Ulafi wa Mkuu wa Chuo cha ufundi Arusha na hatima ya elimu inayotolewa na chuo

TUNDE

Senior Member
Apr 23, 2016
129
77
Si jambo la siri au kificho kwamba kuna ufisadi mkubwa, tena wa kutisha uliofanywa na unaoendelea kufanywa na Mkuu wa chuo cha Ufundi Arusha. Mtu anaweza kushangaa au kuuliza kwanini Mkuu wa Chuo na siyo Menejimenti ya Chuo? Ukweli ni kwamba ni kama vile Chuo hakina Menejimenti kwa sababu Mkuu wa Chuo ndio kila kitu katika Chuo hiki. Mkuu wa chuo ndiye anayeamua masuala ya ununuzi, ukaguzi, uhasibu, sheria, rasilimali watu, na hata idara zifanye nini. Kwa namna anavyofanya kazi ametaka aonekane kama mtendaji wa kila kitu na kwa maana hiyo wasaidizi wake hawana cha kufanya ila kuwa watazamaji tu.

Ni katika hali hiyo Mkuu wa chuo ameona inafaa kutumia nafasi hiyo kujichukulia fedha za serikali na umma kama anavyotaka. Mkuu wa Chuo alianza kwa kujizidishia mshahara kwa kulipwa katika ngazi kubwa kuliko cheo chake. Akawa anakula fedha zinazotengwa kwa ajili ya mafunzo viwandani. Fedha hizi amekuwa akizila kwa kuongeza idadi ya wanafuzi wa kulipwa na kupunguza idadi ya siku kwa waalimu kwenda kukagua wanafuzi wakiwa viwandani. Aliponogewa zaidi aliamua kutoa malipo hewa kutoka katika miradi mbalimbali ya ujenzi na kuyapitishia katika akaunti ya chuo ijulikanayo kama ATC-PCB ambapo huwa amekuwa akiamua kula pesa kutoka katika akaunti hiyo kama anavyotaka. Kama haitoshi Mkuu wa chuo amekuwa akila fedha inayotengwa kwa ajili ya chakula cha wanafunzi kwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata huduma hiyo.

Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni. Mkuu wa chuo alienda mbali zaidi na kuamua kula mshahara wa mwezi mmoja kwa wafanyakazi 25 wa Chuo bila maelezo. Mkuu wa chuo alikula sehemu kubwa ya fedha zilizotolewa na DIDF kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika shamba la Oljoro Arusha. Ubunifu wa Ulafi wa Mkuu wa Chuo uliongezeka na aligundua njia ya kujipatia mapato kutoka mishahara ya wafanyakazi wanaoishi katika nyumba za chuo. Mkuu wa chuo anaishi nyumba ya chuo na halipi chochote lakini aliamua bila ridhaa ya wafanyakazi kukata pesa kutoka mishahara ya wafanyakazi huku ikiwa haifahamiki fedha hizo ziko wapi au zinafanya nini.

Ulafi wa Mkuu wa chuo amepanuka mpaka kufikia kiwango cha kuwa akiongeza gharama za miradi ya ujenzi inayofanywa chuoni. Kwa mfano, Ujenzi wa jengo la madarasa linalojulikana kama Jengo la Umwagiliaji limeongezwa mpaka kukaribia mara dufu. Jengo hilo lilikadiriwa kujengwa kwa Tsh 2.67 bilioni zilizokuwa katika mkataba wa ujenzi lakini mpaka mwisho jengo hilo limetafuna kiasi cha Tsh 4.0 bilioni huku muonekano wake kwa ndani ukionekana kufanywa kwa kiwango cha chini kabisa. Pia katika ujenzi huo idadi kubwa sana ya matofali inaweza kuandikwa kuwa yaliibiwa. Idadi ya matofali yaliyochukuliwa kwa mwavuli wa ukubwa wa Mkuu wa Chuo ni 20,000, idadi ya matofali ambayo yangetosha kujenga madarasa 18 mengine.

Fedha nyingi ambayo ingeweza kufanya maendeleo mengine kwa aajili ya chuo na Taifa inaonekana kuliwa kwa njia ya kifisadi kwa sababu tu ya ulafi wa mtu mmoja asiyekuwa na chembe ya Uzalendo kwa nchi yake.

Madhara ya ulafi na kukosa uzalendo kunaonekana kwenda mpaka kuathiri kiwango cha elimu inayotolewa. Kwa mfano, Mkuu wa chuo ameshindwa kabisa huhuisha mitaala iliyopitwa na wakati inayotumika kufundishia wanafunzi. Kibaya zaidi ni kwamba kwa maelekezo ya Mkuu wa Chuo baadhi ya Idara za kitaaluma zimekuwa zikitumia mitaala isiyofahamika ambayo haijapitishwa na Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) wala Tume ya Vyuo Vikuu (TCU).

