Ujasusi / Upelelezi / Udukuzi: Maana yake halisi na uhatari wake

Yericko Nyerere

JF-Expert Member
Dec 22, 2010
16,987
20,271
Fuatana nami.....

Mpelelezi ni mtu anayekusanya taarifa za adui , mshindani wa biashara au serikali adui ila saa nyingine mpelelezi huyo anaweza kufanya kazi ya kumpeleleza adui ila akamgeuka basi wake aliyemtuma kwa sababu mbalimbali .

Mtu huyu huwa anakusanya taarifa hizi kwa siri kwa kuangalia , kusikiliza , kufuatilia na kutumia vifaa vingine kutokana na ukuaji wa tekinolojia lakini lengo ni lile lile kupata taarifa za siri bila mhusika , wahusika kujua kwamba taarifa zao zinachukuliwa .

Shuguli za upelelezi zimekuwepo kwa miaka mingi toka binadamu ameanza kuishi duniani na kila kipindi zinabadilika utokana na ukuaji wa binadamu kimbinu , vifaa na wahusika wenyewe .

Kutokana na kukua kwa tekinologia watu wengi wametumia tekinologia hizo kukusanya taarifa na kuacha njia za asili ya upelelezi ambazo wakati mwingine ni sahihi kabisa kwa wakati huu .

Ili jamii Fulani isonge mbele kwenye maendeo Fulani ni vizuri iwekeze sana kwenye nyenzo na vitendo vya kipelelezi na hujuma kwa kuwa na watu wazuri kila sehemu pamoja na vifaa.

Labda tujiulize sasa kwanini kuna upelelezi , kwanini watu wanakuwa wapelelezi , mtu anavutiwa kukusanya taarifa za siri za mtu au kampuni au serikali nyingine kwa njia ya siri ?

Kwa kweli hakuna maana moja ya kwanini mtu anaamua kuwa mpelelezi au anaamua kusaliti wenzake kwenye upelelezi na kwenda upande wa adui lakini kuna vichocheo vinne vikuu ambavyo vinatumika kwenye shuguli hizi .

Kitu ambacho kinaweza kuwa namba moja ni hela , fedha au uchumi . kama nchi jirani imeshindwa kabisa kuingiza wapelelezi ndani ya baraza la mawaziri ili kupata taarifa kutumia njia za kawaida basi pesa inaweza kutumika katika kuhonga watu haswa wasaidizi au mawaziri wenyewe hata viongozi wengine ili kupata taarifa wanazozitaka .

Ushindani wa viwanda na biashara kati ya nchi au kampuni unategemeana sana na fedha ambazo hutolewa kwa wapelelezi au wachunguzi wengine ili kupata siri za mshindani wake sokoni au popote .
Katika shuguli za kijeshi zinazofanywa na nchi moja dhidi ya nyingine au vikundi vya kigaidi na vya kihalifu fedha hutumika sana na mfano hao ni tunaposikia kuhusu kundi la al shabab kuhonga baadhi ya polisi wa mipakani ili wavushe silaha na watu kwa ajili ya kufanya mashambulizi au wapewe taarifa mapema wakati polisi wanapofanya msako kwenye maeneo yao .

Kichocheo cha pili ni Itikadi ambayo ni Msimamo au mtazamo kuhusu masuala Fulani ya kimaisha , dini , imani , uongozi na mengine mengi hapa kwenye itikadi ndio makundi mengi ya kigaidi yanachipukia na kupata watu wa kujiunga nao wakifuata mtizamo na misimamo ya imani yao . vyama vya siasa navyo vinapata wafuasi wao kutokana na hili la itikadi ingawa wengine wanaweza kuwa sio wasomi wa itakadi wala kuielewa wanafuata mkumbo mpaka wanapoumizwa au kuumiza wengine ndio wanashtuka kitu ambacho wanakuwa wamechelewa .

Kwahiyo ili uwe mpelelezi mzuri wa kundi la kigaidi lazima uelewe itakadi yao , nchi , vikundi au vyama vya siasa na vikundi vingine vya siri .

Ili serikali na wadau wengine waweze kukabiliana na vikundi vya kigaidi ni vizuri kuwekeza sana kwenye suala la kujua itikadi za vikundi wanavyopambana navyo .

