Ugonjwa wa Tumbo kujaa maji

Siri ya sifuri

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
2,018
1,508
Salaam!

Wakuu nipo nyumbani wilayani Pangani mkoani Tanga namalizia msiba wa kaka yangu wadamu aliefariki katika hospitali ya taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu ikishirikiana na hospitali ya TMJ ya Mikocheni zote za Dar es Salaam.

Tatizo hasa lilikuwa Tumbo kujaa maji, kushindwa kula,kutapika na kwikwi isiyokoma, na kwabahati sana licha ya kufanyiwa kila aina ya vipimo ugonjwa anaougua haukuweza kugundulika,katika kipindi cha takriban miezi minne alichougua alianza kwa kulazwa katika hospital ya taifa Muhimbili Kisha wakamuhamishia TMJ.

Ili afanyiwe vipimo ambavyo Muhimbili hawana pamoja na kutolewa maji tumboni ambayo hujaa tena, kulikuwa na utaratibu wa kumtoa maji tumboni, kila siku ya alhamisi alitolewa maji drip mbili au tatu, alionekana kama kupata nafuu na tukatolewa tukamuuguze nyumbani.

Lakini maendeleo yake yalikuwa ya kusuasua mara apate nafuu mara azidiwe na hali ilipokuwa mbaya zaidi tulimrejesha tena TMJ ambapo alilazwa tena kwa uchunguzi zaidi na kwa mara nyingine tena hawakuweza kugundua tatizo hivyo wakatuhamishia tena Muhimbili, ikumbukwe kipindi chote hicho tiba yakutolewa maji tumboni ilikuwa ikiendelea, baadae alishindwa kabisa kula na kunywa mpaka umauti ulipomkuta, Mungu amlaze mahala pema peponi kaka yangu.

Wakuu kitu kilichonisukuma leo hii kuwahabarisha nikwamba nimepokea taarifa nyingine rafiki yangu wa utotoni nae amefariki kwa tatizo sawa na Hilo la kaka yangu na mwendendo wa kuugua kwake unashabihiana kabisa, ingawaje sisi tunaishi Dar es Salaam yeye alikuwa anaishi Moshi. Wasiwasi wangu ni kwamba kama huu ugonjwa sio mpya basi hauna tiba.

Shukrani za dhati ziwafikie Madaktari na wauguzi wote wa Muhimbili na TMJ kwa ushirikiano na msaada waliotupa.
 
Pole sana Mkuu, binafsi nadhani ni pepo ambalo kwa upande wangu lingewezekana kushindwa kwa njia ya maombi.

Nami niliwahi kuugua magonjwa ya kifua, kichwa kuuma na kizunguzungu kwa wakati mmoja.

Mungu aliniponya kwa uwezo wake kupitia maombi ya mara kwa mara hasa hasa saa 8 usiku, kufunga na kwa imani ilinichukua miaka miwili hatimaye nilipona kabisa.

Hakuna kinachoshindikana mbele zake Mungu ukimwamini.
 
Pole sana mwana Pangani mwenzangu nahisi huyu ni yule Dereva wa TBC hali hii huwatokea watu wanaokaa sana hasa madereva wa safari ndefu huwakuta sana hii ujue gari inabwetesha sana usipokua makini ndipo hupata matatizo km haya.
 
Pole sana Mkuu, binafsi nadhani ni pepo ambalo kwa upande wangu lingewezekana kushindwa kwa njia ya maombi.

Nami niliwahi kuugua magonjwa ya kifua, kichwa kuuma na kizunguzungu kwa wakati mmoja.

Mungu aliniponya kwa uwezo wake kupitia maombi ya mara kwa mara hasa hasa saa 8 usiku, kufunga na kwa imani ilinichukua miaka miwili hatimaye nilipona kabisa.

Hakuna kinachoshindikana mbele zake Mungu ukimwamini.
Asante sana mkuu,
Naamini Imani inaponya.
 
Huu ugonjwa unaitwa ascites

Tumbo likija maji hapo lazima upumuaji uwe na shida

Ova
Asante sana mkuu,
Na alifariki pembeni akiwa na mtungi wa gesi, lakini mbona Madaktar walishindwa kutambua huo ugonjwa!? Na awali walimwanzishia dozi ya TB, haikusaidia.
 
Salaam!

Wakuu nipo nyumbani wilayani Pangani mkoani Tanga namalizia msiba wa kaka yangu wadamu aliefariki katika hospitali ya taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu ikishirikiana na hospitali ya TMJ ya Mikocheni zote za Dar es Salaam.

Tatizo hasa lilikuwa Tumbo kujaa maji, kushindwa kula,kutapika na kwikwi isiyokoma, na kwabahati sana licha ya kufanyiwa kila aina ya vipimo ugonjwa anaougua haukuweza kugundulika,katika kipindi cha takriban miezi minne alichougua alianza kwa kulazwa katika hospital ya taifa Muhimbili Kisha wakamuhamishia TMJ.

Ili afanyiwe vipimo ambavyo Muhimbili hawana pamoja na kutolewa maji tumboni ambayo hujaa tena, kulikuwa na utaratibu wa kumtoa maji tumboni, kila siku ya alhamisi alitolewa maji drip mbili au tatu, alionekana kama kupata nafuu na tukatolewa tukamuuguze nyumbani.

Lakini maendeleo yake yalikuwa ya kusuasua mara apate nafuu mara azidiwe na hali ilipokuwa mbaya zaidi tulimrejesha tena TMJ ambapo alilazwa tena kwa uchunguzi zaidi na kwa mara nyingine tena hawakuweza kugundua tatizo hivyo wakatuhamishia tena Muhimbili, ikumbukwe kipindi chote hicho tiba yakutolewa maji tumboni ilikuwa ikiendelea, baadae alishindwa kabisa kula na kunywa mpaka umauti ulipomkuta, Mungu amlaze mahala pema peponi kaka yangu.

Wakuu kitu kilichonisukuma leo hii kuwahabarisha nikwamba nimepokea taarifa nyingine rafiki yangu wa utotoni nae amefariki kwa tatizo sawa na Hilo la kaka yangu na mwendendo wa kuugua kwake unashabihiana kabisa, ingawaje sisi tunaishi Dar es Salaam yeye alikuwa anaishi Moshi. Wasiwasi wangu ni kwamba kama huu ugonjwa sio mpya basi hauna tiba.

Shukrani za dhati ziwafikie Madaktari na wauguzi wote wa Muhimbili na TMJ kwa ushirikiano na msaada waliotupa.
Poleni sana.
Mi naona kama hawakuweza kusema tatizo watakua na upungufu mkubwa wa ujuzi. Hospitali kama muhimbili sina shaka kuweza wao kujua tatizo sema wanaweza kuona ni tatizo hawana uwezo kutibu. Kwa mfano zipo cancer aina mbalimbali za tumboni kama kwenye wengu, ini, uzazi au tumbo lenyewe husababisha kujaa maji.
Yafaa kueleza hali halisi ya ugonjwa kwa jamaa zake.
 
Pole sana mwana Pangani mwenzangu nahisi huyu ni yule Dereva wa TBC hali hii huwatokea watu wanaokaa sana hasa madereva wa safari ndefu huwakuta sana hii ujue gari inabwetesha sana usipokua makini ndipo hupata matatizo km haya.
Asante sana mkuu.
Ndie yeye, ni kaka yangu kabisa, basi aliipenda kazi yake lakini kazi haikumpenda yeye!
 
Asante sana mkuu.
Kazi ya Mungu haina upinzani!
Pole sana mkuu wangu.

Kaka alifikia umri wa miaka 80 na zaidi? Kama ni chini ya hapo basi tumlilie Mungu asituchukue kabla ya umri wetu aliotupangia.

Kuna wakati wanadamu tunapaswa kumkumbusha Munvu ahadi yake ili tusikamatwe na mitego ya ibilisi.

Pole sana kwa msiba ndugu yangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom