Memtata
JF-Expert Member
- Jul 27, 2013
- 552
- 1,801
Kuna jamaa mmoja aliwahi kata kabisa kiganja cha mkono wa kibaka baada ya kuudaka dirishani kibaka huyo alipoingiza kutaka kuiba.Ipo hivi.
Weekend iliyopita hawa vijana wanaojifanya wahuni wa mtaa walinitaiti mahali usiku, wakanipiga sana na kuniibia vitu vyangu ikiwemo simu na wallet yangu iliyokuwa na pesa na vitambulisho pamoja na kadi za bank. Ofcoz nilikuwa nimepiga maji kidogo ila niliwakariri, niliripoti tukio polisi ila hakuna lolote lililofanyika.
Sasa mimi nikaamua kuwawinda hawa vibaka, alfajiri ya leo nikajifanya nimetoka na begi nikizuga kuwa nasafiri, nikapita yale maeneo yao na kibegi changu, mara watatu wakanivaa wakaniambia niko chini ya ulinzi na nitoe vyote nilivyonavyo.
Kwa sababu nilikuwa nimejiandaa kwa vita, nikajifanya nafungua lile begi langu nikatoa mapanga yangu mawili niliyokuwa nayo, nikaanza kuwashambulia wakawa wanakimbia, nami nikala nao sahani moja, nikamkamata mmoja aliyekuwa kaanguka akawa ndio mateka wangu, yule dogo nimempiga sana na nimemkata vidole viwili vya mkono wa kulia ili iwe fundidho kwa wenzake.
Alafu jamaa akabaki na kiganja hadi siku alipoambiwa kuna dogo mmoja amekatika kiganja maeneo fulani ila yeye alisema alipata ajali. Basi jama akafungasha kiganja hadi kwa wazazi wake na kuwapa full story kisha kuwaachia mzoga wao. Dogo alikuwa ndani aliposikia maelezo akakimbia kupitia mlango wa nyuma.