Ushauri wangu kwa bondia Shabani Kaoneka

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,634
697,929
Naandika haya baada ya kuibukia huko Arusha kwa kiongozi mmoja wa dini mwenye utata mwingi akitafuta kuombewa kwakuwa anajihisi ana mikosi, mambo yake hayaendi na pengine kuna watu wamemsagia kunguni kiroho kiroho na kimwili.

Kwenda kutafuta tiba (ya kiroho) kwa kiongozi wa kidini sio tatizo kabida! Ishu ni kwamba unakwenda kwa nani? Matatizo binafsi huwa hayatatuliwi mbele ya camera na macho ya watu.

Shabani anaumia sana kuona mpinzani wake Mandonga aliyemchakaza kwa TKO aking'ara na kuwa maarufu kuliko yeye..kuna vitu vya kujifunza hapa ambavyo pengine Kaoneka hajavijua bado.

Pamoja na kwamba Shabani Kaoneka ameathiriwa na kabila! Dhana ya kupenda HAKI! Lakini kuna haya pia.

1. Kuteleza si kuanguka

Kipigo chake kwa mandonga kilimpa ushindi sawa kabisa, lakini mpinzani wake akaweka nia, kipigo kilimjeruhi mwili sio nafsi akajiona ana nafasi ya kusimama tena na kusonga mbele. Kwa hili Mandonga ni mshindi.

2. Kukunjua nafsi
Nafsi iliyokunjamana haina nuru na huleta giza usoni, nafsi iliyokunjamana imejaa maumivu, sononi na taharuki
Nafsi iliyokunjamana huleta uzito wa kimwili na kiroho pia! Ushindi wa ulingoni haimaanishi ni ushindi wa maisha. Kuendelea kusononeka kwamba mshindwa wako anapata support kubwa kuliko wewe hakutakusaidia zaidi ya kuzidi kukudidimiza.

3. Mlikutana na mpinzani wako jukwaani
Wewe tayari ukiwa ni bondia wa siku nyingi na ukicheza kwa mazoea kama siku zote za nyuma! Unashinda ama unashindwa na maisha yanasonga, hakuna zaidi.

Mpinzani wako kaingia ulingoni akiwa kapania kusonga mbele na pengine kulitumia pambano lenu kama njia yake ya kutokea bila kujali atashindwa ama atashinda. Mawio na machweo vilikutana. Determination ni kitu kikubwa sana katika maisha.

4. Watu
Kaoneka ogopa sana kiumbe kinaitwa binadamu, siyo wakweli, siyo wema, hawana huruma, wamejawa na unafiki na ghiliba. Kitendo cha kuongea ya moyoni kuhusu mpinzani wako mbele ya watu kimekubomoa badala ya kukujenga! Hao watu ndio pembeni wanakuita kila jina baya. Kamwe katika maisha yako usioneshe maumivu yako mbele ya hadhira

5. Kipimo katika maisha
Kila mtu ana kipimo chake katika maisha, na kila mtu ana nyakati zake za kupata! Hupaswi kuumia sana kwakuwa hujui kipimo chako ni kipi na umeandikiwa nini na kwa wakati gani!

Kuna wenye elimu kubwa lakini ni maskini wa kutupwa lakini kuna standard zero halafu maisha yao ni neema tupu. Kuna ambao wamesota sana na maisha lakini mpaka leo wanasugua gaga! Na kuna waliogusa kidogo tu halafu ikaitika!

6. Haiba

Kaoneka haiba yako ni ukimya na upole na unaishi katika uhalisia sio mtu wa maneno na kelele nyingi.. Haiba huponza na kuathiri wengi. Mpinzani wako ni tofauti kabisa na wewe, background zenu ndio zimewapa matokeo ya sasa!

7. Kuna ishu za kifamilia ukoo nk
Kuna baadhi ya familia hata zipambane vipi kutoboa ni ishu kwakuwa tayari kuna limitations za kiroho wamewekewa.

Kitendo chako cha kuibukia Arusha kwa nabii kina mengi ya kuangazia, pengine hata yule muimba singeli aliyepewa gari kuna mahusiano. Lakini Kaoneka ogopa sana vitu vinavyofanyika mbele ya kamera vina mengi nyuma yake!

