UKAWA, anzeni Mapema Kumwomba Mhe. Tundu Lissu Agombee Urais Mwaka 2020

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Wadau, nimewaza sana kuhusu nani anafaa kuipeperusha bendera ya UKAWA mwaka 2020 kwenye nafasi ile nyeti.
Kwa upande wa CCM najua kuwa bado mheshimiwa John Pombe Magufuli ataendelea kugombea kulingana na utaratibu uliozoeleka.

Hata hivyo changamoto kubwa bado inasaria kwenye vyama vinavyounda Ukawa! Ni yupi safari ijayo; anafaa kugombea urais kupitia wa vyama hivi?
Hili ni swali moja kubwa mno, si kwao tu bali na kwa watanzania kwa ujumla.

Swali ambalo kulingana na unyeti wake, linahitaji uwekevu wa hekima, au tuseme utulivu wa mawazo unaoweza kupalilia njia ya kuliendea jawabu, kinyume kabisa na ule utaratibu wa kukimbilia majibu mepesi; ambayo aghalabu huwa hayawezi kukidhi haja ya jamii yenye upevu wa kifikra.

Pengine kabla sijaanza kuitetea hoja yangu; ni vizuri watawala wetu; katika nyakati zote, wakafahamu kwamba watanzania wa leo wanahitaji maisha bora tu, na si hadithi za alfulela-ulela.

Sasa kwenye mada, kwa nini Tundu Antipas Lissu na si mwingine?

1) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja mpaka mtoto mdogo akamwelewa!
Ukizingatia kuwa nchi yetu kwa sasa uelewa wa watu si haba, na unazidi kuongezeka kila mwaka.

2) Tundu Lissu ni Mwanasheria mwenye akili nyingi, na mtazamo mpana mno!
Na kwa kutumia ufahamu wake huo atasaidia sana wakati wa kampeni kuongeza ushawishi pindi atakapogusa nyanja mbalimbali na kuja na majibu muafaka kwa jamii ambayo kimsingi imekuwa kama watazamaji tu ilihali sherehe ni yao!

3) Tundu Lissu Hana kashfa yoyote ndani ya taifa hili.

4) Tundu Lissu ni jasiri wa asili yake, ambae wakati wote huenda mbele tuu, na kamwe harudi nyuma katika lile analolisimamia.

5) Ndiye Mwanasheria ambaye anaweza kutupatia katiba ya wananchi ambayo wanasiasa wengi wameonesha uoga kuitetea!

6) Ni kijana pia, ambapo katika daftari la wapiga kura; wengi wao ni vijana.

7) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kuhoji mambo yaliyopinda hivyo anawezakutoa changamoto kubwa kwa wale walio madarakani sasa.
Sababu ziko nyingi mnaweza kuziongeza

Na mwisho pengine niseme hivi labda nitaeleweka zaidi.

Ukawa, au tuseme upinzani kwa ujumla, kutokumtumia mwanasheria huyu mbobevu katika eneo hili muhimu, hiyo haina tofauti kabisa na ile hadithi ya wale wazungu wa kale waliowakuta wasukuma wa Mwadui Shinyanga; wakicheza bao kwa kutumia vipande vya almasi kama kete!!

Je wewe unasemaje kuhusu hili?
 
Acha kumtaja mapema ... CCM wameshaliona hilo ndiyo maana wanampachika kesi ili apoteze sifa huko mbeleni kama watafanikiwa!!
 
Hata mwaka bado mnaanza kutafuta SUB ebu achene watu wafanye kazi, wagombea liwe swala la mwisho na tengenezeni vizazi vipya wapeni nafasi watu wenu wa excel mkianza kuweka masultan mtaendelea kuokota kwenye nyavu.
 
labda wampigie magoti kumuomba mzee
sababu walishapiga hela sasa ujasiri wa kumkata hawana
 
Wadau, nimewaza sana kuhusu nani anafaa kuipeperusha bendera ya UKAWA mwaka 2020 kwenye nafasi ile nyeti.

Kwa upande wa CCM najua kuwa bado mheshimiwa John Pombe Magufuli ataendelea kugombea kulingana na utaratibu uliozoeleka.

Hata hivyo changamoto kubwa bado inasaria kwenye vyama vinavyounda Ukawa!

Ni yupi safari ijayo; anafaa kugombea urais kupitia wa vyama hivi?

Hili ni swali moja kubwa mno, si kwao tu bali na kwa watanzania kwa ujumla.

Swali ambalo kulingana na unyeti wake, linahitaji uwekevu wa hekima, au tuseme utulivu wa mawazo unaoweza kupalilia njia ya kuliendea jawabu, kinyume kabisa na ule utaratibu wa kukimbilia majibu mepesi; ambayo aghalabu huwa hayawezi kukidhi haja ya jamii yenye upevu wa kifikra.

Pengine kabla sijaanza kuitetea hoja yangu; ni vizuri watawala wetu; katika nyakati zote, wakafahamu kwamba watanzania wa leo wanahitaji maisha bora tu, na si hadithi za alfulela-ulela.

Sasa kwenye mada, kwa nini Tundu Antipas Lissu na si mwingine?

1) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja mpaka mtoto mdogo akamwelewa!
Ukizingatia kuwa nchi yetu kwa sasa uelewa wa watu si haba, na unazidi kuongezeka kila mwaka.

