Uhafidhina ni nini hasa? Maana yake inapotoshwa...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
40,000
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina".

Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa.

Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? Au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?
 
Da kweli hili nebo watu wengi hawafahamu maana yake nahisi wanalisikia tu dichewelle na BBC swahili tu
 
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina". Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa. Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?

CC: Zitto Kabwe
 
Last edited by a moderator:
Ni tabu sana kujitetea unapokosa hoja. Matokeo yake ni kutoa maneno yasiyo na maana kabisa na yasiyoingia katika muktadha husika. Hebu angalia na hili "....nasikia wamenifukuza hata uwenyekiti wa PAC" Hivi kejeli kama hii maana yake nini? kwamba akina Baregu, Safari, Dr Slaa, Tundu Lissu, JJ Mnyika, Mbowe nk ni mambumbumbu ya ajabu yasiyoweza kujua nini wanafanya?
 
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina". Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa. Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?


Ngoja Tumsubiri faizaFox aje, maana tangu ule mjadala wa MS ulianzishwa na @Yerico Nyerere uishe yeye ana kazi moja tu ya Kumpinga @Mzee Mwanakijiji kwa kila kitu
 
Last edited by a moderator:
Kwa hiyo Mhishimiwa saaana, Mzee Mwanakijiji, Unataka kutuambia kwamba Mwishiwa ZZK ni MLIBERALI? Sijasema kama sasa ndo napata picha ni kwanini jamaa hajaoa mpaka leo!
Yeah kumbe ZZK ni mliberali tehe tehe.
 
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina". Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa. Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?

usipoandika ulichoandika makala zako kwenye gazeti la kufungia vitumbua tanzania daima hazitachapishwa na hivyo kukunyima ulaji unaopata kwa makala hizo, endelea kutumikia kafiri. WAHAFIDHINA ni pamoja na MADJ na Padri muasi ambao kwao malengo ya chma ni kubaki saccos ya watu wachache bila kutaka mabadiliko chanya.
 
Uhafidhina ni Conservatism, kwa kiingereza.Kwa lugha nyepesi ni hali ya kupenda uasili wa mambo kwa gharama yoyote hata kama mambo hayo yako relevant au irrelevant katika wakati husika. Neno hili hutumika kutoa maudhui yanayofanana na maana hiyo katika nyanja mbalimbali, lakini hutumika zaidi katika maswala ya siasa. Kwa mfano nchini Marekani Chama cha REPUBLICAN kinaweza kutambulika kama chama cha Kihafidhina kutokana na tendency yake ya kupenda historia ya Marekani ibaki, ambayo imetaliwa na ubaguzi na kutukuza watu wenye race nyeupe pamoja na matajiri, ikiwa ni pamoja na kupenda kulinda matajiri. Pia Chama cha CONSERVATIVE kinatambulika kama chama cha kihafidhina kutokana na historia ya siasa za Uingereza ambapo mabwanyenye walihodhi siasa za Uingereza kwa muda mrefu mpaka pale mabadiliko ya kimuundo ya jamii ya Uingereza yaliyopelekea kuibuka kwa matabaka ya Wafanyakazi na Wafanyabiashara kuwa na nguvu na kutaka kuwa na uwakilishi na pia kuongoza siasa za Uingereza, na ndio mwanzo wa vyama vya Labour pamoja na vingine vyenye mlengo kama huo. Sina uhakika Zitto aliliongea kwa maana gani katika speech yake ila kwa kuwa amekaa muda mrefu CHADEMA atakuwa yeye anajua alichokuwa anamahanisha. Katika hali ya sasa duniani vyama vyenye mlengo wa kulia vinahusishwa zaidi na uhafidhina tofauti na vile vyenye mlengo wa kushoto ambavyo vinapenda inclusion ya matabaka mbalimbali kama vile wahamiaji, maskini n.k. Tunaweza kujiuliza je Uhafidhina wa CHADEMA ni uhafidhina wa aina gani?
 
Uhafidhina ni ile hali ya kutokukubali mabadiliko au kuendelea kushikilia kushikilia misimamo ya kale

Msimamo wa kale wa Chadema ni upi?

Kuna watu wanataka kubeba historia ya CCM na kuiweka Chadema kwenye mizani ile ile ndio maana wanaanza kutumia maneno ambayo dhana yake ina mahala pake.
 
mwanakijiji....
huitendei haki nafsi yako
hulitendei haki taifa lako
huwatendei haki watanzani
huitendei haki taaluma yako
huvitendei haki vipaji vyako...............
una njaa sana ya tamaa ya mali kiasi cha kujitia upofu,ukiziwi na utaahira kiasi cha kuthamini malipo kidogo ya vipande vya dhahabu kupitia makala zako kwenye gazeti la MBOWE.. endeleeni kuyaita mabadiliko kwa jina jipya la uhaini lakini HAMTAFANIKIWA.
UHAFIDHINA sio dhana mpya na wengi wetu tunajua maana yake. ila kwa sababu safari hii neno hili linatumika dhidi ya wale wanaochangia ugali wako, basi unataka kutupa tafsiri mpya. karibu utupe tafsiri mpya kwani tunawajua nyie akina PRO-MANGI mko mbioni kuiandika upya kamusi ya kiswahili kwa kuabdilisha baadhi ya maneno kama vile
mabadiliko -kuwa mapinduzi
ufisadi ndani ya chadema-kuwa matumizi sahihi ya fedha
wataka mabadiliko kwa njia ya democrasia -kuwa wahaini n.k n.k n.k
 
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina". Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa. Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?

Nasubiri makala yako juu ya huu mnyukano mzee.
 
Mhafidhina ni mbowe(too local) na slaa ,ambao hawajali ukomo wa madaraka refer waraka wa ushindi 2013 in short wasiopenda demokrasia!!
 
Kama kuna neno linarudiwa rudiwa katika sakata linaloendelea sasa hivi ndani ya CDM ni kile kinachoitwa "uhafidhina" na wale wanaoita "Wahafidhina". Sijui kama ndugu zetu wanaotumia neno hili wanalitumia wakijua maana yake hasa au wanalipa maana isiyokuwa yake hasa. Uhafidhina kwani una matatizo gani gani? Na unalinganishwa na nini kwa upande mwingine maana katika siasa za kimataifa unapozungumzia "uhafidhina" unalinganisha na uliberali; je wale wanaopinga uhafidhina wao ni waliberali? au wao ni watu huru (independents) au ni waliberali-mamboleo (neo-liberalists); au wao ni wataka mabadiliko (progressives)? Au wale wenye msimamo mkali (fundamentalists) ndio wanachukuliwa kama wahafidhina?

Mwanakijiji kwa kujitia uziwi eti kwa sababu tu hilo neno limetumiwa na hasimu wake!

Uhafidhina kwa maana iliyo wazi kabisa ni 'kukataa kukubali mabadiliko'.

Hili neno linatokana na neno hifadhi. Kuhifadhi maana yake ni kutunza/ kuchunga kitu. Kwa hiyo ukiitwa mhafidhina kwa kifupi utakuwa ni mtu mwenye tabia ya kutaka kubakia katika hali uliyo nayo kitabia yaani rigidity.

Kwa hiyo kwa muktadha wa kinachoondelea sasa, CC ya CHADEMA imejaa wahafidhina i.e wako too local.

Ukipractice kitu ambacho wahafidhina hawajawahi kukisia, unaitwa msaliti.
 
Back
Top Bottom