Mkuu, swali zuri sana hata mie ningependa kufahamu ila nina wasiwasi kama huu ugonjwa una jina la kiswahili!
Kitia umesema"Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo."
Kwa hiyo utakuwa una uzoefu mkubwa -unaweza kutusaidia jinsi ulivyowasaidia hao wazee wako na jinsi ulivyousimamisha usiendelee bila dawa kama ulivyosema?Asante.
Usemalo ni kweli. Huu ni ugonjwa ambao umeanza kuwa diagnosed siku hizi za karibuni. Mara nyingi huwapata watu kuanzia miaka 65. Itokeapo hivyo watu huchukulia kuwa ni dalili za uzee, kusahau n.k. Ugonjwa ukiendelea mgonjwa huanza kuchanganyikiwa, kusahau matukio, watu n.k. Natumaini mpaka sasa wengi tunafikiria kuwa mzee amechanganyikiwa, au amekuwa kichaa, ila ni athari za huu ugonjwa. Ingawa ugonjwa huo haujapata tiba bado, kuna dawa za kupunguza makali na kuusimamisha mahali ulipofikia usiendelee. Ugonjwa usipodhibitiwa, husababisha kifo. Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo.
Kuna haja ya kuifahamisha jamii kuhusu ugonjwa huo na athari zake, namna ya kuudhibiti na namna ya kutoa malezi kwa wagonjwa. Vile vile kuna haja ya kuangalia jinsi sheria inavyoweza kumlinda mgonjwa maana imetokea mara nyingi mgonjwa kutapeliwa mali zake kutokana na hali hiyo ya kuchanganyikiwa.
Hivi ni wewe uliyeuliza jina la ugonjwa huu kwa kiswahili?nilikuwa najaribu kuangalia kamusi ya magonjwa ghafla nikaona maelezo yako yanaelekea kutoa jibu nikahisi labda ulikuwa unatoa kitendawili sasa naona unasubiri mji.
Usemalo ni kweli. Huu ni ugonjwa ambao umeanza kuwa diagnosed siku hizi za karibuni. Mara nyingi huwapata watu kuanzia miaka 65. Itokeapo hivyo watu huchukulia kuwa ni dalili za uzee, kusahau n.k. Ugonjwa ukiendelea mgonjwa huanza kuchanganyikiwa, kusahau matukio, watu n.k. Natumaini mpaka sasa wengi tunafikiria kuwa mzee amechanganyikiwa, au amekuwa kichaa, ila ni athari za huu ugonjwa. Ingawa ugonjwa huo haujapata tiba bado, kuna dawa za kupunguza makali na kuusimamisha mahali ulipofikia usiendelee. Ugonjwa usipodhibitiwa, husababisha kifo. Mpaka sasa familia yangu imeathirika na wazee wawili, na nafahamu familia zingine tatu ambazo wazee wao wamekumbwa na ugonjwa huo.
Kuna haja ya kuifahamisha jamii kuhusu ugonjwa huo na athari zake, namna ya kuudhibiti na namna ya kutoa malezi kwa wagonjwa. Vile vile kuna haja ya kuangalia jinsi sheria inavyoweza kumlinda mgonjwa maana imetokea mara nyingi mgonjwa kutapeliwa mali zake kutokana na hali hiyo ya kuchanganyikiwa.
BONDIA,muhamed ali, si anao ugonjwa huu,au nimechanganya,yeye wanasema kaupata sababu ya kupigwa mangumi