Hapa kwenye itikadi ndipo uzalendo unatakiwa kujengwa kwa vijana , watoto na wengine kwenye taasisi za elimu ili wasiweze kuangukia kwenye mikono ya wahalifu na maadui wengine kutokana na itikadi zao mfano china wana ukomunisti , nchi za magaribi wana itikadi zao na mengine mengi .

Wakati mwingine watu au mtu anaweza kuingia kwenye makubaliano na adui baada ya kukamatwa akifanya upelelezi au hata kabla lakini adui anaweza kuona yeye anafaa akampa mafunzo na mbinu nyingine ili aweze kupelelezi kwa niaba ya adui huyo mwisho wa makubaliano kama haya mara nyingi ni watu kuuwawa na hujuma nyingine nyingi dhidi ya nchi yake au watu wake wa karibu .

Mmoja wa wapelelezi maarufu kwenye suala hili anaitwa Kamanda Zig Zag , yeye alikua mfungwa kwenye gereza la uingereza kwenye kisiwa Fulani kisiwa hicho kilivyotekwa na wajerumani yeye akaandika barua kutaka kujiunga na jeshi la kijerumani baada ya muda alipelekwa ufaransa kwa mafunzo kisha akatumwa uingereza ili akalipue kiwanda cha kutengeneza ndege za kivita . Alivyotua uingereza akatoa taarifa kwa mamlaka za uingereza sasa akawa upande wa uingereza tena akatengeneza mlipuko bandia na kuaminisha wajerumani kwamba kweli kimelipuliwa kisha waingereza wakamtuma arudi ujerumani kwahiyo akawa mpelelezi wa uingereza ndani ya ujerumani .wajerumani walimtuma maeneo mengi ulaya kwa kudhani anawasaidia kumbe taarifa zote zilikuwa zinaenda kwao uingereza .

Kuna wakati mtu analazimika kufanya upelelezi dhidi ya mtu au watu baada ya nguvu kutumika au kulazimishwa ili labda asiuwawe au ndugu zake wa karibu asiuwawe mara nyingi wanaweza kutumika wapenzi na wapendwa wengine ili mtu afikie muafaka wa kufanya upelelezi dhidi ya nchi , kampuni , washirika na wengine wa karibu .

Hapa kwenye nguvu wakati mwingine mtu anaweza kusingiziwa kitu au kuingizwa kwenye kashfa au kutengenezwa uwongo ili akubali kufanya upelelezi dhidi ya wengine lakini sio kwa hiari yake .

Pia kuna suala la umuhimu au umaarufu wa mtu au uzuri wake , kuna watu wengi maarufu kama wanamuziki au wacheza mpira na warembo wanatumia fursa hiyo kufanya upelelezi dhidi ya maadui wa nchi zao au washindani wa kibiashara wanajua kwa kutumia njia hiyo wanaweza kuingia chumbani , kulala na wanaume au wanawake , kuchungulia simu au kuweka vinasa Sauti , kujua marafiki au ndugu wa karibu , mipango ya biashara na mengine mengi .

Baadhi ya watu haswa vijana wanajiingiza au wanaweza kuingizwa kwenye shuguli za kipelelezi kwa wao kupenda vile wanavyoona kwenye sinema au kusoma vitabu au kuhadithiwa na wao wanaamua kujihusisha na upelelezi lakini bila kuwa na mafunzo au mtu yoyote anayemuongoza kwenye mambo mbalimbali anayotakiwa kufanya .

Wengine wanaweza kuwa wapelelezi wazuri ndani ya polisi , majeshi na kampuni lakini hawalipwi vizuri au hawaridhiki na baadhi ya vitu matokeo yake ni kuuza siri na mikakati mengine kwa wapinzani au maadui ili kuweza kuleta mabadiliko na mengine ndani ya taasisi yake au kuiua kabisa isiwepo .

Mahusiano binafsi kati ya watu au mtu ni moja ya kichocheo kikubwa cha watu kuweza kufanya upelelezi mara nyingi yanaweza kuwa mahusiano ya kifamilia kuoleana , kuowa au kuolewa hii maarufu inaitwa HONEY TRAP na hii ni ngumu kugundulika kwa sababu ni mambo binafsi sana na yanaweza kuchukua muda mrefu kwenda vizazi na vizazi viongozi na viongozi .

Kama nilivyosema hapo juu upelelezi umeanza siku nyingi na kila jamii inategemea upelelezi ili iweze kujua mwingine ili kuweza kupambana au kushindana nae ili aweze kuwa juu kwenye mambo mbalimbali na upelelezi umebadilika kwa kiasi kikubwa sana .

Ni vizuri taasisi zetu kuwekeza vizuri kwenye upelelezi kupata vijana hodari , wapewe mafunzo ya kutosha , mishahara , motisha , vifaa na kuzidi kuwaongezea ujuzi ili kuweza kupambana katika dunia ya sasa ya sayansi na tekilologia .

Upelelezi usiishie ndani ya jeshi la polisi au JKT , au Usalama wa Taifa tu , hata vyuo vinatakiwa kuwa na wapepelelezi , kampuni za nchini zinatakiwa kuwa na wapepepezi , mashirika ya umma yanatakiwa kuwa na wapelelezi , viwanda vya ndani vinatakiwa kuwa na wapelelezi na wote hawa wanatakiwa kufanya kazi pamoja ili kuleta maendeleo kwa jamii ya watanzania .

Nchi za wenzetu zinaendelea na kuendeleza ushindani mkubwa kwenye nyanja hii , uchina ilishtuka ikapeleka wapelelezi nchi nyingi ili wakalete tekinolojia na maarifa kwao sasa wako mbali , wakati wa vita kuu ya dunia wamarekani waliiba wanasayansi wengi wa ujerumani ambao walisaidia kujenga uwezo mkubwa wa jeshi la marekani na taasisi nyingine ndio maana ikawa mbabe wa dunia kwa kipindi kirefu .

Kumbuka kazi za upelelezi ni ngumu na zenye siri nyingi na kubwa sana , wapelelezi wengi pia wana mafunzo ya kujilinda , kupambana na kushambulia usijaribu kupambana nae kama una uhakika ni bora kutoa taarifa kwa vyombo husika wamshugulikie .

Mwisho upelelezi usitumike katika kutafuta taarifa mbaya tu , hapana , kuna taarifa nyingine nzuri zinaweza kutumika vyuoni , wizarani , kwenye majeshi na sehemu nyingine kwa ajili ya kuboresha au kujenga zana na vifaa vya kisasa

LENGO LA MAELEZO/MAKALA HAYA NI KUFUNDISHA, UKIKAMATWA KWA KAZI HIZI UNAWEZA KUUWAWA , KUTESWA NA KUPOTEZA MENGI.

Mkala haya ni marudio, kwa mara yakwanza niliandika April 21, 2011

.............................

"Kuna watu wasipokuelewa maneno na matendo yako, mshukuru Jah, wewe bado unafikra chanya, wakianza kukuelewa jichunguze ni wapi umeanguka maana umeanza kuwaza kama wao"
 
Polisi wanakitengo cha upepelezi, jwtz wanakitengo cha upepelelezi, jkt na magereza nao wanakitengo.

Sasa hapo ujasusi ni kitengo gani?
 
Polisi wanakitengo cha upepelezi, jwtz wanakitengo cha upepelelezi, jkt na magereza nao wanakitengo.

Sasa hapo ujasusi ni kitengo gani?

Nje ya TISS na JWTZ (TMI) hao wengine huitwa intelijensia tu, ama domestication intelligence's
 
Mkuu makala zako mara nyingi hunivutia mno, je kuna wapelelezi mpaka sehemu za ibada? Mfano sheikh, ustaadh au padre au askofu naam mchungaji anaweza akawa mpelelezi?
 
Kwanini sasa mambo yanayofanywa na nchi yaliyo ya siri au vikao vya mawaziri nyeti huliki agenda zao source ni nini haswa.
 
