Bushmamy
JF-Expert Member
- Aug 18, 2019
- 8,848
- 15,253
Waungwana wa Jf,
Nimetoka mkoa ninaoishi nikasafiri mkoa mwingine kwa ajili ya mapumziko na kuweka akili sawa. Nyumbani nikimuacha binti wa kazi ambae nimekaa naye kwa muda wa mwaka mmoja sasa, ni binti mchapakazi, na asiye na kiburi na pia ni msafi sana, shida yake kubwa ilikuwa akiwa na mwanaume huyu akiachana nae ndani ya wiki anaye mwingine. Nilimuonya sana lakini ndo hivo, nikapiga simu kwa wazazi wake wakamuonya wala hakusikia.
Basi tukaamua tumuache kama alivyo ilmradi wajibu wake nyumbani anautimiza kwangu haikuwa shida, maisha yanaendelea.
Nikiwa huku ile wiki ya kwanza mwishoni napata simu kutoka kwa jirani 'Bushmamy kwema huko? Nikamjibu Nipo salama, akaendelea kusema kuwa binti yako ni mjamzito na inaonekana ana mimba ya miezi miwili maana alivyokuja hapa kwangu alisema ana kama miezi miwili hajaona siku zake, ndo nikamshauri akanunue kipimo kucheki ni Mimba tayari kinaonyesha"'akamaliza kuongea tukaagana.
Basi bwana mi nikaagiza Kilimanjaro ya baridi nikapiga pafu 4 ndo nikaanza kutafakari nafanyeje kwa sababu niliwaza yafuatayo:
Huyu binti nilimpenda tu vile hakuwa na kiburi.
Pili ni mchapakazi na msafi
Tatu kule kwao wanamtegemea kila mwezi atume hela ya kusaidia wazazi.
Nne ni mvumilivu katika hali zote za kiuchumi ninazopitia, na pia ni muaminifu sana hana tamaa na hela.
Pamoja na mambo mengine mengi tu maana nilipanga kuishi naye kabisa kama mdogo wangu ili baadaye nimpeleke ufundi cherehani au nimtafutie kazi lakini mambo ndo yameshakuwa hivyo maana hata hajui mimba ni ya nani.
Hadi sasa sijamwambia kama najua chochote kuhusu hali yake nasubiri nirudi.
Naombeni ushauri tafadhali maana binti ana miaka 20.
Nimetoka mkoa ninaoishi nikasafiri mkoa mwingine kwa ajili ya mapumziko na kuweka akili sawa. Nyumbani nikimuacha binti wa kazi ambae nimekaa naye kwa muda wa mwaka mmoja sasa, ni binti mchapakazi, na asiye na kiburi na pia ni msafi sana, shida yake kubwa ilikuwa akiwa na mwanaume huyu akiachana nae ndani ya wiki anaye mwingine. Nilimuonya sana lakini ndo hivo, nikapiga simu kwa wazazi wake wakamuonya wala hakusikia.
Basi tukaamua tumuache kama alivyo ilmradi wajibu wake nyumbani anautimiza kwangu haikuwa shida, maisha yanaendelea.
Nikiwa huku ile wiki ya kwanza mwishoni napata simu kutoka kwa jirani 'Bushmamy kwema huko? Nikamjibu Nipo salama, akaendelea kusema kuwa binti yako ni mjamzito na inaonekana ana mimba ya miezi miwili maana alivyokuja hapa kwangu alisema ana kama miezi miwili hajaona siku zake, ndo nikamshauri akanunue kipimo kucheki ni Mimba tayari kinaonyesha"'akamaliza kuongea tukaagana.
Basi bwana mi nikaagiza Kilimanjaro ya baridi nikapiga pafu 4 ndo nikaanza kutafakari nafanyeje kwa sababu niliwaza yafuatayo:
Huyu binti nilimpenda tu vile hakuwa na kiburi.
Pili ni mchapakazi na msafi
Tatu kule kwao wanamtegemea kila mwezi atume hela ya kusaidia wazazi.
Nne ni mvumilivu katika hali zote za kiuchumi ninazopitia, na pia ni muaminifu sana hana tamaa na hela.
Pamoja na mambo mengine mengi tu maana nilipanga kuishi naye kabisa kama mdogo wangu ili baadaye nimpeleke ufundi cherehani au nimtafutie kazi lakini mambo ndo yameshakuwa hivyo maana hata hajui mimba ni ya nani.
Hadi sasa sijamwambia kama najua chochote kuhusu hali yake nasubiri nirudi.
Naombeni ushauri tafadhali maana binti ana miaka 20.