Waziri wa madini
JF-Expert Member
- Jun 12, 2019
- 379
- 465
Habari Wana JF Leo naandika huku machozi yananilengalenga.
Mimi ni mfanyakazi katika moja ya taasisi iliyo chini ya Serikali, kitu kilichonisukuma kuandika uzi huu ni kutaka kuamsha fikra za umoja na usawa katika imani zetu sehemu zetu za kazi kuna haja ya makusudi kuwepo usawa na hali ya kuvumiliana katika masuala ya kiimani ukizingatia Taifa letu ni moja na sisi ni wamoja na serikali haina dini Ila inaheshimu na kutambua dini zote.
Kuna matukio ambayo yamekuwa na muendelezo mbaya katika baadhi ya maofisi na mashirika mbalimbali binafsi ntajitolea mfano wangu.
Ikitokea nikawa nataka kufanya ibada kwa mujibu wa taratibu za dini yangu kwakuwa mimi ni muumini ninayefanya ibada mara tano kwa siku imekuwa changamoto kubwa kwanza naonekana kama mdini japo sijawahi kuhubiri kuhusu dini ,
Yani Ile kuhakikisha nafanya tu ibada hainipiti naonekana mdini na watu wanajadili, lakini hali tofauti kwa wenzangu wa Imani tofauti wao mtu akiwa mfanyaji ibada na mtu wa Imani thabiti anaoneka ni mtu sahihi na mchamungu hasa tena mtu mwema mwenye upendo, hautosikia mijadala kumuhusu wala kumuhoji.
Kuna siku tulikuwa tupo katika semina, basi kama ada ikabidi tufungue kwa maombi kiukweli nilishtushwa sana na matokeo yaliyotokea siku hyo.
Kwanza tulitakiwa tusimame,tufumbe macho na kufata kanuni na taratibu za kuitikia maombi ya dini nyingine hata kama taratibu zile na maombi yale yana ukakasi kwa upande wa Imani yangu, pili maombi ya upande mmoja tu yalitosha kufungua na kufunga Ile semina pasi na kuhusisha maombi au duah za imani nyingine hali ya kuwa inatambulika tupo katika mchanganyiko wa Imani.
Kuna mdada mmoja alikuwa ni bosi katika kitengo fulani ,watu walimuundia zengwe kwa kigezo cha udini kisa tu alikuwa yupo katika Imani tofauti na Imani ya mastafu wengi wa hapamean kulitengenezwa kama umoja Fulani wa kiibada sasa yeye pekee ndio alikuwa na Iman tofauti na wenzake wengi, waka waambia madereva waseme dada yule huwa anachagua madereva wa Imani yake tu pindi anapotaka kwenda safari,Basi dada wa watu akapigwa chini japo alikuwa mtendaji mzuri.
Lengo na kusudio la mada hii ni kwamba tuheshimu na kuthamini Imani za wenzetu Hakika ubaguzi ni dhambi mbaya Sana na yenye madhara makubwa .
Taifa letu limejengwa kwa misingi ya umoja ,upendo na kuvumiliana .
Tusiwekeze katika udini na ukabila haya Mambo yatatukwamisha katika kufikia mafanikio Kama Taifa.
Tusiweke chuki ya udini na ubaguzi au baadhi kujiona wao ndio wapo sahihi na wenzao wamepotea sababu niliwahi kumsikia mtu hapa kazini akisema yani nataman hata watu wa imani fulani wasiwepo hapa kazini sababu kila mtu wa Imani Ile ni mshirikina na anamajini. Haya Mambo yanaleta chuki na kuondosha upendo.
Kama ikiwa viongozi wetu wa dini ni wamoja wanakaa pamoja na kuwa wamoja na hata dini zetu zimetufunza umoja kwa nn tunabaguana sisi sote ni watoto wa mama mmoja WaArika na WaTanzania tupendane tuheshimiane ,tuilinde tunu yetu ya amani.
Mimi ni mfanyakazi katika moja ya taasisi iliyo chini ya Serikali, kitu kilichonisukuma kuandika uzi huu ni kutaka kuamsha fikra za umoja na usawa katika imani zetu sehemu zetu za kazi kuna haja ya makusudi kuwepo usawa na hali ya kuvumiliana katika masuala ya kiimani ukizingatia Taifa letu ni moja na sisi ni wamoja na serikali haina dini Ila inaheshimu na kutambua dini zote.
Kuna matukio ambayo yamekuwa na muendelezo mbaya katika baadhi ya maofisi na mashirika mbalimbali binafsi ntajitolea mfano wangu.
Ikitokea nikawa nataka kufanya ibada kwa mujibu wa taratibu za dini yangu kwakuwa mimi ni muumini ninayefanya ibada mara tano kwa siku imekuwa changamoto kubwa kwanza naonekana kama mdini japo sijawahi kuhubiri kuhusu dini ,
Yani Ile kuhakikisha nafanya tu ibada hainipiti naonekana mdini na watu wanajadili, lakini hali tofauti kwa wenzangu wa Imani tofauti wao mtu akiwa mfanyaji ibada na mtu wa Imani thabiti anaoneka ni mtu sahihi na mchamungu hasa tena mtu mwema mwenye upendo, hautosikia mijadala kumuhusu wala kumuhoji.
Kuna siku tulikuwa tupo katika semina, basi kama ada ikabidi tufungue kwa maombi kiukweli nilishtushwa sana na matokeo yaliyotokea siku hyo.
Kwanza tulitakiwa tusimame,tufumbe macho na kufata kanuni na taratibu za kuitikia maombi ya dini nyingine hata kama taratibu zile na maombi yale yana ukakasi kwa upande wa Imani yangu, pili maombi ya upande mmoja tu yalitosha kufungua na kufunga Ile semina pasi na kuhusisha maombi au duah za imani nyingine hali ya kuwa inatambulika tupo katika mchanganyiko wa Imani.
Kuna mdada mmoja alikuwa ni bosi katika kitengo fulani ,watu walimuundia zengwe kwa kigezo cha udini kisa tu alikuwa yupo katika Imani tofauti na Imani ya mastafu wengi wa hapamean kulitengenezwa kama umoja Fulani wa kiibada sasa yeye pekee ndio alikuwa na Iman tofauti na wenzake wengi, waka waambia madereva waseme dada yule huwa anachagua madereva wa Imani yake tu pindi anapotaka kwenda safari,Basi dada wa watu akapigwa chini japo alikuwa mtendaji mzuri.
Lengo na kusudio la mada hii ni kwamba tuheshimu na kuthamini Imani za wenzetu Hakika ubaguzi ni dhambi mbaya Sana na yenye madhara makubwa .
Taifa letu limejengwa kwa misingi ya umoja ,upendo na kuvumiliana .
Tusiwekeze katika udini na ukabila haya Mambo yatatukwamisha katika kufikia mafanikio Kama Taifa.
Tusiweke chuki ya udini na ubaguzi au baadhi kujiona wao ndio wapo sahihi na wenzao wamepotea sababu niliwahi kumsikia mtu hapa kazini akisema yani nataman hata watu wa imani fulani wasiwepo hapa kazini sababu kila mtu wa Imani Ile ni mshirikina na anamajini. Haya Mambo yanaleta chuki na kuondosha upendo.
Kama ikiwa viongozi wetu wa dini ni wamoja wanakaa pamoja na kuwa wamoja na hata dini zetu zimetufunza umoja kwa nn tunabaguana sisi sote ni watoto wa mama mmoja WaArika na WaTanzania tupendane tuheshimiane ,tuilinde tunu yetu ya amani.