mwanapolo
Senior Member
- Mar 29, 2011
- 193
- 56
Leo asubuhi kulikuwa na tukio la kutaka kupora hela zilizokuwa zinaingia ofisi ya kuuzia madini ya Classic, kwenye purukushani hizo majambazi walimpiga risasi mlizi Joseph na kumwua hapohapo ila walishindwa kupora hela kwani zilikuwa ziengizwa ofini tayari. Inaonyesha hao majambazi walikuwa na habari kuwa kuna hela inaingia kwenye hiyo ofisi ndio maana waliweka mitego pale ofsini kwa nje.
Kilichonisikitisha zaidi ni kumuua mlinzi ambae hana kosa lolote na pia alikuwa mtu wa watu, vijana wote wanao uza Tanzanite kwenye hiyo ofisi ni rafiki nao. na matukio kama haya tulikuwa tumeyasahau hapa arusha kwetu, kuna mkono wa mtu hapa kwenye hili tukio na polisi wanamjua na yupo uraiani kwa sasa.
Kilichonisikitisha zaidi ni kumuua mlinzi ambae hana kosa lolote na pia alikuwa mtu wa watu, vijana wote wanao uza Tanzanite kwenye hiyo ofisi ni rafiki nao. na matukio kama haya tulikuwa tumeyasahau hapa arusha kwetu, kuna mkono wa mtu hapa kwenye hili tukio na polisi wanamjua na yupo uraiani kwa sasa.