Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,023
- 18,562
Kama unataka kudanganya na kupotosha uma, basi ni afadhali hata utumie akili japo kidogo, si kama alivyojidhihirisha huyu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, kwa kile alichokisema;
Alipoulizwa jana kuhusiana na tukio hilo, Kamanda Barlow alithibitisha na kusema kwamba Ofisa Uhamiaji huyo alifananishwa kwa kila kitu na jambazi aliyekuwa anakusudia kwenda kuvamia na kupora katika ghala moja maeneo ya Nyakato ambalo hata hivyo hakulitaja.
Hivi inaingia akilini kwamba mtu anawekewa mtego kwa kukusudia kupora, mbali kabisa na eneo ambalo anakusudia kulipora, na sio mtego unawekwa kwenye eneo ambalo linakusudiwa kuporwa? Na ukimkamata mtu huyo "anayekusudia kupora" mbali na eneo la kupora, utamfikisha mahakamani kwa kosa gani - tulimakamata njiani akiwa anawaza kupora?
Tunajua Polisi wetu wengi ni wavivu wa kutumia akili na wepesi wa kutumia nguvu, lakini wasidhani kwamba Watanzania wote ni wajinga kiasi hicho.
Ukweli ni kwamba bwana Buchafwe ulilengeshwa kuuwawa na mshukuru Muumba wako kwa kukuepusha na kifo.
Alipoulizwa jana kuhusiana na tukio hilo, Kamanda Barlow alithibitisha na kusema kwamba Ofisa Uhamiaji huyo alifananishwa kwa kila kitu na jambazi aliyekuwa anakusudia kwenda kuvamia na kupora katika ghala moja maeneo ya Nyakato ambalo hata hivyo hakulitaja.
Hivi inaingia akilini kwamba mtu anawekewa mtego kwa kukusudia kupora, mbali kabisa na eneo ambalo anakusudia kulipora, na sio mtego unawekwa kwenye eneo ambalo linakusudiwa kuporwa? Na ukimkamata mtu huyo "anayekusudia kupora" mbali na eneo la kupora, utamfikisha mahakamani kwa kosa gani - tulimakamata njiani akiwa anawaza kupora?
Tunajua Polisi wetu wengi ni wavivu wa kutumia akili na wepesi wa kutumia nguvu, lakini wasidhani kwamba Watanzania wote ni wajinga kiasi hicho.
Ukweli ni kwamba bwana Buchafwe ulilengeshwa kuuwawa na mshukuru Muumba wako kwa kukuepusha na kifo.