Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,821
- 59,411
Hamna ubaya wowote mtu kuwa karibu na jiraniye maana ukaribu huo unaweza ukazaa urafiki sawa na undugu ukapata mtu wa kusaidiana nae.
Anyway kuna ambalo mie nimeshindwa kujua nia yake kwahiyo nataka kujua wanajamvi mnalionaje.
Kuna wanandoa wamehamia sehemu mpya hata mwezi haujaisha, wanapoishi ni ndani ya geti ambapo mwenye nyumba anaishi pamoja na mpangaji mwingine (mtu na mkewe, mtoto na dada wa kazi).
Hawa wapangaji wapya hawana dada wa kazi ila mke ni mjamwepesi kwahiyo kushirikiana muhimu. Sasa juzi jioni kaka alikua anamsaidia mkewe kuosha vyombo nje kwenye karo wakati ye anapika, mara yule mke wa jirani yao (mpangaji mwenza) akatoka nje na kumkuta yule kaka akiosha vyombo. Yule dada akamuuliza 'kheee unaosha vyombo'? Kaka akajibu 'ndio' tu alafu akaendelea. Dada akatoa offer. . .'acha nanii (dada wake wa kazi) atakusaidia'.
Sasa mhusika anajiuliza na kuuliza ni kwamba yule jirani aliona mumewe anaonewa kuosha vyombo akamuonea huruma ama? Au jirani anachokonoa tu ya watu akiwa hajui wanaishi vipi?Inahusu kutoa msaada kwa mume wa mtu bila kuombwa ikiwa mkewe yupo? Au ndio mafumbo ya "kwanini unaosha
vyombo na mwanamke unae?"
Mie nimeshindwa kujua kama ndo kujaliana kwa majirani au kuna jingine.
Anyway kuna ambalo mie nimeshindwa kujua nia yake kwahiyo nataka kujua wanajamvi mnalionaje.
Kuna wanandoa wamehamia sehemu mpya hata mwezi haujaisha, wanapoishi ni ndani ya geti ambapo mwenye nyumba anaishi pamoja na mpangaji mwingine (mtu na mkewe, mtoto na dada wa kazi).
Hawa wapangaji wapya hawana dada wa kazi ila mke ni mjamwepesi kwahiyo kushirikiana muhimu. Sasa juzi jioni kaka alikua anamsaidia mkewe kuosha vyombo nje kwenye karo wakati ye anapika, mara yule mke wa jirani yao (mpangaji mwenza) akatoka nje na kumkuta yule kaka akiosha vyombo. Yule dada akamuuliza 'kheee unaosha vyombo'? Kaka akajibu 'ndio' tu alafu akaendelea. Dada akatoa offer. . .'acha nanii (dada wake wa kazi) atakusaidia'.
Sasa mhusika anajiuliza na kuuliza ni kwamba yule jirani aliona mumewe anaonewa kuosha vyombo akamuonea huruma ama? Au jirani anachokonoa tu ya watu akiwa hajui wanaishi vipi?Inahusu kutoa msaada kwa mume wa mtu bila kuombwa ikiwa mkewe yupo? Au ndio mafumbo ya "kwanini unaosha
vyombo na mwanamke unae?"
Mie nimeshindwa kujua kama ndo kujaliana kwa majirani au kuna jingine.