Kwa kuongezea nyama kidogo. Fedha na Blackmail ni njia moja wapo ya organization fulani kujipenyeza kwenye nyingine. Agents wa organization moja wana wa assess watu wa organization nyingine ambao ndo hasa wana interest nao. Interest utokana na how close hao agents au analysts wanaokuwa assessed wapo karibu na information inayotakiwa. Huwa wanaangalia weakness za mhusika. Kma ni mtu wa kupenda sana maisha ya juu basi hiyo ndo gia watayomuingia nayo. Watampa offer ambayo hawezi kukataa. Kwenye upande wa blackmail wanaangalia labda kuna kitu mhusika anacho ambacho amaekifanya siri kwa mwajiri wake na mbacho muajiriwa anaweza akapoteza kazi yake kwa hiyo yupo tayari kufanya lolote kuhakikisha siri haitoki. Kwa hiyo wakifanikiwa kumturn muhusika then mhusika ataaanza kuwapa information in exchange ya aidha fedha au siri yake kuendelea kulindwa. At that point mhusika anakuwa ni mole ndani ya organization aliyoajiriwa na upande wa pili ya ambao ndo wanahitaji information anakuwa ndo kama asset wao. Huyu asset anakuwa assigned mtu anajulika kama handler ambaye ndo kazi yake kuhakikisha ana maintain mawasiliano na huyu Asset kwa kufuata muongozo fulani ambao unakuwa umetengenezwa na hiyo organization. Kama ulivyosema ujasusi huwa haushishiii kwenye serikali tu. Big companies zinachunguzana ili kujua trade secrets za mwingine. Kwa Tanzania ujasusi upo kiserikali. Unapokuwa mtu prominent au taasisi kubwa au hata chama cha siasa chenye mwelekeo wa kushika dola kuchunguzwa ni muhimu. Kwa hiyo chama kama Chadema lazima wafuatiliwe kujua agenda zao.
 
Mkuu makala zako mara nyingi hunivutia mno, je kuna wapelelezi mpaka sehemu za ibada? Mfano sheikh, ustaadh au padre au askofu naam mchungaji anaweza akawa mpelelezi?

Kwa aina ya mfumo wa kijasusi nchini, kila mtu maarufu yupo chini ya wapelelezi.

Kila taasisi ipo chini ya wapelelezi,

Lakini tatizo moja nikuwa upelezi unaofanywa nchini ni wa kiserikali tu.
 
Kwa kuongezea nyama kidogo. Fedha na Blackmail ni njia moja wapo ya organization fulani kujipenyeza kwenye nyingine. Agents wa organization moja wana wa assess watu wa organization nyingine ambao ndo hasa wana interest nao. Interest utokana na how close hao agents au analysts wanaokuwa assessed wapo karibu na information inayotakiwa. Howa wanaangalia weakness za mhusika. Kma ni mtu wa kupenda sana maisha ya juu basi hiyo ndo gia watayomuingia nayo. Watampa offer ambayo hawezi kukataa. Kwenye upande wa blackmail wanaangalia labda kuna kitu mhusika anacho ambacho amaekifanya siri kwa mwajiri wake na mbacho muajiriwa anaweza akapoteza kazi yake kwa hiyo yupo tayari kufanya lolote kuhakikisha siri haitoki. Kwa hiyo wakifanikiwa kumturn muhusika then mhusika ataaanza kuwapa information in exchange ya aidha fedha au siri yake kuondlea kulindwa. At that point mhusika anakuwa ni mole ndani ya organization aliyoajiriwa na upande wa pili ya ambao ndo wanahitaji information anakuwa ndo kama asset wao. Huyu asset anakuwa assigned mtu anajulika kama handler ambaye ndo kazi yake kuhakikisha ana maintain mawasiliano na huyu Asset kwa kufuata muongozo fulani ambao unakuwa umetengenezwa na hiyo organization. Kama ulivyosema ujasusi huwa haushishiii kwenye serikali tu. Big companies zinachunguzana ili kujua trade secrets za mwingine.

Excellent!!!!
 
Last edited by a moderator:
Intellijensia ya nchi hii ni noma, hakuna ambapo hawapo, misikitini, makanisani, mitaani, wachoma chips, ma baa maid, hata wale wazee mafundi cherehani mbele ya maduka ya wahindi wengi wao wako ktk system. Hata baadhi ya masheikhe, mapadre, maaskofu, wachungaji nk. katika suala la upelelezi Tanzani ni kitu ingine
 
Mkuu makala zako mara nyingi hunivutia mno, je kuna wapelelezi mpaka sehemu za ibada? Mfano sheikh, ustaadh au padre au askofu naam mchungaji anaweza akawa mpelelezi?

Wapo mfano padre slaa,shekh issa ponda akina john mnyika
 
Back
Top Bottom