Mimi niishie hapa! Ninachoweza kukushauri usijilize wala kulalama tena mbele ya hadhira. Jitenge na haya maisha ya 'macho' ya viumbe wanaoitwa binadamu. Tiba yako unayo mwenyewe, katafute chumvi yako ya mawe itakutoa kutoka kwenye kuonekana mpaka kuonekana kama jina lako lilivyo.

Nakuombea.

 
Ule ulikua wakati wa mandonga kubarikiwa haijalishi Kwa namna Gani. Kaoneka awe mtulivu ukifika wakati wake atapiga kazi mpaka mikono iote sugu + mapambano nje ya nchi.

Ushauri Kwa mandonga, ngoma huvuma na mwisho hupasuka. Umaarufu unafika kikomo akiendekeza anasa yatamkuta ya Mike Tyson
 
Ule ulikua wakati wa mandonga kubarikiwa haijalishi Kwa namna Gani. Kaoneka awe mtulivu ukifika wakati wake atapiga kazi mpaka mikono iote sugu + mapambano nje ya nchi.

Ushauri Kwa mandonga, ngoma huvuma na mwisho hupasuka. Umaarufu unafika kikomo akiendekeza anasa yatamkuta ya mike tyson
Na ajihadhari sana na chawa na akina Delilah
 
Bro ujumbe mzuri mno madini ya ukweli sana. Halafu kaoneka hajajua kuwa nyota ya Mandonga sio kupigwa au kupiga kwake, umaarufu wa Mandonga ni kama ngoma ambayo ilizimwa nguvu baada ya kunyeshewa Mvua, fursa ya kkuonekana kwenye masumbwi Kwa Mandonga alopewa na kapten Ssemuju promoter wa ngumi ndio imempaisha mandonga, Mandonga anakipawa Cha kuongea, kumbukumbu, akili sharp ya kushika vitu kichwani.

Mandonga anakipiji Cha marketing na promotion, kabla ya pambano lao la Songea mandoga ashakuwa maarufu kupitia Tambo zake kuelekea hilo pambano kipande cha ha video cha Tambo za Mandonga ndio kilivuta hisia na kuleta mvuto wa pambano lile na mchezo wa ngumi kwa ujumla, aina ya uongeaji wake, kipawa chake, majigambo, kujiamini, vijembe na mipasho kwa mpinzani, mikwara, misemo ya lugha na ubunifu ndio nguzo ya Mandonga na umaarufu wake, sauti ya kusikika, energy ya kuongea, fursa ambayo waandishi wameiona kwake hupata win-win.

Kaoneka hawezi kuwa Mandonga kamwe, upiga debe na hustle za Mandonga za stendi na ugumu wa maisha stendi yenye ubabe, kelele, ushawishi Kwa abiria zimemjenga.

Brand ya Mandonga ni long time kitambo ila haikuwa na broader scope ya kuwa captured kwenye broadcasting, social medias na digital platforms zote.

Mandonga alikosa visibility na popularity ya critical mass hasa mileages cover. Kaoneka anatumia akili finyu iliozoeleka ya aina ya legendary jealous kwa underdogs katika maisha.

Multi talented Mandonga Mtu kazi, the athlet, the comedian, the promoter, the visionary, the magnetic being, the Viber of his own making, the most resilient being, a man with UN imaginable courage with no despair, full of hopes.

Kuna mengi ya kuongea acha niishie hapa.

Blessings to Mandonga

Wadiz
 
Bro ujumbe mzuri mno madini ya ukweli sana. Halafu kaoneka hajajua kuwa nyota ya Mandonga sio kupigwa au kupiga kwake, umaarufu wa Mandonga ni kama ngoma ambayo ilizimwa nguvu baada ya kunyeshewa Mvua, fursa ya kkuonekana kwenye masumbwi Kwa Mandonga alopewa na kapten Ssemuju promoter wa ngumi ndio imempaisha mandonga, Mandonga anakipawa Cha kuongea, kumbukumbu, akili sharp ya kushika vitu kichwani.
Kaoneka hawezi kuwa Mandonga kamwe, upiga debe na hustle za Mandonga za stendi na ugumu wa maisha stendi yenye ubabe, kelele, ushawishi Kwa abiria zimemjenga.
 
