Ukinyang'anywa mtoto, unaweza kuchukua maamuzi kama haya?

hebu acha uongo,mi nna marafiki zangu wengi tu wamelelewa na mama zao mbona hawaichukii hiyo hali? Kwani kuna shida gani kama mtu hataki kuolewa na anataka mtoto akizaa! Kila mtu ana maamuzi yake bana ilimrad havunji sheria.

Huyo yamemkuta na ni yeye ndo anasikia vibaya hana lolote kutuchafulia hali ya hewa tu
 
Angalau hapa umeongea pointi ni kweli kuna wanawake wengine hawana ethics za kuwa mama, ila hapo pa bluu mimi nawajua wadada poa kibao na wanawapenda na kuwatunza watoto wao vizuri kuliko hao walioko maofisini. Ila huyo dk angeenda ustawi wa jamii huwa wanachunguza kama huyo mama hafai kukaa na mtoto wanamnyang'anya tena kisheria kabisa. Ila kwenda kumchukua wakati mama yake hayupo hakutumia busara kabisa mi ningemnyofoa hiyo zubri yake kabisa. Mbafu sana yeye
Punguza jazba maty mwenzio atakojolea wapi?ok anahtaji maombez ya week1
 
Mimi ninaye mama na amenizaa kwa heshima kubwa kabisa wakiwa na baba yangu katika ndoa takatifu, nawapenda sana wazazi wangu. Na nimeshuhudia watoto waliozaliwa kwa mtindo unaofanana na ule wa mbuzi aliyekutana na beberu machungani, watoto hao hawaipendi hata kidogo hali hiyo na inawanyanyapaa sana. Ndicho ninacholaani, tabia ya wanawake kujizalisha hovyo tu kama mbuzi machungani, kwa nini msitulie mkaolewa kwanza ndipo mzae? Mnawakosea sana haki hao watoto mnaowazaa hovyo katika hayo mazingira ya utovu wa maadili. Wanawake badilikeni.

Shukuru Mungu wewe uliyejikuta umezaliwa katika hali hiyo ya 'ndoa takatifu'
 
kwanza mbona alichelewa,angemalkizia kutenganisha kichwa na kiwiliwili chake.

sio suluhisho hilo Tatiana, ondoa hilo pepo la mauaji,
isitoshe utamfanya huyo mtoto aishi na kukua bila kumwona baba yake katika maisha yake yote,
na mbaya zaidi akija kujua kuwa mama ndo alimuua baba,
hata upendo wake kwako hautakuwepo milele!!!!
Issue ni kukaa na kuzungumza pamoja tu!!!!!!
 
Yan huyo dada alikosea kidogo angelenga kile kisu kwenye kifanyio cha huyo dr ili akidondoshe kabisaa! aone kama angetamka mameno ya kashfa kiasi hicho! eti nilikua na shida na mtoto!!!!!!! Pambafu kabisa huyo dr

Ahahaha!yani.and kuna mtu kasema wamama wawe na busara,yani huyo mwanaume alivokua anamtumia kama chombo cha reproduction busara zake zilikua wap?.
 
Nilimpeleka mtoto hosp for a check up maana alikuwa na ka-homa kidogo! Wakati nasubiri kuingia kwa daktari nikasikia kelele za kilio toka chumba kingine, mama/dada mmoja akawa analia "nataka mtoto wangu, nipe mtoto wangu"
Kwa makadirio ya haraka mimi na wateja wengine wa pale hospitalini tukahisi kwamba yule dada/mama alikuja na mtoto mgonjwa na either amefariki au kuna kitu kibaya kimetokea!
Mara tukasikia tena kelele za kuomba msaada "ananiua, ananinyonga", ikabidi tukimbilie kwenda kuona nini kinatokea! Tukakuta Doctor mwanaume ambaye Tshirt yake imelowa damu anamkaba yule mama sakafuni, wakaachanishwa!
Sasa baada ya ile sakata kutulia, yule Dr akaingia kufanyiwa dressing ya wounds za kisu nyuma ya kichwa na shingoni!
Ikabidi tutafute sababu ya yule mama kumjeruhi yule Dr ambaye tulidhani ni mume wake, kumbe ni tofauti kidogo! Yule mama aliongea kwa uchungu sana, akatueleza kwamba yeye na yule Dr walikuwa ni wapenzi,
Huyo Dr ana mke na watoto sita wa kike, sasa amezaa na yule nyumba ndogo mtoto wa kiume! Yule jamaa akakata mahusiano na yule dada, mtoto alipofikisha mwaka 1 na miezi mitatu yule Dr akaja akamchukua mtoto on mother's absence
Akaenda kumficha anakojua! Sasa ndo yule mama akaja kudai mtoto pale kazini kwa hawara yake/baba mtoto! Dr akam-provoke kuwa yeye hakuwa na shida na yule dada, alikuwa na shida na mtoto wa kiume, so achape lapa! Dada wa watu ndo akawa mbogo, Dr akaanza kumdunda, dada akatoa bisu lake akampa za shingoni na utosini!
Je wapendwa wazazi wenzangu, ingekuwa wewe ungeweza kuchukua uamuzi kama huo?

