Umefaidika nini na JF tangu ulipojiunga?

Acheni utani, JF imekuwa ya msaada sana kwangu.
Nakumbuka zilikuwa zimebaki siku chache sana nifunge ndoa. Bestman wangu akawa haeleweki. Nikiwasiliana naye kuhusu mipango ya kwenda kufanya manunuzi (tena kwa ghalama zangu) ananikwepa. Nilipomkumbusha siku ya kwenda rehearsal na kubaini hatuko ukurasa mmoja nikachanganyikiwa. Haraka sana nikamkumbuka mtu mmoja aliyewahi kuniomba mchango wa harusi kwa PM hapa JF. Huyu mtu japo nilimchangia, hatukuwa tumewahi kukutana na wala hatukuwa tunajuana. Roho ikanituma kuwasiliana naye. Jibu lilikuwa, USIPATE SHIDA. Hivyo ndivyo ilivyokuwa JF ikawa imenipa Bestman and Best-friend. Asante sana JF, Udumu Milele

Mkuu nimeipenda hii.
 
JF BWANA. Kiboko ya mambo yote. Hongera all members from junior to VIP members. Idumu JF MILELE NA MILELE. Hakuna kama Great thinkers, wengine wanafuatia. God bless wana JF WOTE.
 
Mi nimewachapa nao sana wadada na wa mama wa humu.
Ukiandika tu mstari wa kunivutia, lazima nikutafutie muda nichepuke na sabuni yangu mkononi.
 
Wapo waliopata wachumba na kuoana hapahapa JF, wapo wanaofanya biashara na kufanikiwa kupitia hapahapa JF, wapo wanaopata mawazo ya biashara na kijasiriamali.
Kuhusu elimu ndio usiseme, JF ni shule tosha. Marafiki pia wanapatikana kwa sana tu hapa mtandaoni, je wewe binafsi JF imekufanyia nini ambacho unaona ni kikubwa?

nimepata faida ya kupigwa ban mara 2 ndani ya week kadhaa
 
Nimepata mke wa pili hapa hapa JF.......Siku ikifika nitamtaja rasmi na kumtabulisha kwa wadau wa JF !!
 
kipindi kile inaitwa jambo forum.. kilichonileta ilikuwa ni mziki.. kulikuwa na nyimbo "zilipendwa" .. kuhusu faida ! mhh! idadi ya thanks nilizotoa zinajieleza.. but kuna watu napenda sana thread zao "hawamo kwenye jukwaa la siasa" sitowataja wasije wakafanya ya "mgema akisifiwa tembo hulitia maji"

long live JF
 
I spend many time in my research laboratory, but when I turn my computer the first thing is JF and when I wanna switch off my computer, the last program is JF. I am proud to be JF member!

Nimeshasahau kama kuna magazeti! Najisikia kama niko karibu na bongo, kwani mambo mengi nayapata wakati mwingine nakuwa source of information to people who are in Tanzania.
 
Chemchem na Bubujiko la mawazo mbadala, mgando hata ya kipuuzi ya wenzetu wenye magamba. Najua kuna gharama kubwa kuendesha JF lakini haikosekani kutoa latest news na michango kede kede kwa kujitolea. Nadhani hapa ndipo Tanzania ilipo.
 
Nimejifunza mengi kuhusu sisi tunavyofikiri.
JF ina fikra pana katika kila jambo
Uhuru wa kujieleza na kuwasiliana unatumika vilivyo
Wamo waalimu na wanafunzi humu ndani, lakini pia wamo watezamaji wengi tu:smiling:
 
nilichojifunza
1.kutoogopa kufa zamani nlikuwa mwoga wa kifo,lakini toka nijue jf siogopi
2.nimejifunza computer humu jf
3.uwezo wangu wa kufikiri na kuchambua mambo umeongezeka sana
4.nimemtafutia kazi moja wa member wa jf ni competent sana
5.nilikuwa sijui hii nchi ilivyotafunwa
 
Aseee!
Jf imenikutanisha na wazee wa TISS! Komfuu zake balaa!
Bongo hakuna sheria.
 
sijui niseme nafaidika au ni vipi, kwani nimekuwa addicted, nikiamuka ni jf, nikiwa kazini kazi zikipungua ni jf, nikirudi home ni jf mpaka naenda lala, mimi nafikiri jf imekuwa kama mke kwa upande wangu.
 
mimi si wa siku nyingi hapa jf lakini aliyeniambia habari za jf kwa mara ya kwanza sitamsahau kwani hakika jf ni kisima cha mawazo ,maarifa etc.hapa kuna watu wanajua kudadavua mambo si mchezo,ni chuo cha mafunzo kwa anaetaka kujifunza.wale tulioko jf tuwashawishi na wengine waje waelimike tuikomboe nchi yetu.
 
Jf imenifundisha mengi sanaa. Kwa mda mfupi nilioanza kuingia humu jukwaani nimekuwa na ujasiri wa kuhoji kila nachoambiwa, yaani upeo wangu wa kufikiri kabla ya kutenda umeongezeka sanaa.

Pia kubwa kuliko yote ninapata hot news kila sikuu...viva forever jf.
 
