Uongozi UVCCM waombwa kujiuzuru

fangfangjt

JF-Expert Member
Apr 25, 2008
571
139
wanachama wa UVCCM waomba uongozi wao ujiuzuru , baada ya kutoa matamko ya kukashfu viongozi wa chama na serikali wastaafu -East Africa Radio news



UPDATE

http://www.mwananchi.co.tz/habari/49-uchaguzi-mkuu/11023-makonda-sasa-ataka-uvccm-ivunjwe

Geofrey Nyangóro
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kupitia Mkoa wa Kilimanjaro, Paul Makonda, ameelezea azma yake ya kupendekeza kwa chama hicho, wazo la kutaka kuvunjwa kwa jumuiya hiyo na kuundwa upya.

Makonda ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, alisema azma hiyo inatokana na kitendo cha mafisadi kujiingiza katika jumuiya hiyo na kutumia vibaraka wao kutekeleza malengo yao ya kukihujumu chama.

Machi 28 mwaka huu, Makonda alishauri mabaraza ya jumuiya hiyo katika ngazi ya taifa na mikoa na sekretarieti zake, yajiuzulu ndani ya kipindi cha siku saba.

Hata hivyo ushauri huo ulipuuzwa.Katika mazungumzo yake ya jana, Makonda alisema baada ya kuona ushauri huo umepuuzwa, sasa anaandaa pendekezo la kutaka jumuiya hiyo, ivunjwe na kuundwa mpya.

Kwa mujibu wa kada huyo wa CCM, pendekezo hilo ataliwakilisha kwa sekretarieti mpya ya CCM.Alisema pamoja na mambo mengine, atapendekeza jumuiya hiyo mpya iitwe UV-CCM Maadili, kulingana na malengo na matakwa yake kwa vijana na chama.

"Kwenye katiba yetu ya chama, ibara ya 15 inatoa mamlaka kwa chama kuondoa, kupunguza jumuiya zake au kuongeza. Mimi nimeweka nia na nataka vijana wa CCM kote nchini kuunga mkono mchakato huu. Nitawasilisha mapendekezo ya kuanzishwa kwa jumuiya mpya ya vijana, ambayo itatimiza majukumu yote yaliyosababisha kuanzishwa kwa umoja huo,"alisema Makonda.


Alisema jambo lingine linalomsukuma kufikia uamuzi huo ni uongozi uliopo kwenye jumuiya hiyo, kushindwa kuwajibika."Baadhi ya viongozi wanadiriki kujipambanua kuwa marafiki wa mafisadi walioligharimu taifa na kusababisha athari zitakazodumu kwa miaka mingi," alisema.

"Namna pekee ya kukabiliana na tatizo hilo ni kuanzisha jumuiya hiyo mpya itakayojishughulisha na masuala ya vijana ili waweze kujiona kuwa sehemu ya CCM na wenye jukumu la kukijenga chama na kulitumikia taifa kwa uadilifu," alisisitiza.

Katika hatua nyingine, mwanachama huyo wa CCM alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuridhia mabadiliko ya sekratarieti kuu ya chama.Alisema tukio kama hilo halijawahi kutokea tangu enzi za Tanu na CCM.

Alisema hata hivyo kilichofanyika ni kuwaondoa watu dhaifu.Alisema kinachotakiwa kufanyika hivi sasa ni mabadiliko ya mfumo utakaozingatia utendaji wa kazi wa kitaalamu na kutaka chama hicho kuachana na mfumo wa kizamani wa kufanya kazi kwa mazoea.

"Sekratarieti iliyopita ilifanya kazi kwa mazoea iliteua watu kwa kutumia urafiki badala ya kuzingatia uwezo wa utendaji, ilifanya vitu kwa kusukumwa na uhitaji wa nje kuliko mikakati ya ndani na hilo ndilo lilisababisha tuhangaike kukirekebisha chama sasa,"alisema.
MWISHO
 
Mhhhhh.................

Shedding.jpg
 
Makonda sasa ataka UVCCM ivunjwe

Geofrey Nyangóro
MJUMBE wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) kupitia Mkoa wa Kilimanjaro, Paul Makonda, ameelezea azma yake ya kupendekeza kwa chama hicho, wazo la kutaka kuvunjwa kwa jumuiya hiyo na kuundwa upya.

Makonda ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, alisema azma hiyo inatokana na kitendo cha mafisadi kujiingiza katika jumuiya hiyo na kutumia vibaraka wao kutekeleza malengo yao ya kukihujumu chama.

Machi 28 mwaka huu, Makonda alishauri mabaraza ya jumuiya hiyo katika ngazi ya taifa na mikoa na sekretarieti zake, yajiuzulu ndani ya kipindi cha siku saba.

Hata hivyo ushauri huo ulipuuzwa.Katika mazungumzo yake ya jana, Makonda alisema baada ya kuona ushauri huo umepuuzwa, sasa anaandaa pendekezo la kutaka jumuiya hiyo, ivunjwe na kuundwa mpya.

Kwa mujibu wa kada huyo wa CCM, pendekezo hilo ataliwakilisha kwa sekretarieti mpya ya CCM.Alisema pamoja na mambo mengine, atapendekeza jumuiya hiyo mpya iitwe UV-CCM Maadili, kulingana na malengo na matakwa yake kwa vijana na chama.

"Kwenye katiba yetu ya chama, ibara ya 15 inatoa mamlaka kwa chama kuondoa, kupunguza jumuiya zake au kuongeza. Mimi nimeweka nia na nataka vijana wa CCM kote nchini kuunga mkono mchakato huu. Nitawasilisha mapendekezo ya kuanzishwa kwa jumuiya mpya ya vijana, ambayo itatimiza majukumu yote yaliyosababisha kuanzishwa kwa umoja huo,"alisema Makonda.


Alisema jambo lingine linalomsukuma kufikia uamuzi huo ni uongozi uliopo kwenye jumuiya hiyo, kushindwa kuwajibika."Baadhi ya viongozi wanadiriki kujipambanua kuwa marafiki wa mafisadi walioligharimu taifa na kusababisha athari zitakazodumu kwa miaka mingi," alisema.

"Namna pekee ya kukabiliana na tatizo hilo ni kuanzisha jumuiya hiyo mpya itakayojishughulisha na masuala ya vijana ili waweze kujiona kuwa sehemu ya CCM na wenye jukumu la kukijenga chama na kulitumikia taifa kwa uadilifu," alisisitiza.

Katika hatua nyingine, mwanachama huyo wa CCM alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuridhia mabadiliko ya sekratarieti kuu ya chama.Alisema tukio kama hilo halijawahi kutokea tangu enzi za Tanu na CCM.

Alisema hata hivyo kilichofanyika ni kuwaondoa watu dhaifu.Alisema kinachotakiwa kufanyika hivi sasa ni mabadiliko ya mfumo utakaozingatia utendaji wa kazi wa kitaalamu na kutaka chama hicho kuachana na mfumo wa kizamani wa kufanya kazi kwa mazoea.

"Sekratarieti iliyopita ilifanya kazi kwa mazoea iliteua watu kwa kutumia urafiki badala ya kuzingatia uwezo wa utendaji, ilifanya vitu kwa kusukumwa na uhitaji wa nje kuliko mikakati ya ndani na hilo ndilo lilisababisha tuhangaike kukirekebisha chama sasa,"alisema.
MWISHO
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom