Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 848
- 1,212
Siku zote natafakari busara, akili, mazingira na wakati uliolazimisha vyama vikuu vya Upinzani Tanzania kusahau historia mbaya, kuachana na umimi na kuunganisha nguvu na kuwa kitu kimoja - Siitazami UKAWA kama kete muhimu katika Uchaguzi Mkuu uliopita ambapo Lowassa alishinda, bali jinsi ilivyojenga uwanja mzuri katika kutekeleza na kutatua migogoro isiyo ya lazima - Zoezi la Uchaguzi wa Mameya, Wenyeviti wa Halmashauri limekwenda vizuri sana chini ya UKAWA, Mgogoro wa Zanzibar - Msimamo safi kutoka UKAWA. Tunashauri UKAWA ijijenge kimfumo na kitaasisi ili kupanua fursa zaidi ya uwakilishi mbadala kwa wananchi.