Ugonjwa wa Alzheimer

Kitia

JF-Expert Member
Dec 2, 2006
418
74
Napenda kuuliza kama kuna mtu yeyote anayefahamu jina la ugonjwa wa Alzheimer kwa kiswahili. Natanguliza shukrani.
 
Mkuu, swali zuri sana hata mie ningependa kufahamu ila nina wasiwasi kama huu ugonjwa una jina la kiswahili!
 
Mkuu, swali zuri sana hata mie ningependa kufahamu ila nina wasiwasi kama huu ugonjwa una jina la kiswahili!

Usemalo ni kweli. Huu ni ugonjwa ambao umeanza kuwa diagnosed siku hizi za karibuni. Mara nyingi huwapata watu kuanzia miaka 65. Itokeapo hivyo watu huchukulia kuwa ni dalili za uzee, kusahau n.k. Ugonjwa ukiendelea mgonjwa huanza kuchanganyikiwa, kusahau matukio, watu n.k. Natumaini mpaka sasa wengi tunafikiria kuwa mzee amechanganyikiwa, au amekuwa kichaa, ila ni athari za huu ugonjwa. Ingawa ugonjwa huo haujapata tiba bado, kuna dawa za kupunguza makali na kuusimamisha mahali ulipofikia usiendelee. Ugonjwa usipodhibitiwa, husababisha kifo. Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo.

Kuna haja ya kuifahamisha jamii kuhusu ugonjwa huo na athari zake, namna ya kuudhibiti na namna ya kutoa malezi kwa wagonjwa. Vile vile kuna haja ya kuangalia jinsi sheria inavyoweza kumlinda mgonjwa maana imetokea mara nyingi mgonjwa kutapeliwa mali zake kutokana na hali hiyo ya kuchanganyikiwa.
 
Kitia umesema"Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo."
Kwa hiyo utakuwa una uzoefu mkubwa -unaweza kutusaidia jinsi ulivyowasaidia hao wazee wako na jinsi ulivyousimamisha usiendelee bila dawa kama ulivyosema?Asante.
 
Kitia umesema"Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo."
Kwa hiyo utakuwa una uzoefu mkubwa -unaweza kutusaidia jinsi ulivyowasaidia hao wazee wako na jinsi ulivyousimamisha usiendelee bila dawa kama ulivyosema?Asante.

Kwa bahati mbaya, mzee mmoja alipoanza kuugua, tulijua kuwa amechanganyikiwa kwa ajili ya uzee. Hali iliendelea hivyo hivyo na kwa bahati mbaya akafariki. Kwa sababu hapakuwa na diagnosis ya kutosha, wala autopsy, hatukuweza kujua kwa uhakika kuwa ni kitu gani kilichomuua. Ilikuwa ni rahisi zaidi kuona dalili hizo kwa mzee wetu wa pili. Tulimleta kututembelea huku ughaibuni, ndio tukagundua kuwa tabia yake imebadilika kabisa, anasahau sana, na mara nyingi matamshi yake hayaleti maana. Hapo ndipo tukampeleka hospitali, akafanyiwa medical check up, psychiatric analysis na pia kufanyiwa MRI scan ya ubongo. Vipimo vilionyesha kuwa tayari ameshambuliwa na huo ugonjwa wa alzheimer. Daktari alitueleza hakuna dawa za ku reverse effects za ugonjwa huo, ila kuna dawa amabazo zinaweza kufanya ugonjwa huo usiendelee zaidi. Kwa mfano, hataacha kusahau, lakini rate ya kusahau itabakia palepale, badala ya kuendelea. Mojawapo ya dawa hizo ni Vitamin E (IDO-E9) pamoja na Arisept, au Doneratio, dawa ambazo mpaka sasa anatumia. Hata hivyo, dawa hizo, hasa hizi mbili za mwisho hazipatikani Tanzania, na imebidi tuwe tunatuma kila mara. Hizo anatakiwa kunywa maisha.

Care ya mgonjwa wa alzheimer ni ngumu sana kwa mgonjwa, na wewe unayetoa huduma. Kisaikolojia ita ku affect sana ukiona mzazi wako amebadilika amekuwa na hali hiyo. Mara nyingi atakuudhi kwa maneno yake, na inahitaji uvumilivu na upole katika kutoa huduma. Vilevile kuna haja ya kumpatia mgonjwa mental exercises ili aweza kutumia ubongo. Michezo kama karata, bao nk husaidia. Vile vile inabidi kumpa majukumu ya kufanya kutokana na uwezo wake.

Kutokana na kwamba ugonjwa huu umeanza kuonekana kwetu, kuna haja ya kuelimisha umma kuhusu athari zake. Vilevile kuipa sekta ya afya uwezo wa ku diagnose na kutoa matibabu, ambayo inabidi kupata dawa hizo kwa bei nafuu. Kama nilivyosema awali, kuna haja ya kuangalia jinsi sheria itakavyowalinda watu waliathirika na ugonjwa huu.
 