Bro ujumbe mzuri mno madini ya ukweli sana. Halafu kaoneka hajajua kuwa nyota ya Mandonga sio kupigwa au kupiga kwake, umaarufu wa Mandonga ni kama ngoma ambayo ilizimwa nguvu baada ya kunyeshewa Mvua, fursa ya kkuonekana kwenye masumbwi Kwa Mandonga alopewa na kapten Ssemuju promoter wa ngumi ndio imempaisha mandonga, Mandonga anakipawa Cha kuongea, kumbukumbu, akili sharp ya kushika vitu kichwani.

Mandonga anakipiji Cha marketing na promotion, kabla ya pambano lao la Songea mandoga ashakuwa maarufu kupitia Tambo zake kuelekea hilo pambano kipande cha ha video cha Tambo za Mandonga ndio kilivuta hisia na kuleta mvuto wa pambano lile na mchezo wa ngumi kwa ujumla, aina ya uongeaji wake, kipawa chake, majigambo, kujiamini, vijembe na mipasho kwa mpinzani, mikwara, misemo ya lugha na ubunifu ndio nguzo ya Mandonga na umaarufu wake, sauti ya kusikika, energy ya kuongea, fursa ambayo waandishi wameiona kwake hupata win-win.

Kaoneka hawezi kuwa Mandonga kamwe, upiga debe na hustle za Mandonga za stendi na ugumu wa maisha stendi yenye ubabe, kelele, ushawishi Kwa abiria zimemjenga.

Brand ya Mandonga ni long time kitambo ila haikuwa na broader scope ya kuwa captured kwenye broadcasting, social medias na digital platforms zote.

Mandonga alikosa visibility na popularity ya critical mass hasa mileages cover. Kaoneka anatumia akili finyu iliozoeleka ya aina ya legendary jealous kwa underdogs katika maisha.

Multi talented Mandonga Mtu kazi, the athlet, the comedian, the promoter, the visionary, the magnetic being, the Viber of his own making, the most resilient being, a man with UN imaginable courage with no despair, full of hopes.

Kuna mengi ya kuongea acha niishie hapa.

Blessings to Mandonga


Wadiz
Brand ya Mandonga ni long time kitambo ila haikuwa na broader scope ya kuwa captured kwenye broadcasting, social medias na digital platforms zote.

Mandonga alikosa visibility na popularity ya critical mass hasa mileages cover. Kaoneka anatumia akili finyu iliozoeleka ya aina ya legendary jealous kwa underdogs katika maisha.
 
Kipimo katika maisha

Kila mtu ana kipimo chake katika maisha, na kila mtu ana nyakati zake za kupata! Hupaswi kuumia sana kwakuwa hujui kipimo chako ni kipi na umeandikiwa nini na kwa wakati gani!

Kuna wenye elimu kubwa lakini ni maskini wa kutupwa lakini kuna standard zero halafu maisha yao ni neema tupu. Kuna ambao wamesota sana na maisha lakini mpaka leo wanasugua gaga! Na kuna waliogusa kidogo tu halafu ikaitika!
 
Napenda kutolea ufafanuzi juu ya hili nilipewa Zawadi ya gari na mtumishi anayejiita Nabii Mkuu na sio hiyo gari mnayoiona kwenye picha ila utata umekuja pale ambapo watu wa George kasambale wanapohitaji nije kushukuru kanisani kila wakati Siwezi pia mm nina magari mengi tu
20230204_035506.jpg
 
Mkuu, kina zile dawa za kufanya ngumi iwe nzito.

Pia mfanyie wema kwa kumpa dawa za mvuto, umfushe na kumuosha mikosi.
Naandika haya baada ya kuibukia huko Arusha kwa kiongozi mmoja wa dini mwenye utata mwingi akitafuta kuombewa kwakuwa anajihisi ana mikosi, mambo yake hayaendi na pengine kuna watu wamemsagia kunguni kiroho kiroho na kimwili.