Katika kutaka kubana matumizi ili pia kupata pesa ya kuweza kuiba kwa njia ya ufisadi na ulafi, Mkuu wa Chuo anatumia wafanyakazi waendeshaji wasio na sifa kufundisha wanafunzi wa ngazi ya shahada. (Bachelor of Engineering). Ni mambo ya ajabu sana yanayofanyika kweli mtu mwenye akili zake timamu akiyaona anaweza kushangaa sana na kujiuliza kama Mkuu wa Chuo anayo elimu ya kiwango kinachozungumzwa maana yanayofanyika yanasikitisha. Msomi wa kiwango cha PhD ni mtafiti na huamini katika utafiti lakini hapa ni tofauti.

Hivi karibuni kulikuwa na habari za ugunduzi wa chopa (Helicopter) uliofanywa na chuo lakini hakukuwa na utafiti wowote uliokuwa umefanywa ili kutokana na utafiti huo chopa hiyo iweze kutengenezwa. Hakukuwa na andiko lolote la kitaalamu ambalo lingekuwa mwongozo wa utengenezaji wa chopa hiyo. Hata hivyo utengenezaji wa toy hiyo ya chopa ulipigwa marufuku na serikali na hivyo kuwa imetumia muda na rasilimali za serikali bila tija yoyote.

Katika mazingira yanayofanana na hayo pia kulikuwa na mbwembwe na viapizo vingi sana kuwa Chuo cha Ufundi Arusha Chaapa kumaliza tatizo la umeme nchini. Lakini sababu kubwa ya viapizo hivyo ilikuwa ni utafiti uliokuwa umefanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhusu kutengeneza mashine (turbine) ya kuweza kufua umeme kwa njia ya maji ambayo haikuwa imefika mwisho. Hakukuwa na utafiti wowote uliofanywa na chuo wala hakukuwa na andiko lolote lililokuwa limeandikwa na chuo huhusu utengenezaji wa turbine za kufua umeme ambao Mkuu wa chuo alionekana kwa wakati huo kila chombo cha habari akijaribu kuchota akili za watanzania kwa mambo yasiyo ya kweli.

Ni wakati sasa Uchunguzi wa kina wa umahiri wa kitaaluma wa chuo hiki uweze kufanyika ili kuepusha hasara kubwa zaidi inayoweza kusababishwa kwa kuendelea kuamini kisichokuwepo. Elimu ni msingi wa maendeleo ya Taifa lolote, Ni hujuma mbaya sana ikiwa tutakubali elimu ya Taifa letu ikahujumiwa na walafi wa aina ya Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha.
 
Duh, Jamaa anapiga ile mbaya. Kaweza na kujitengenezea kabodi kake ka Wakurugenzi. Kila siku wanamfagilia kwa kazi nzuri anayofanya. Siku si nyingi, elimu ya chuo itakuwa imezikwa kaburini.
 
Tunaomboleza kifo cha nguli wa siasa za Tanzania Marehemu Samweli Sitta. Lakini kimoja ambacho tunatakiwa kujifunza ni kuwa alikuwa akiuguzwa katika hispitili ya The TECHNICAL UNIVERSITY OF MUNICH. Vyuo vilivyojaliwa kufanya tafiti na vyenye uwezo mkubwa wa kufanya mambo. Hapa kwetu kama inavyoonekana kwa mada iliyotolewa kazi kubwa inayofanywa ni wizi, matumizi mabaya ya ofisi, na kudanganya umma. Hakuna kingine, nadhani baada ya ushindi wa Triump na Tunaye Rais Magufuli ambao wote hawataki mambo ya hovyo-hovyo kama haya yanayofanyika katika chuo hicho, tutegemee kuona mabadiliko.
 
Uzoefu unaonesha kwamba wengi wa wanaothubutu kufanya mambo ya ajabu kiasi hicho wanaamini katika nguvu za Sangoma. Hapo alipo atakuwa amejichimbia mambo ambayo hakuna anayeweza kuona kinachosemwa. Uzuri au ubaya wa sangoma ni kwamba nguvu zake huwa zinakwisha nguvu baada ya muda. Ikiwa atashindwa kwenda kuzirudishia ni lazima mambo yote yaonekane. inaaminika safari nyingi za wakubwa watatu wa chuo ni katika harakati za kujilinda kwa wataalamu wa sangoma mambo yao yasionekane kwa wenye mamlaka. Heri yao wanaofanya kazi zao kwa uadilifu.
 
Umeandika meengi ila hujamtaja jina.

Unamwogopa?

Ikiwa ni kweli na una ushahidi katika hayo yote na utakuwa tayari kuyaeleza haya hadharani itakuwa jambo jema sana.

Serikali imchukulie hatua huyu Mkuu wa Chuo.
 
Ni kweli kabisa, Mkuu wa chuo anaonekana kuwa na ulafi. Hivi karibuni alipitisha sera ya kupaki magari akilenga kuendelea kukata mishahara ya wafanyakazi, kulipia paking ya magari yao. Alikata mishahara kulipia nyumba wakati yeye hakatwi, yeye ana maji lakini chuo kizima hakina maji kwa zaidi ya miezi miwili sasa. Na kwa upande mwingine anatafuta kila njia ya kufanya wafanyakazi wa chuo kuwa masikini.

Baada ya habari za ufisadi wa Mkuu wa chuo kuzagaa inaonekana kama kuna pesa iliyokuwa imefichwa imeanza kutolewa ifanye kazi za chuo. Ni muda mrefu nyumba zilikuwa zimechakaa na zilikuwa hazikarabatwi ila kidogo sasa zinakarabatiwa japo kwa kasi isiyoridhisha na gharama zimepelekwa juu kama kawaida. Inaaminika pia kuna kazi zitafanyika katika shamba la oljoro baada ya habari za ufisadi wa Mkuu wa Chuo kusambaa.

Itafaa pesa yote iliyoibwa ikarudishwa ili kupunguza ukubwa wa tatizo. hata kama kuna mashamba na viwanja vilivyokuwa vimenunuliwa kwa pesa hiyo ni bora vikauzwa ili kurudisha pesa hiyo ikafanya maendeleo ya chuo.
 
Hebu mtutajie huyu MTU au Luna MTU anatamani nafasi take maana hizi tuhuma zimeanza muda mrefu humu JF
 
Du ! Habari zilizopo ni kwamba nyumba nyingi za watumishi zinakarabatiwa kwa hela kubwa na ambayo inaweza kujenga nyumba mpya. Ni ukweli usiofichika kwamba toka mishahara ya wafanyakazi ianze kukatwa inakadiriwa tayari kiasi cha Tsh 300,000,000/= kitakuwa kimesha kusanywa. Ajabu ni kwamba ukarabati uliofanyika/ unaofanyika hauendani na kiasi kilichopo. Inasemekana kwa vile kiasi kikubwa cha hela hizi zitakuwa zimeenda mifukoni mwa watu, ndio maana kuna uwezekano wa wahusika kudanganya kuwa nyumba moja inakarabatiwa kwa kiwango cha zaidi ya 15,000,000/= ili ku- justfy matumizi ya hela hizi. Kiuhalisia kwa nyumba moja ukarabati hauwezi kuzidi Tsh 5,000,000/=.

Inaaminika kwamba kadri Mkuu wa Chuo anapozidi kukaa ofisini ndivyo anavyozidi kubuni njia mbalimbali za kuhujumu Chuo, Serikali na Taifa kwa ujumla. Ni ukweli usiopingika kwamba kama chuo kingekuwa shirika au kampuni ingeshakuwa imetangazwa mufilisi. Mtazamo mkubwa wa Mkuu wa chuo ni kuwa ni kwa namna gani anastaafu kutokana na utumishi wa umma. Kwa mtizamo huo, kwake kila kinachopita machoni kwa Mkuu wa Chuo ni halali yake bila kujali italeta athari gani kwa jamii.

Hivi sasa Mkuu wa Chuo amekuwa na kawaida ya kubuni safari za mara kwa mara lakini wafanyakazi hawajawahi kupewa mrejesho wa safari hizo na tija yake.
 
Si jambo la siri au kificho kwamba kuna ufisadi mkubwa, tena wa kutisha uliofanywa na unaoendelea kufanywa na Mkuu wa chuo cha Ufundi Arusha. Mtu anaweza kushangaa au kuuliza kwanini Mkuu wa Chuo na siyo Menejimenti ya Chuo? Ukweli ni kwamba ni kama vile Chuo hakina Menejimenti kwa sababu Mkuu wa Chuo ndio kila kitu katika Chuo hiki. Mkuu wa chuo ndiye anayeamua masuala ya ununuzi, ukaguzi, uhasibu, sheria, rasilimali watu, na hata idara zifanye nini. Kwa namna anavyofanya kazi ametaka aonekane kama mtendaji wa kila kitu na kwa maana hiyo wasaidizi wake hawana cha kufanya ila kuwa watazamaji tu.

