuwa umewekwa tu kwenye angle nzuri ya mapenzi.
Waambieni ukweli hapa. Libwata lipo au halipo? Wapeni ushuhuda. Ila mimi nasema limbwata lipo. Nimelikwepa mara kadhaa kutoka kwa michepuko
Mshana Jr