Tunashauriwa na dini zote kueshimu ndoa hii inatokana na tabia mbaya ya uzinifu.
 
sio suluhisho hilo Tatiana, ondoa hilo pepo la mauaji,
isitoshe utamfanya huyo mtoto aishi na kukua bila kumwona baba yake katika maisha yake yote,
na mbaya zaidi akija kujua kuwa mama ndo alimuua baba,
hata upendo wake kwako hautakuwepo milele!!!!
Issue ni kukaa na kuzungumza pamoja tu!!!!!![/QUOTE]

Wakati akimchukua mbona hakukaa tuzungumze pamoja?? Mie ndo nimuanze?? Wewe tulia
 
Anakemewa yupi hapa? dr au mama mtoto?

huyu mama alietaka kuua,
alipaswa kukemewa kabisa!!!!
unajua labda kwakuwa haijatolewa sababu ya msingi ya kwanini dr. aliamua kumchukua mtoto,
yawezekana, malezi ya huyu mtoto kwa yule mama yalikuwa na kasoro fulani,
Achilia mbali kuwa huyo ndo alikuwa mtoto wa kiume pekee kwa dr.
 
Ahahaha!yani.and kuna mtu kasema wamama wawe na busara,yani huyo mwanaume alivokua anamtumia kama chombo cha reproduction busara zake zilikua wap?.

Eti???? Huyo mama mpaka kufikia uamuzi huo ameshaumia sana.
Na huyo mwanaume alikuwa hajatulia kwenye ndoa yake
ndo maana kafanya uzinifu na kupata mtoto hapo busara ya mwanaume iko wapi???
 
sio suluhisho hilo Tatiana, ondoa hilo pepo la mauaji,
isitoshe utamfanya huyo mtoto aishi na kukua bila kumwona baba yake katika maisha yake yote,
na mbaya zaidi akija kujua kuwa mama ndo alimuua baba,
hata upendo wake kwako hautakuwepo milele!!!!
Issue ni kukaa na kuzungumza pamoja tu!!!!!![/QUOTE]

Wakati akimchukua mbona hakukaa tuzungumze pamoja?? Mie ndo nimuanze?? Wewe tulia

sasa ukishamchoma kisu na kumtoa roho,
suluhisho ndo lipi hapo Desidii!!!!
kwasababu mwisho wa siku huyo mwanamke anahitaji faraja ili aendelee na maisha yake
Isitoshe kumbuka hasira, hasara!!!!!!!!!
 
huyu mama alietaka kuua,
alipaswa kukemewa kabisa!!!!
unajua labda kwakuwa haijatolewa sababu ya msingi ya kwanini dr. aliamua kumchukua mtoto,
yawezekana, malezi ya huyu mtoto kwa yule mama yalikuwa na kasoro fulani,
Achilia mbali kuwa huyo ndo alikuwa mtoto wa kiume pekee kwa dr.

Unataka sababu gani ya msingi???
Kashasema dr. anataka mtoto wa kiume ana watano wakike
 
Nilitaka achukue Uamuzi Mkubwa zaidi lakini huo wa KUUA ni mbaya
coz isingemsadia chochote zaidi ya KIFUNGO!!!
Pls 2sichukue uamuzi mbaya na 2jitahidi kucontrol hasira zetu!!!
 
Eti???? Huyo mama mpaka kufikia uamuzi huo ameshaumia sana.
Na huyo mwanaume alikuwa hajatulia kwenye ndoa yake
ndo maana kafanya uzinifu na kupata mtoto hapo busara ya mwanaume iko wapi???

sidhani kama tunatakiwa tufike huku kwenye uaminifu wa ndoa,
kwani tukisema hivo,
hata huyo mwanamke amefanya vibaya kuzaa na mume wa mtu!
issue hapa ni kwamba, mwanamke anapaswa kukemewa kwa kutaka kuua!
hayo mengiene ya uzinzi n.k, ni ya baadae sana!
 
Back
Top Bottom