Ni katika hali hiyo Mkuu wa chuo ameona inafaa kutumia nafasi hiyo kujichukulia fedha za serikali na umma kama anavyotaka. Mkuu wa Chuo alianza kwa kujizidishia mshahara kwa kulipwa katika ngazi kubwa kuliko cheo chake. Akawa anakula fedha zinazotengwa kwa ajili ya mafunzo viwandani. Fedha hizi amekuwa akizila kwa kuongeza idadi ya wanafuzi wa kulipwa na kupunguza idadi ya siku kwa waalimu kwenda kukagua wanafuzi wakiwa viwandani. Aliponogewa zaidi aliamua kutoa malipo hewa kutoka katika miradi mbalimbali ya ujenzi na kuyapitishia katika akaunti ya chuo ijulikanayo kama ATC-PCB ambapo huwa amekuwa akiamua kula pesa kutoka katika akaunti hiyo kama anavyotaka. Kama haitoshi Mkuu wa chuo amekuwa akila fedha inayotengwa kwa ajili ya chakula cha wanafunzi kwa kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata huduma hiyo.

Ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni. Mkuu wa chuo alienda mbali zaidi na kuamua kula mshahara wa mwezi mmoja kwa wafanyakazi 25 wa Chuo bila maelezo. Mkuu wa chuo alikula sehemu kubwa ya fedha zilizotolewa na DIDF kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika shamba la Oljoro Arusha. Ubunifu wa Ulafi wa Mkuu wa Chuo uliongezeka na aligundua njia ya kujipatia mapato kutoka mishahara ya wafanyakazi wanaoishi katika nyumba za chuo. Mkuu wa chuo anaishi nyumba ya chuo na halipi chochote lakini aliamua bila ridhaa ya wafanyakazi kukata pesa kutoka mishahara ya wafanyakazi huku ikiwa haifahamiki fedha hizo ziko wapi au zinafanya nini.

Ulafi wa Mkuu wa chuo amepanuka mpaka kufikia kiwango cha kuwa akiongeza gharama za miradi ya ujenzi inayofanywa chuoni. Kwa mfano, Ujenzi wa jengo la madarasa linalojulikana kama Jengo la Umwagiliaji limeongezwa mpaka kukaribia mara dufu. Jengo hilo lilikadiriwa kujengwa kwa Tsh 2.67 bilioni zilizokuwa katika mkataba wa ujenzi lakini mpaka mwisho jengo hilo limetafuna kiasi cha Tsh 4.0 bilioni huku muonekano wake kwa ndani ukionekana kufanywa kwa kiwango cha chini kabisa. Pia katika ujenzi huo idadi kubwa sana ya matofali inaweza kuandikwa kuwa yaliibiwa. Idadi ya matofali yaliyochukuliwa kwa mwavuli wa ukubwa wa Mkuu wa Chuo ni 20,000, idadi ya matofali ambayo yangetosha kujenga madarasa 18 mengine.

Fedha nyingi ambayo ingeweza kufanya maendeleo mengine kwa aajili ya chuo na Taifa inaonekana kuliwa kwa njia ya kifisadi kwa sababu tu ya ulafi wa mtu mmoja asiyekuwa na chembe ya Uzalendo kwa nchi yake.

Madhara ya ulafi na kukosa uzalendo kunaonekana kwenda mpaka kuathiri kiwango cha elimu inayotolewa. Kwa mfano, Mkuu wa chuo ameshindwa kabisa huhuisha mitaala iliyopitwa na wakati inayotumika kufundishia wanafunzi. Kibaya zaidi ni kwamba kwa maelekezo ya Mkuu wa Chuo baadhi ya Idara za kitaaluma zimekuwa zikitumia mitaala isiyofahamika ambayo haijapitishwa na Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) wala Tume ya Vyuo Vikuu (TCU).

Katika kutaka kubana matumizi ili pia kupata pesa ya kuweza kuiba kwa njia ya ufisadi na ulafi, Mkuu wa Chuo anatumia wafanyakazi waendeshaji wasio na sifa kufundisha wanafunzi wa ngazi ya shahada. (Bachelor of Engineering). Ni mambo ya ajabu sana yanayofanyika kweli mtu mwenye akili zake timamu akiyaona anaweza kushangaa sana na kujiuliza kama Mkuu wa Chuo anayo elimu ya kiwango kinachozungumzwa maana yanayofanyika yanasikitisha. Msomi wa kiwango cha PhD ni mtafiti na huamini katika utafiti lakini hapa ni tofauti.

Hivi karibuni kulikuwa na habari za ugunduzi wa chopa (Helicopter) uliofanywa na chuo lakini hakukuwa na utafiti wowote uliokuwa umefanywa ili kutokana na utafiti huo chopa hiyo iweze kutengenezwa. Hakukuwa na andiko lolote la kitaalamu ambalo lingekuwa mwongozo wa utengenezaji wa chopa hiyo. Hata hivyo utengenezaji wa toy hiyo ya chopa ulipigwa marufuku na serikali na hivyo kuwa imetumia muda na rasilimali za serikali bila tija yoyote.

Katika mazingira yanayofanana na hayo pia kulikuwa na mbwembwe na viapizo vingi sana kuwa Chuo cha Ufundi Arusha Chaapa kumaliza tatizo la umeme nchini. Lakini sababu kubwa ya viapizo hivyo ilikuwa ni utafiti uliokuwa umefanywa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kuhusu kutengeneza mashine (turbine) ya kuweza kufua umeme kwa njia ya maji ambayo haikuwa imefika mwisho. Hakukuwa na utafiti wowote uliofanywa na chuo wala hakukuwa na andiko lolote lililokuwa limeandikwa na chuo huhusu utengenezaji wa turbine za kufua umeme ambao Mkuu wa chuo alionekana kwa wakati huo kila chombo cha habari akijaribu kuchota akili za watanzania kwa mambo yasiyo ya kweli.

Ni wakati sasa Uchunguzi wa kina wa umahiri wa kitaaluma wa chuo hiki uweze kufanyika ili kuepusha hasara kubwa zaidi inayoweza kusababishwa kwa kuendelea kuamini kisichokuwepo. Elimu ni msingi wa maendeleo ya Taifa lolote, Ni hujuma mbaya sana ikiwa tutakubali elimu ya Taifa letu ikahujumiwa na walafi wa aina ya Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha.
7640_10153996847952487_1296214619587581403_n.jpg
 
Hili Tangazo limepitwa na wakati, na halielezi uhalisia wa mambo yanayolalamikiwa chuoni. Ni jambo la ukweli kwamba Uongozi wa Chuo umekuwa ukinyanyasa na kuonea wafanyakazi, na hata kufukuza wafanyakazi bila makosa/hatia . Mbona CMA imeshatoa uamuzi kwa baadhi ya wafanyakazi wanaodaiwa kufukuzwa kazi kwa kutofuata sheria, kanuni na taratibu kwamba walionewa na hivyo warudishwe kazini? Hii ni hasara nyingine kwa Chuo tayari, ni nani atalipa gharama za hasara hiyo?
 
Umeandika meengi ila hujamtaja jina.

Unamwogopa?

Ikiwa ni kweli na una ushahidi katika hayo yote na utakuwa tayari kuyaeleza haya hadharani itakuwa jambo jema sana.

Serikali imchukulie hatua huyu Mkuu wa Chuo.
Mkuu wa Chuo hiki anatambulika kama Richard Joseph Masika Mushi. (Inafahamika kuwa ni mwenyeji wa Kibosho-Moshi-Kilimanjaro. Ameajiri mtaalamu wa kilimo anayelipwa mshahara na serikali kwa ajili ya kushughulikia mashamba ya Mkuu wa Chuo anayolima maua kwenye Green house alizojenga nyumbani kwao Kibosho.

Kadhalika Utemi ni Afisa habari wa chuo anayejulikana kama Gasto Leseiyo ambaye ni Mjomba wa Mkuu wa Chuo. Hivyo Gasto Leseiyo anapambana kufa na kupona kujaribu kumtetea Mkuu wa Chuo ambaye ni mjomba wake japo kwa kutaka kupotosha na kudanganya kuhusu ukweli wa maovu mengi yanayofanywa na Mkuu wa Chuo ambayo siyo ya kificho na yapo bayana kabisa.
 
Hana tofauti na MGANIRWA Wa NIT

Ndarichako naomba hivi vyuo NIT na Cha ARUSHA vichunguzwe
kweli hata mimi ninasapotii hili swala mana
mkuu wa chuo cha NIT kwanza anakipeleka chuo kama taasisi yake binafsi anaongoza kwa kufata matakwa yakeeeeeeeee
naomba hawa vigogo wachunguzwe
 
Nimegundua mambo mawili.
1.Wachangiaji wengi wa mada hii ni wageni ,wamefungua account Nov 2016
2 .Mleta mada alikuwa mfanyakazi wa hicho chuo na inaonekana "walikuwa wanapiga dili wote" kabla ya kufarakana na hatimaye kufukuzwa kazi.
Halafu mbona mleta mada huna ubunifu kwa kurejea hii kashfa mara kwa mara? Hujisikii kupuuzwa?
 
Back
Top Bottom