Ujumbe Kwa CloudsFM na Gerald Hando

WADAU. Nimekuwamsikilizaji wa kipindi cha asubuhi cha Clouds FM cha Power Breakfast, ambachoni maarufu sana siku hizi, siku za karibuni GERALD HANDO kupitia segment yakeya Jicho la Ng’ombe amedhihirisha dhamira yake hasi kwa taifa letu, dhamirailiyojaa unafiki mkubwa.
HakikaGerald amejivika kuwa mtetezi wa maovu ya serikali, hususan bajeti hii ambayohata serikali yenyewe imekiri kuwa ni mbovu ikifanya mkakati wa kuiboresha.Ndugu zangu wenye nia thabiti ya kuleta mabadiliko katika mfumo mbovu wa serikalihii, nawaomba tuungane kwa nguvu zetu zote kukataa propaganda chafu za GeraldHando (siamini kama ni msimamo wa Clouds Fm kama ndivyo wawathibitishiewananchi).

Leo asubuhiamewakejeli wabunge wetu wote wanaoikosoa bajeti hii, akidai wanatafutaattention kwa wananchi, tena akienda mbali kwa kudai ni watovu wa nidhamu kwababa yao (Rais), tena hawafanyi kilichowapeleka bungeni. Hivi yeye ni nanimpaka atoe kashfa zote hizo? Au kwa kuwa amepewa jukwaa la kubwabwaja. Hakikanimemshusha thamani kwa hoja zake dhaifu!
Wadau,naandika kwa urefu nikiwa very disappointed na hawa wana habari uchwara (kamaGerald Hando) ambao wanaweka maslahi yao badala ya umma. Sielewi kwa mtazamo waGerald Hando wabunge kazi yako bungeni ni ipi kama sio kuihoji na kuibanaserikali, yawezekana hawafahamu hata majukumu ya mbunge (inataka elimu ilikujua hilo sijui kama anayo), anataka waende kusinzia kama baadhiwalivyochukuliwa na picha?.
Iwapoameamua kuwa msemaji wa serikali ya CCM, basi tujulishwe kwani hatuna tatizo naRadio Uhuru amabyo ni propaganda machine ya CCM, kila mtu anajua hilo na hatuna tatizao nalo, ilawapigania ukombozi wa kweli tutaendelea kuibana serikali, tukiwatumia wabungewetu kama Mnyika kueleza umma uozo wa serikali hii, asitukatishe tama kwanihatofanikiwa kamwe. Hongera Mnyika tuko nyuma yako katika hili.
Aluta Kontinua mpakaserikali itambue haki ya wananchi. Ole wao wanafiki siku zao zinahesabika

Hicho kipindi kilikufa baada ya "vichwa" wawili kutoka pale. Kipanya na hasa Fina Mango. Huyo Hando ndio aliwasaliti hao wawili hadi wakafukuzwa kazi. mwisho wa CCM ndio mwisho wa Radio hii
 
Hata akiwatukana wabunge Magamba , hawathubutu kumwita bungeni kama walivyofanya kwa Mama Teri. Gamba linazidi kunyauka.
 
Clauz dhaifu,gerad dhaifu,kibonde dhaaaaiifuuuuuuuuuuuuuu,shame on you wote wenye fikra za chama kimoja.
 
Kama kumbukumbu zangu hazinidanganyi huyu jamaa ndo aliwasailiti akina Fina Mango na Kipanya katika kitu walichokusudia kukifanya kwa pamoja pamoja,so historia inaonyesha huyu jamaa ni wa kuogopwa ,in short ni mnafiki sana.Mimi nilishaachaga kusikiza hii redio ya chama zamani sana.
 
Mengine sijui lakini kwa hili alilosema asubuhi nadhani mtoa post hajamtendea haki. Nasema hivyo kwa sabb nimemsikia vizuri Gerad na msingi wa hoja yake ilikuwa kwa wabunge na mawaziri wa ccm kumchangia pesa mwiguru kwa matusi aliyochangia juzi. Then alijaribu kuonesha kuwa sio vyema wabunge kujadili watu badala ya kujadili bajeti. Namlaani kwa kusema kuwa Mnyika (ingawa hakumsema kwa jina) kamkosea adabu JK, kwangu nadhani Mnyika alitumia busara ya juu sana kumuelezea huyu raisi wetu, hakuna namna nyingine ya kumuelezea zaidi ya kusema kuwa ni "raisi dhaifu", kama ipo watuambie!!!!!!
 
huwa kuna wakati narudi nyuma na kujiuliza ilikuwaje Sugu akafanya suluhu na watu wa aina hii wanatafuta kula yao wanajikomba popote mradi maisha yao yaende??????? Ilikuwa Wafu Fm sijui imefufukaje??
 
Kosa lako ni kusikliza hiyo radio.

Sasa angalia alivyo kukera,yan ungekuwa na mke mwenye mimba si ange kereka mpaka mimba ingetoka.
 
Ili usipate pressure za bure, sikiliza kipindi cha leo tena kama unaona ni lazima kuisikiliza radio clouds!!
Watangazaji wengi wa wafu fm pamoja na mmiliki wake wameshajidhihirisha siku nyingi wako upande wa serikali ya raisi dhaifu, sasa sijui hapo mtu utategemeaje maoni tofauti kutoka kwao.
 
Hao wakina Gerald Hando na baadhi ya wafanyakazi wengine wa Cloudsfm wanaamini kuwa nidhamu ya uoga, kujikomba-komba na kujipendekeza kwa mkuu ndio suluhisho la matatizo yao binafsi, inawezekana ikawa kweli. Ila Taifa alitajengwa kwa mawazo yao mgando. Tunahitaji watu wenye uthubutu wa kusema ukweli uliopo :sad: hatakama itawagharimu maisha yao kwa manufaa ya vizazi vijavyo !
 
Alikua analilia ukuu wa wilaya kumbe yupo serious!
Clouds wanajikomba sana kwa kuandaa vishereha vya birthday za hao wadhaifu!

Nami nilisikia siku hiyo alivyokuwa analalamimika kukosa ukuu wa wilaya. Ukiona hivyo kuna kitu kaahidiwa na mzee dhaifu
tusikilizie siku za karibuni tuone
 
Kwa fikra kama za Hando, bila shaka meya Masaburi hatakosea kama akisema huyo mtangazaji anafikiri kwa kutumia makalio! Tehe!tehe!
 
Back
Top Bottom