Swali zuri sana buji buji .. Binafsi sijajifunza lolote zaidi ya kugundua -

1) kuna wa tzn ni wavivu wa kufikiri.. wengi mno humu JF mfano mchungaji REV au MZEE Mwanakijiji . akianzisha thread na kuandika HAHAHAHA "watamwaga thanks nyingi sana" wapo hao watu humu JF

2) kuna watu wanajifanya wajuaji wa mambo na wakibanwa wanatelekeza thread na kuingia na new user name

3) kuna watu ni wapumbavu kiasi kwamba wanaweka kinyongo na avatar yenye jina flani, lakini ni swahiba wa avatar ya jina flani wanashindwa kufikiri kwamba inawezekana zile avatar mbili ni ndugu! its a mater of reading btwn lines

4)Nimegundua wa tzn wengi wana mawazo ya kizinzi

5) Nime gundua wa tnz wengi they are afraid kutoa mawazo yao wenyewe kama yalivyo akiogopa wana JF watakuo kuja na kumuandikia "crap"

6) Nimegunduwa kwamba as long mbongo akiwa na NET + TIME basi anadhani ni lazima a replay kila thread katika jukwaa la siasa la JF mfano mzuri ID ya kings of kings .. topic ikiwa out of his thinking capacity atakopi thread nzima na kutoa conclusion na kuandika crap. au kuweka picha.

7) Nimegunduwa wana JF wanapenda sifa za kijinga "kujianzishia thread" na kujipa hongera!

8) Nimegundua kwamba wana JF wengi they are afraid of being different

9) Nimegundua members wengi wa JF wanadhani ukiwa mwana JF lazima uwe mfuasi wa chadema na kwamba watu wote walio JF basi ni chadema

10) Sijajifunza lolote humu JF but nashukuru napata updates kinachoendelea ndani ya TZN



 
Swali zuri sana buji buji .. Binafsi sijajifunza lolote zaidi ya kugundua -

1) kuna wa tzn ni wavivu wa kufikiri.. wengi mno humu JF mfano mchungaji REV au MZEE Mwanakijiji . akianzisha thread na kuandika HAHAHAHA "watamwaga thanks nyingi sana" wapo hao watu humu JF

2) kuna watu wanajifanya wajuaji wa mambo na wakibanwa wanatelekeza thread na kuingia na new user name

3) kuna watu ni wapumbavu kiasi kwamba wanaweka kinyongo na avatar yenye jina flani, lakini ni swahiba wa avatar ya jina flani wanashindwa kufikiri kwamba inawezekana zile avatar mbili ni ndugu! its a mater of reading btwn lines

4)Nimegundua wa tzn wengi wana mawazo ya kizinzi

5) Nime gundua wa tnz wengi they are afraid kutoa mawazo yao wenyewe kama yalivyo akiogopa wana JF watakuo kuja na kumuandikia "crap"

6) Nimegunduwa kwamba as long mbongo akiwa na NET + TIME basi anadhani ni lazima a replay kila thread katika jukwaa la siasa la JF mfano mzuri ID ya kings of kings .. topic ikiwa out of his thinking capacity atakopi thread nzima na kutoa conclusion na kuandika crap. au kuweka picha.

7) Nimegunduwa wana JF wanapenda sifa za kijinga "kujianzishia thread" na kujipa hongera!

8) Nimegundua kwamba wana JF wengi they are afraid of being different

9) Nimegundua members wengi wa JF wanadhani ukiwa mwana JF lazima uwe mfuasi wa chadema na kwamba watu wote walio JF basi ni chadema

10) Sijajifunza lolote humu JF but nashukuru napata updates kinachoendelea ndani ya TZN




Nimegundua huwezi kuelewa kuwa kupata updates JF ni kufaidika. Kweli JF inatukutanisha na kila aina ya watu
 
Wapo waliopata wachumba na kuoana hapahapa JF, wapo wanaofanya biashara na kufanikiwa kupitia hapahapa JF, wapo wanaopata mawazo ya biashara na kijasiriamali.
Kuhusu elimu ndio usiseme, JF ni shule tosha. Marafiki pia wanapatikana kwa sana tu hapa mtandaoni, je wewe binafsi JF imekufanyia nini ambacho unaona ni kikubwa?

Bujibuji huwa nafurahia sana mada zako.Huwa ni za kuleta utata ila zina maana kubwa sana.MIMI nimejifunza mengi hasa katika upande wa teknolojia.Pia katika ushauri wa kimasomo na maisha ndo usiseme.Pia nimefanikiwa kupata uwezn wa kuelewa mambo kwa upana na sio kwa ufinyu.Hata nikitaka kunnua BAISKELI nikija hapa ntapata ushauri.Nipo njian naelekea dar kununua computer kwenye duka la mwana JF mwenzangu.Tena kwa bei ambayo hakuna wizi ndani yake.JE kwa nini member wa JF karibia wote wana Busara sana?tofaut na kule FB?toka nijiunge sina maswali tata yanayonisumbua kwani kila linalonitatiza huwa naliweka hapa jf.Nina mengi ya kuongea ila naishia hapa kwani nipo ndani ya basi na mwendo ni mkali sana.Nikifika dar nataman nikuone bujibuji.
 
Back
Top Bottom