2) Tundu Lissu ni Mwanasheria mwenye akili nyingi, na mtazamo mpana mno!
Na kwa kutumia ufahamu wake huo atasaidia sana wakati wa kampeni kuongeza ushawishi pindi atakapogusa nyanja mbalimbali na kuja na majibu muafaka kwa jamii ambayo kimsingi imekuwa kama watazamaji tu ilihali sherehe ni yao!

3) Tundu Lissu Hana kashfa yoyote ndani ya taifa hili.

4) Tundu Lissu ni jasiri wa asili yake, ambae wakati wote huenda mbele tuu, na kamwe harudi nyuma katika lile analolisimamia.

5) Ndiye Mwanasheria ambaye anaweza kutupatia katiba ya wananchi ambayo wanasiasa wengi wameonesha uoga kuitetea!

6) Ni kijana pia, ambapo katika daftari la wapiga kura; wengi wao ni vijana.

7) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kuhoji mambo yaliyopinda hivyo anawezakutoa changamoto kubwa kwa wale walio madarakani sasa.
Sababu ziko nyingi mnaweza kuziongeza

Na mwisho pengine niseme hivi labda nitaeleweka zaidi.

Ukawa, au tuseme upinzani kwa ujumla, kutokumtumia mwanasheria huyu mbobevu katika eneo hili muhimu, hiyo haina tofauti kabisa na ile hadithi ya wale wazungu wa kale waliowakuta wasukuma wa Mwadui Shinyanga; wakicheza bao kwa kutumia vipande vya almasi kama kete!!

Je wewe unasemaje kuhusu hili?
Kweli injini imenokishwa na oili chafu. Poleni sana wadau. Sisi huku CCM ni hili jembe letu Dkt Magufuli usiku na mchana wala hatuwazi. Ila wasi wasi wangu Tundu Lisu hana bil 10.
 
Pia itakuwa ni kumwandaa kwa ajiri ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.
 
Wadau, nimewaza sana kuhusu nani anafaa kuipeperusha bendera ya UKAWA mwaka 2020 kwenye nafasi ile nyeti.
Kwa upande wa CCM najua kuwa bado mheshimiwa John Pombe Magufuli ataendelea kugombea kulingana na utaratibu uliozoeleka.

Hata hivyo changamoto kubwa bado inasaria kwenye vyama vinavyounda Ukawa! Ni yupi safari ijayo; anafaa kugombea urais kupitia wa vyama hivi?
Hili ni swali moja kubwa mno, si kwao tu bali na kwa watanzania kwa ujumla.

Swali ambalo kulingana na unyeti wake, linahitaji uwekevu wa hekima, au tuseme utulivu wa mawazo unaoweza kupalilia njia ya kuliendea jawabu, kinyume kabisa na ule utaratibu wa kukimbilia majibu mepesi; ambayo aghalabu huwa hayawezi kukidhi haja ya jamii yenye upevu wa kifikra.

Pengine kabla sijaanza kuitetea hoja yangu; ni vizuri watawala wetu; katika nyakati zote, wakafahamu kwamba watanzania wa leo wanahitaji maisha bora tu, na si hadithi za alfulela-ulela.

Sasa kwenye mada, kwa nini Tundu Antipas Lissu na si mwingine?

1) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja mpaka mtoto mdogo akamwelewa!
Ukizingatia kuwa nchi yetu kwa sasa uelewa wa watu si haba, na unazidi kuongezeka kila mwaka.

2) Tundu Lissu ni Mwanasheria mwenye akili nyingi, na mtazamo mpana mno!
Na kwa kutumia ufahamu wake huo atasaidia sana wakati wa kampeni kuongeza ushawishi pindi atakapogusa nyanja mbalimbali na kuja na majibu muafaka kwa jamii ambayo kimsingi imekuwa kama watazamaji tu ilihali sherehe ni yao!

3) Tundu Lissu Hana kashfa yoyote ndani ya taifa hili.

4) Tundu Lissu ni jasiri wa asili yake, ambae wakati wote huenda mbele tuu, na kamwe harudi nyuma katika lile analolisimamia.

5) Ndiye Mwanasheria ambaye anaweza kutupatia katiba ya wananchi ambayo wanasiasa wengi wameonesha uoga kuitetea!

6) Ni kijana pia, ambapo katika daftari la wapiga kura; wengi wao ni vijana.

7) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kuhoji mambo yaliyopinda hivyo anawezakutoa changamoto kubwa kwa wale walio madarakani sasa.
Sababu ziko nyingi mnaweza kuziongeza

Na mwisho pengine niseme hivi labda nitaeleweka zaidi.

Ukawa, au tuseme upinzani kwa ujumla, kutokumtumia mwanasheria huyu mbobevu katika eneo hili muhimu, hiyo haina tofauti kabisa na ile hadithi ya wale wazungu wa kale waliowakuta wasukuma wa Mwadui Shinyanga; wakicheza bao kwa kutumia vipande vya almasi kama kete!!

Je wewe unasemaje kuhusu hili?
Acha kuchekesha wewe yaani tundu lisu apambane na jemedari magufuri, mapema sana! Mtaanza kulalama oooh kura zimeibiwa
 
Back
Top Bottom