Kwenda kutafuta tiba (ya kiroho) kwa kiongozi wa kidini sio tatizo kabida! Ishu ni kwamba unakwenda kwa nani? Matatizo binafsi huwa hayatatuliwi mbele ya camera na macho ya watu.

Shabani anaumia sana kuona mpinzani wake Mandonga aliyemchakaza kwa TKO aking'ara na kuwa maarufu kuliko yeye..kuna vitu vya kujifunza hapa ambavyo pengine Kaoneka hajavijua bado.

Pamoja na kwamba Shabani Kaoneka ameathiriwa na kabila! Dhana ya kupenda HAKI! Lakini kuna haya pia.

1. Kuteleza si kuanguka
Kipigo chake kwa mandonga kilimpa ushindi sawa kabisa, lakini mpinzani wake akaweka nia, kipigo kilimjeruhi mwili sio nafsi akajiona ana nafasi ya kusimama tena na kusonga mbele. Kwa hili Mandonga ni mshindi.

2. Kukunjua nafsi
Nafsi iliyokunjamana haina nuru na huleta giza usoni, nafsi iliyokunjamana imejaa maumivu, sononi na taharuki
Nafsi iliyokunjamana huleta uzito wa kimwili na kiroho pia! Ushindi wa ulingoni haimaanishi ni ushindi wa maisha. Kuendelea kusononeka kwamba mshindwa wako anapata support kubwa kuliko wewe hakutakusaidia zaidi ya kuzidi kukudidimiza.

3. Mlikutana na mpinzani wako jukwaani
Wewe tayari ukiwa ni bondia wa siku nyingi na ukicheza kwa mazoea kama siku zote za nyuma! Unashinda ama unashindwa na maisha yanasonga, hakuna zaidi.

Mpinzani wako kaingia ulingoni akiwa kapania kusonga mbele na pengine kulitumia pambano lenu kama njia yake ya kutokea bila kujali atashindwa ama atashinda. Mawio na machweo vilikutana. Determination ni kitu kikubwa sana katika maisha.

4. Watu
Kaoneka ogopa sana kiumbe kinaitwa binadamu, siyo wakweli, siyo wema, hawana huruma, wamejawa na unafiki na ghiliba. Kitendo cha kuongea ya moyoni kuhusu mpinzani wako mbele ya watu kimekubomoa badala ya kukujenga! Hao watu ndio pembeni wanakuita kila jina baya. Kamwe katika maisha yako usioneshe maumivu yako mbele ya hadhira

5. Kipimo katika maisha
Kila mtu ana kipimo chake katika maisha, na kila mtu ana nyakati zake za kupata! Hupaswi kuumia sana kwakuwa hujui kipimo chako ni kipi na umeandikiwa nini na kwa wakati gani!

Kuna wenye elimu kubwa lakini ni maskini wa kutupwa lakini kuna standard zero halafu maisha yao ni neema tupu. Kuna ambao wamesota sana na maisha lakini mpaka leo wanasugua gaga! Na kuna waliogusa kidogo tu halafu ikaitika!

6. Haiba
Kaoneka haiba yako ni ukimya na upole na unaishi katika uhalisia sio mtu wa maneno na kelele nyingi.. Haiba huponza na kuathiri wengi. Mpinzani wako ni tofauti kabisa na wewe, background zenu ndio zimewapa matokeo ya sasa!

7. Kuna ishu za kifamilia ukoo nk
Kuna baadhi ya familia hata zipambane vipi kutoboa ni ishu kwakuwa tayari kuna limitations za kiroho wamewekewa.

Kitendo chako cha kuibukia Arusha kwa nabii kina mengi ya kuangazia, pengine hata yule muimba singeli aliyepewa gari kuna mahusiano. Lakini Kaoneka ogopa sana vitu vinavyofanyika mbele ya kamera vina mengi nyuma yake!

Mimi niishie hapa! Ninachoweza kukushauri usijilize wala kulalama tena mbele ya hadhira. Jitenge na haya maisha ya 'macho' ya viumbe wanaoitwa binadamu. Tiba yako unayo mwenyewe, katafute chumvi yako ya mawe itakutoa kutoka kwenye kuonekana mpaka kuonekana kama jina lako lilivyo.

Nakuombea.

View attachment 2493528
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom