Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,340
- 51,900
Anaandika, Robert Heriel,
Mtibeli.
Hakuna kazi rahisi kama kuuondoa Umaskini. Rahisi Sana. Ukisikia mtu anakuambia kupambana na umaskini na ikazidi ngumu basi jua huyo ni muongo au anazungumzia, Siasa.
Matatizo ya asili yanakabiliwa kwa urahisi na kanuni rahisi kuliko matatizo ya kutengenezwa.
Ujinga wa asili ni rahisi kuundoa kwenye jamii kuliko ujinga wa uliotengenezwa.
Taikon katika chunguzi zangu nikabaini ya kuwa matatizo mengi ya ulimwengu huu sio ya asili bali ni matatizo ya bandia ambayo yamebuniwa kwa Faida Fulani ya Watu fulani, na yale matatizo ya asili hakuna ugumu wa kuyaondoa.
Vijana lazima muelewe kuwa ni rahisi sana kupambana na umaskini ulioukuta hapo nyumbani kwenu, lakini ni ngumu sana kukabiliana na Umaskini wa kusababishwa na mtu au Watu wengine, na hapa nazungumzia wale walioitwa au wanaojiita watawala iwe kisheria au kwa namna yoyote ile.
Kanuni ya kupambana na Umaskini wa asili ni mbili tuu.
1. Kufanya kazi kwa juhudi, bidii akili na maarifa.
2. Kutumia rasilimali kwa usahihi bila kuathiri mazingira.
Rasilimali hizo ni muda, Watu, na Mali na maliasili. Kwenye muda kuna wakati uliopita(tumia Data Sahihi zilizopita) wakati uliopo ambao upo, na wakati ujao. Rasilimali Watu. Hapa utapata nguvu kazi na mawazo(akili) za Watu wengine ambazo wewe isingewezekana kuwa nazo. Ardhi, maji, misitu, wanyama ni sehemu ya maliasili.
Yaani kwenu kama ni maskini kwa asili. Basi ukitaka utoboe ni kanuni mbili hizo.
Wakati unahangaika kupambana na Umaskini wa asili unakuja kugundua kuwa kumbe kuna umaskini mwingine wa kutengeneza. Umaskini Bandia. Hapo ndio unashangaa Watu wanapambana lakini hatoboi.
Ni uongo kusema Kufanikiwa (kuushinda Umaskini) ni majaliwa ya Mungu. Mtu yeyote anayeweza hivyo jua tayari keshatengenezwa kifikra na walewale wasiotaka ajue ukweli.
Kufanikiwa (kuushinda Umaskini wa Asili) sio majaliwa kutoka kwa mwenyezi Mungu bali ni uamuzi wa mtu au jamii yenyewe. Mziki upo kwenye Umaskini Bandia.
Umaskini Bandia unaletwa kwa mwavuli wa kuuondoa Umaskini wa asili.
Mataifa makubwa hutengeneza mazingira ya kuufuta Umaskini wa asili ili kupumbaza Watu lakini nyuma yake kwa jicho jingine wanakuletea umaskini Bandia ambao ni mgumu sana kuuondoa
Serikali batili au zenye dhulma huzuga kwa kuonyesha zinahangaika kupambana na umaskini wa asili wa wananchi lakini ukiangalia kwa jicho jingine mambo huwa tofauti kabisa.
Umaskini Bandia sifa yake kuu ni ile dhana ya watawala kukuambia bila wao nchi haiwezi kuendelea. Au ile dhana ya kusema wataleta barabara au maendeleo. Hao ndio wanaotengeneza umaskini Bandia hata kama watajenga vitu wasemavyo lakini utastaajabu bado jamii ipo kwenye lindi la umaskini mkubwa.
Umaskini Bandia upo hata kwenye Dini. Ile kusema bila kwenda kwenye nyumba za ibada kuombewa hutofanikiwa(hutoushinda umaskini) ndio umaskini wenyewe huo.
Huna haja ya kumuomba Mungu ili uondokane na Umaskini wa asili kwa sababu naturally kila kiumbe kimezaliwa na uwezo wa kuuondoa Umaskini wake na jamii yake pasipo msaada kutoka nje, lakini Umaskini bandia yaani wakutengenezewa huo unahitaji nguvu ya ziada kukabiliana nao.
Je, mpaka sasa huo unapambana nao ni umaskini wa asili au Bandia(wakubambikiwa)?
Taikon acha nipumzike sasa.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.
Mtibeli.
Hakuna kazi rahisi kama kuuondoa Umaskini. Rahisi Sana. Ukisikia mtu anakuambia kupambana na umaskini na ikazidi ngumu basi jua huyo ni muongo au anazungumzia, Siasa.
Matatizo ya asili yanakabiliwa kwa urahisi na kanuni rahisi kuliko matatizo ya kutengenezwa.
Ujinga wa asili ni rahisi kuundoa kwenye jamii kuliko ujinga wa uliotengenezwa.
Taikon katika chunguzi zangu nikabaini ya kuwa matatizo mengi ya ulimwengu huu sio ya asili bali ni matatizo ya bandia ambayo yamebuniwa kwa Faida Fulani ya Watu fulani, na yale matatizo ya asili hakuna ugumu wa kuyaondoa.
Vijana lazima muelewe kuwa ni rahisi sana kupambana na umaskini ulioukuta hapo nyumbani kwenu, lakini ni ngumu sana kukabiliana na Umaskini wa kusababishwa na mtu au Watu wengine, na hapa nazungumzia wale walioitwa au wanaojiita watawala iwe kisheria au kwa namna yoyote ile.
Kanuni ya kupambana na Umaskini wa asili ni mbili tuu.
1. Kufanya kazi kwa juhudi, bidii akili na maarifa.
2. Kutumia rasilimali kwa usahihi bila kuathiri mazingira.
Rasilimali hizo ni muda, Watu, na Mali na maliasili. Kwenye muda kuna wakati uliopita(tumia Data Sahihi zilizopita) wakati uliopo ambao upo, na wakati ujao. Rasilimali Watu. Hapa utapata nguvu kazi na mawazo(akili) za Watu wengine ambazo wewe isingewezekana kuwa nazo. Ardhi, maji, misitu, wanyama ni sehemu ya maliasili.
Yaani kwenu kama ni maskini kwa asili. Basi ukitaka utoboe ni kanuni mbili hizo.
Wakati unahangaika kupambana na Umaskini wa asili unakuja kugundua kuwa kumbe kuna umaskini mwingine wa kutengeneza. Umaskini Bandia. Hapo ndio unashangaa Watu wanapambana lakini hatoboi.
Ni uongo kusema Kufanikiwa (kuushinda Umaskini) ni majaliwa ya Mungu. Mtu yeyote anayeweza hivyo jua tayari keshatengenezwa kifikra na walewale wasiotaka ajue ukweli.
Kufanikiwa (kuushinda Umaskini wa Asili) sio majaliwa kutoka kwa mwenyezi Mungu bali ni uamuzi wa mtu au jamii yenyewe. Mziki upo kwenye Umaskini Bandia.
Umaskini Bandia unaletwa kwa mwavuli wa kuuondoa Umaskini wa asili.
Mataifa makubwa hutengeneza mazingira ya kuufuta Umaskini wa asili ili kupumbaza Watu lakini nyuma yake kwa jicho jingine wanakuletea umaskini Bandia ambao ni mgumu sana kuuondoa
Serikali batili au zenye dhulma huzuga kwa kuonyesha zinahangaika kupambana na umaskini wa asili wa wananchi lakini ukiangalia kwa jicho jingine mambo huwa tofauti kabisa.
Umaskini Bandia sifa yake kuu ni ile dhana ya watawala kukuambia bila wao nchi haiwezi kuendelea. Au ile dhana ya kusema wataleta barabara au maendeleo. Hao ndio wanaotengeneza umaskini Bandia hata kama watajenga vitu wasemavyo lakini utastaajabu bado jamii ipo kwenye lindi la umaskini mkubwa.
Umaskini Bandia upo hata kwenye Dini. Ile kusema bila kwenda kwenye nyumba za ibada kuombewa hutofanikiwa(hutoushinda umaskini) ndio umaskini wenyewe huo.
Huna haja ya kumuomba Mungu ili uondokane na Umaskini wa asili kwa sababu naturally kila kiumbe kimezaliwa na uwezo wa kuuondoa Umaskini wake na jamii yake pasipo msaada kutoka nje, lakini Umaskini bandia yaani wakutengenezewa huo unahitaji nguvu ya ziada kukabiliana nao.
Je, mpaka sasa huo unapambana nao ni umaskini wa asili au Bandia(wakubambikiwa)?
Taikon acha nipumzike sasa.
Robert Heriel,
Taikon wa Fasihi,
Kwa sasa Dar es Salaam.