Mchokoo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2015
- 1,179
- 1,579
Wadau, nimewaza sana kuhusu nani anafaa kuipeperusha bendera ya UKAWA mwaka 2020 kwenye nafasi ile nyeti.
Kwa upande wa CCM najua kuwa bado mheshimiwa John Pombe Magufuli ataendelea kugombea kulingana na utaratibu uliozoeleka.
Hata hivyo changamoto kubwa bado inasaria kwenye vyama vinavyounda Ukawa! Ni yupi safari ijayo; anafaa kugombea urais kupitia wa vyama hivi?
Hili ni swali moja kubwa mno, si kwao tu bali na kwa watanzania kwa ujumla.
Swali ambalo kulingana na unyeti wake, linahitaji uwekevu wa hekima, au tuseme utulivu wa mawazo unaoweza kupalilia njia ya kuliendea jawabu, kinyume kabisa na ule utaratibu wa kukimbilia majibu mepesi; ambayo aghalabu huwa hayawezi kukidhi haja ya jamii yenye upevu wa kifikra.
Pengine kabla sijaanza kuitetea hoja yangu; ni vizuri watawala wetu; katika nyakati zote, wakafahamu kwamba watanzania wa leo wanahitaji maisha bora tu, na si hadithi za alfulela-ulela.
Sasa kwenye mada, kwa nini Tundu Antipas Lissu na si mwingine?
1) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja mpaka mtoto mdogo akamwelewa!
Ukizingatia kuwa nchi yetu kwa sasa uelewa wa watu si haba, na unazidi kuongezeka kila mwaka.
2) Tundu Lissu ni Mwanasheria mwenye akili nyingi, na mtazamo mpana mno!
Na kwa kutumia ufahamu wake huo atasaidia sana wakati wa kampeni kuongeza ushawishi pindi atakapogusa nyanja mbalimbali na kuja na majibu muafaka kwa jamii ambayo kimsingi imekuwa kama watazamaji tu ilihali sherehe ni yao!
3) Tundu Lissu Hana kashfa yoyote ndani ya taifa hili.
4) Tundu Lissu ni jasiri wa asili yake, ambae wakati wote huenda mbele tuu, na kamwe harudi nyuma katika lile analolisimamia.
5) Ndiye Mwanasheria ambaye anaweza kutupatia katiba ya wananchi ambayo wanasiasa wengi wameonesha uoga kuitetea!
6) Ni kijana pia, ambapo katika daftari la wapiga kura; wengi wao ni vijana.
7) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kuhoji mambo yaliyopinda hivyo anawezakutoa changamoto kubwa kwa wale walio madarakani sasa.
Sababu ziko nyingi mnaweza kuziongeza
Na mwisho pengine niseme hivi labda nitaeleweka zaidi.
Ukawa, au tuseme upinzani kwa ujumla, kutokumtumia mwanasheria huyu mbobevu katika eneo hili muhimu, hiyo haina tofauti kabisa na ile hadithi ya wale wazungu wa kale waliowakuta wasukuma wa Mwadui Shinyanga; wakicheza bao kwa kutumia vipande vya almasi kama kete!!
Je wewe unasemaje kuhusu hili?
Kwa upande wa CCM najua kuwa bado mheshimiwa John Pombe Magufuli ataendelea kugombea kulingana na utaratibu uliozoeleka.
Hata hivyo changamoto kubwa bado inasaria kwenye vyama vinavyounda Ukawa! Ni yupi safari ijayo; anafaa kugombea urais kupitia wa vyama hivi?
Hili ni swali moja kubwa mno, si kwao tu bali na kwa watanzania kwa ujumla.
Swali ambalo kulingana na unyeti wake, linahitaji uwekevu wa hekima, au tuseme utulivu wa mawazo unaoweza kupalilia njia ya kuliendea jawabu, kinyume kabisa na ule utaratibu wa kukimbilia majibu mepesi; ambayo aghalabu huwa hayawezi kukidhi haja ya jamii yenye upevu wa kifikra.
Pengine kabla sijaanza kuitetea hoja yangu; ni vizuri watawala wetu; katika nyakati zote, wakafahamu kwamba watanzania wa leo wanahitaji maisha bora tu, na si hadithi za alfulela-ulela.
Sasa kwenye mada, kwa nini Tundu Antipas Lissu na si mwingine?
1) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja mpaka mtoto mdogo akamwelewa!
Ukizingatia kuwa nchi yetu kwa sasa uelewa wa watu si haba, na unazidi kuongezeka kila mwaka.
2) Tundu Lissu ni Mwanasheria mwenye akili nyingi, na mtazamo mpana mno!
Na kwa kutumia ufahamu wake huo atasaidia sana wakati wa kampeni kuongeza ushawishi pindi atakapogusa nyanja mbalimbali na kuja na majibu muafaka kwa jamii ambayo kimsingi imekuwa kama watazamaji tu ilihali sherehe ni yao!
3) Tundu Lissu Hana kashfa yoyote ndani ya taifa hili.
4) Tundu Lissu ni jasiri wa asili yake, ambae wakati wote huenda mbele tuu, na kamwe harudi nyuma katika lile analolisimamia.
5) Ndiye Mwanasheria ambaye anaweza kutupatia katiba ya wananchi ambayo wanasiasa wengi wameonesha uoga kuitetea!
6) Ni kijana pia, ambapo katika daftari la wapiga kura; wengi wao ni vijana.
7) Tundu Lissu ana uwezo mkubwa wa kuhoji mambo yaliyopinda hivyo anawezakutoa changamoto kubwa kwa wale walio madarakani sasa.
Sababu ziko nyingi mnaweza kuziongeza
Na mwisho pengine niseme hivi labda nitaeleweka zaidi.
Ukawa, au tuseme upinzani kwa ujumla, kutokumtumia mwanasheria huyu mbobevu katika eneo hili muhimu, hiyo haina tofauti kabisa na ile hadithi ya wale wazungu wa kale waliowakuta wasukuma wa Mwadui Shinyanga; wakicheza bao kwa kutumia vipande vya almasi kama kete!!
Je wewe unasemaje kuhusu hili?