Usemalo ni kweli. Huu ni ugonjwa ambao umeanza kuwa diagnosed siku hizi za karibuni. Mara nyingi huwapata watu kuanzia miaka 65. Itokeapo hivyo watu huchukulia kuwa ni dalili za uzee, kusahau n.k. Ugonjwa ukiendelea mgonjwa huanza kuchanganyikiwa, kusahau matukio, watu n.k. Natumaini mpaka sasa wengi tunafikiria kuwa mzee amechanganyikiwa, au amekuwa kichaa, ila ni athari za huu ugonjwa. Ingawa ugonjwa huo haujapata tiba bado, kuna dawa za kupunguza makali na kuusimamisha mahali ulipofikia usiendelee. Ugonjwa usipodhibitiwa, husababisha kifo. Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo.

Kuna haja ya kuifahamisha jamii kuhusu ugonjwa huo na athari zake, namna ya kuudhibiti na namna ya kutoa malezi kwa wagonjwa. Vile vile kuna haja ya kuangalia jinsi sheria inavyoweza kumlinda mgonjwa maana imetokea mara nyingi mgonjwa kutapeliwa mali zake kutokana na hali hiyo ya kuchanganyikiwa.

Hivi ni wewe uliyeuliza jina la ugonjwa huu kwa kiswahili?nilikuwa najaribu kuangalia kamusi ya magonjwa ghafla nikaona maelezo yako yanaelekea kutoa jibu nikahisi labda ulikuwa unatoa kitendawili sasa naona unasubiri mji.
 
Hivi ni wewe uliyeuliza jina la ugonjwa huu kwa kiswahili?nilikuwa najaribu kuangalia kamusi ya magonjwa ghafla nikaona maelezo yako yanaelekea kutoa jibu nikahisi labda ulikuwa unatoa kitendawili sasa naona unasubiri mji.

Asante mkuu. Sisubiri mji hata kidogo. Natafuta mchango wa jumuia kutaka kujua zaidi kuhusu ugonjwa huu katika jamii yetu. Naomba nisieleweke kivingine.
 
Usemalo ni kweli. Huu ni ugonjwa ambao umeanza kuwa diagnosed siku hizi za karibuni. Mara nyingi huwapata watu kuanzia miaka 65. Itokeapo hivyo watu huchukulia kuwa ni dalili za uzee, kusahau n.k. Ugonjwa ukiendelea mgonjwa huanza kuchanganyikiwa, kusahau matukio, watu n.k. Natumaini mpaka sasa wengi tunafikiria kuwa mzee amechanganyikiwa, au amekuwa kichaa, ila ni athari za huu ugonjwa. Ingawa ugonjwa huo haujapata tiba bado, kuna dawa za kupunguza makali na kuusimamisha mahali ulipofikia usiendelee. Ugonjwa usipodhibitiwa, husababisha kifo. Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo.

Kuna haja ya kuifahamisha jamii kuhusu ugonjwa huo na athari zake, namna ya kuudhibiti na namna ya kutoa malezi kwa wagonjwa. Vile vile kuna haja ya kuangalia jinsi sheria inavyoweza kumlinda mgonjwa maana imetokea mara nyingi mgonjwa kutapeliwa mali zake kutokana na hali hiyo ya kuchanganyikiwa.

Ni kweli ugonjwa wa Alzheimer unahusishwa sana na umri mkubwa kwa sababu hutokea zaidi kwa watu wazima/wazee. Kwa ufupi husababishwa na aina fulani ya protini (amyloid beta) ambayo huunganika pamoja na kusababisha seli za ubongo kutofanya kazi ipasavyo. Dalili zake ni kama ulizozitaja. Wataalamu wa afya (madaktari) wanaweza kutuelezea kwa undani zaidi. Kwa Tanzania inawezekana ukawa umeanza kuwa diagnosed au kufanyiwa utafiti katika siku za karibuni ila kwa nchi kama USA utafiti ulianza zamani. Alzhemier ni mojawapo kati ya magonjwa yanayo waathiri wamarekani kwa wingi.
 
BONDIA,muhamed ali, si anao ugonjwa huu,au nimechanganya,yeye wanasema kaupata sababu ya kupigwa mangumi
 
Asante SANA Kitia-bora mtu ukala chako mapema kabla ya age hiyo. Maana umenikumbusha nilipokuwa age 7,kazi yangu ilikuwa ni kushughulika na babu yangu,ambaye kwa unavyozungumza naona kwa zaidi ya 75% alikuwa na ugonjwa huo,maana nilikuwa namwambia twende kula,yeye anazungumzia mambo ya benki au mke wake anamuuliza unanijua anasema ndio wewe si Mr.so and so,wao. looh uliponimaliza nguvu sasa ni hizo dawa kuwa hazipatikani uswahilini,yaaani hapo ndio watu kwa kuepuka kifo wanajivua uzalendo kwenda kuishi sehemu ambayo ikinifika hali hiyo angalau nipate kidonge.
 
Back
Top Bottom