-umiza moyo.....

Sanda Matuta

JF-Expert Member
May 9, 2007
949
134
Namshukuru mwenyezi,sifa na takbira.
Labana afanya kazi,akifata yake dira.
Humpa naye mridhi,jazha nema ongezea.
Humnyima kwa uwazi,yule anaye mkusudia.
Huyu ndio Mwenyezi,Mungu tunaye msujudia.

Mbingu yake ardhi,kwa ajabu ameumba.
Adam wake mwenzi,Hawa kumuwekea.
Mwanamke akamuenzi,sifa zake jaalia.
Kwenye zake tenzi,vitabuni utakuta.
Quraani ina mengi,yale kwenye Bibilia

Hili Swali watenzi,majibu nina yatakaa.
Moyo kitu thamani,nani anza umizaa?
Turudi kule bustanini,Maisha yalipoanza
Adam kwenda porini,mwanamke aka data
Kam-ruhusu shetani,chokochoko zake leta.

Amwambia,”hakutamani,ndio maana anatoka.
Usikute ana mpenzi.huko anako kwenda.
Anafanya kama kazi,aliyoka kataza Rabuka.
Wewe ana kuhini,huku yeye ajirusha
Haya mengine mengi,kichwani aka mjaza.

Aka-umia moyoni,simanzi zika mjaa.
Moyo wake maskini,ndio ukawa wa kwanza.
Hasira ndio kiini,uchamungu kumtoka
Kulipiza aka-tamani,moyo Adamu kuvunja
Shetani haku muhini,kumpa tunda kumega.

Moyo kauumiza nani,shetani au lasulallah
Hawa akapata poni,mumewe akamtaka
Adamu yu mafunzoni,akamuhasi Rabuka.
Kwa matendo ya chumbani,wakalivunja agano
Malenga mnipe yakini,nani kauumiza moyo?
 
Last edited:
Namshukuru mwenyezi,sifa na takbira.
Labana afanya kazi,akifata yake dira.
Humpa naye mridhi,jazha nema ongezea.
Humnyima kwa uwazi,yule anaye mkusudia.
Huyu ndio Mwenyezi,Mungu tunaye msujudia.

Mbingu yake ardhi,kwa ajabu ameumba.
Adam wake mwenzi,Hawa kumuwekea.
Mwanamke akamuenzi,sifa zake jaalia.
Kwenye zake tenzi,vitabuni utakuta.
Quraani ina mengi,yale kwenye Bibilia

Hili Swali watenzi,majibu nina yatakaa.
Moyo kitu thamani,nani anza umizaa?
Turudi kule bustanini,Maisha yalipoanza
Adam kwenda porini,mwanamke aka data
Kam-ruhusu shetani,chokochoko zake leta.

Amwambia,”hakutamani,ndio maana anatoka.
Usikute ana mpenzi.huko anako kwenda.
Anafanya kama kazi,aliyoka kataza Rabuka.
Wewe ana kuhini,huku yeye ajirusha
Haya mengine mengi,kichwani aka mjaza.

Aka-umia moyoni,simanzi zika mjaa.
Moyo wake maskini,ndio ukawa wa kwanza.
Hasira ndio kiini,uchamungu kumtoka
Kulipiza aka-tamani,moyo Adamu kuvunja
Shetani haku muhini,kumpa tunda kumega.

Moyo kauumiza nani,shetani au lasulallah
Hawa akapata poni,mumewe akamtaka
Adamu yu mafunzoni,akamuhasi Rabuka.
Kwa matendo ya chumbani,wakalivunja agano
Malenga mnipe yakini,nani kauumiza moyo?


Mkulu SM

kulikoni,mbona sintofahamu kila mahara??
 
Nimetunga kwa kubuni,beti zangu nimeweka.
Malenga mlio pwani,bara hata Amerika
Nina itaka yakini,majibu yenu kupata.
Ya niingie akilini,mtima wangu tulizaa
Binaadamu na Shetani,nani moyo kauumizaa?
 
Nimetunga kwa kubuni,beti zangu nimeweka.
Malenga mlio pwani,bara hata Amerika
Nina itaka yakini,majibu yenu kupata.
Ya niingie akilini,mti wangu tulizaa
Binaadamu na Shetani,nani moyo kauumizaa?

unakaribia mwaka sasa,hamna wakujibu,Mkuu sanda jibu mwenyewe lete vituz.........
 
Moyo uloumizwa,hakika wote twabuni,
Maana tunda kumeza, mwishowe ni huzuni
Hili lilishasemezwa, na mola kule bustanini
Jibulo kama waweza,huna budi kubaini,

Adam kuumbwa kwanza, Eva akaja badae
Kisa Adamu kuwaza, akaeje mwenyewe?
Rabuka akampooza,kwa kumpa mwenziwe
Hapo ikamwisha waza, pasipo mfanowe

Haikuishia hapo, wawili mle bustanini
Mola akawapa onyo,mlemle bustanini
Wakalielewa onyo,japo wasiweke manani
Ikajakuwa songo, walipokosa umakini

Joka a.k.a Shetani , saa ngapi asiwarubuni
Na vile walivyodhani, wamo daima rahani
Kumbe sivyo asilani, pembeni kuna kisirani
Ukawa ndio ushindani , joka akaingia nafsini

Na kama ilivyo ada, joka kiumbe hatari
Adam kutokuwaza , kuzingatia tahadhari
Akamwacha mamie Eva, asemeshwe na kikari
Utashangaa vipi aliweza,ilhali Adam yu askari

Tunda lilipoangazwa, hakika likavutia
Eva hamu kajazwa , Adam akampatia
Adam akapumbazwa, Tunda kalumangatia
Utasemaje kaumizwa, ilhali alijitakia?
 
Moyo uloumizwa,hakika wote twabuni,
Maana tunda kumeza, mwishowe ni huzuni
Hili lilishasemezwa, na mola kule bustanini
Jibulo kama waweza,huna budi kubaini,

Adam kuumbwa kwanza, Eva akaja badae
Kisa Adamu kuwaza, akaeje mwenyewe?
Rabuka akampooza,kwa kumpa mwenziwe
Hapo ikamwisha waza, pasipo mfanowe

Haikuishia hapo, wawili mle bustanini
Mola akawapa onyo,mlemle bustanini
Wakalielewa onyo,japo wasiweke manani
Ikajakuwa songo, walipokosa umakini

Joka a.k.a Shetani , saa ngapi asiwarubuni
Na vile walivyodhani, wamo daima rahani
Kumbe sivyo asilani, pembeni kuna kisirani
Ukawa ndio ushindani , joka akaingia nafsini

Na kama ilivyo ada, joka kiumbe hatari
Adam kutokuwaza , kuzingatia tahadhari
Akamwacha mamie Eva, asemeshwe na kikari
Utashangaa vipi aliweza,ilhali Adam yu askari

Tunda lilipoangazwa, hakika likavutia
Eva hamu kajazwa , Adam akampatia
Adam akapumbazwa, Tunda kalumangatia
Utasemaje kaumizwa, ilhali alijitakia?


WOS,
i salute!!!!!
wewe mkali mno......................!!!!
 
Back
Top Bottom