KotelaMamba
JF-Expert Member
- Apr 8, 2020
- 640
- 1,011
Wakuu, nimesema mke au mchepuko wa jirani kwasababu sina uhakika kama ni mke wake ama vipi.
Sisi tunaishi eneo moja tulivu sana, eneo moja wapo huku Bunju.
Tunakaribia Miaka Miwili tokea tuhamie.
Tuna jirani yetu, amehamia hana hata Mwezi so hatufahamiani zaidi ya kuonana njiani hasa nyakati za Asubuhi.
Jamaa huwa anampeleka mtoto wake kupanda school bus 🚌, huyo mtoto anaweza kuwa class Four au Three.
Ni kijana mpole sana, kwa mwonekano.
Kutoka kwenye Nyumba yake hadi kwetu ni kama mita 10-15.
Na nafikiri kwenye hiyo nyumba anaishi na huyo mtoto tu, au sijui kwasababu nimewahi kuwaona wao tu na ni asubuhi tu, Tunaokaa Nje ya mji tunaamka mapema sana kukimbizana na foleni, na tunarudi mida imeenda.
Sasa juzi kumetokea varangati ambalo limeleta mtafaruku.
Mida ya Saa Sita kasoro hivi usiku, tulianza kusikia kelele za Mwanamke kama vile anadai kitu, kutokea kwa jirani yetu huyo, zilianza chini chini hivi na baadae zikapanda.
Niliweza kusikia maneno machache na Jamaa akawa anaongea kwa hasira na kwa nguvu.
Wakaanza kutukanana, tusi kubwa ni kuitana Malaya, Jamaa anamwambia huyo Mwanamke wewe ni Malaya tu, yeye anamjibu Malaya ni wewe na baba yako, na maneno mengine mengine wakati huo kama vile kuna kitu wanagombania, inawezekana ni funguo.
Huyo Mwanamke anasisitiza jamaa ampe, mwamba kakaza, sasa sijui alikuwa amemshika kwasababu purukushani zilikuwa kubwa, Jamaa anamwambia atampasua, anamjibu huwezi kunifanya kitu ma.l.aya mkubwa wewe!!.
Hapo wife wangu yuko Dirishani anawasikiliza, mimi niko Kitandani sikutaka kuamka kabisa, gafla yule Mwanamke akapiga yowe moja la juu kabisa, kwa nyumba zilivyo sisi ndio tuko nao karibu kuliko nyumba za majirani wengine. Mabishano yao yalikuwa yamedumu kama dakika 15 hivi
Baada ya lile yowe la mwisho, nikasikia mkurumo wa gari, Wife akaniambia huyo jamaa anaondoka amka ukamzuie au ujue amemfanyia nini huyo Mwanamke, nikashtuka kidogo! Ile natafakari kwenye ile nyumba taa za ndani zikazimwa.
Wife akaniambia kuna mtu, huko ndani ila Kelele za yule Mwanamke na Jamaa hazikusikika tena. Wakati wote huo wife alikuwa anatamani niende nikaamulie huo ugomvi ambao sijui lolote.
Sasa gafla naona wife anachukua mto wake (pillow) anasema anaenda kulala chumba kingine, simply kwasababu nilishindwa kutoka na kuanza kunilaumu kwa mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu, ananiambia sina msaada wowote ule.
Wakuu kosa langu hapo ni lipi?
Unawezaje kuingilia ugomvi ambao hujui ulikotokea?
Naambiwa nina roho mbaya, kisa sikwenda na mimi dirishani kujaribu kuangalia kinachoendelea.
Ndoa ina miaka 6 hii ila bado sijamfahamu vizuri huyu wife wangu...Nahisi ana vichembe chembe vya u feminist.
Sisi tunaishi eneo moja tulivu sana, eneo moja wapo huku Bunju.
Tunakaribia Miaka Miwili tokea tuhamie.
Tuna jirani yetu, amehamia hana hata Mwezi so hatufahamiani zaidi ya kuonana njiani hasa nyakati za Asubuhi.
Jamaa huwa anampeleka mtoto wake kupanda school bus 🚌, huyo mtoto anaweza kuwa class Four au Three.
Ni kijana mpole sana, kwa mwonekano.
Kutoka kwenye Nyumba yake hadi kwetu ni kama mita 10-15.
Na nafikiri kwenye hiyo nyumba anaishi na huyo mtoto tu, au sijui kwasababu nimewahi kuwaona wao tu na ni asubuhi tu, Tunaokaa Nje ya mji tunaamka mapema sana kukimbizana na foleni, na tunarudi mida imeenda.
Sasa juzi kumetokea varangati ambalo limeleta mtafaruku.
Mida ya Saa Sita kasoro hivi usiku, tulianza kusikia kelele za Mwanamke kama vile anadai kitu, kutokea kwa jirani yetu huyo, zilianza chini chini hivi na baadae zikapanda.
Niliweza kusikia maneno machache na Jamaa akawa anaongea kwa hasira na kwa nguvu.
Wakaanza kutukanana, tusi kubwa ni kuitana Malaya, Jamaa anamwambia huyo Mwanamke wewe ni Malaya tu, yeye anamjibu Malaya ni wewe na baba yako, na maneno mengine mengine wakati huo kama vile kuna kitu wanagombania, inawezekana ni funguo.
Huyo Mwanamke anasisitiza jamaa ampe, mwamba kakaza, sasa sijui alikuwa amemshika kwasababu purukushani zilikuwa kubwa, Jamaa anamwambia atampasua, anamjibu huwezi kunifanya kitu ma.l.aya mkubwa wewe!!.
Hapo wife wangu yuko Dirishani anawasikiliza, mimi niko Kitandani sikutaka kuamka kabisa, gafla yule Mwanamke akapiga yowe moja la juu kabisa, kwa nyumba zilivyo sisi ndio tuko nao karibu kuliko nyumba za majirani wengine. Mabishano yao yalikuwa yamedumu kama dakika 15 hivi
Baada ya lile yowe la mwisho, nikasikia mkurumo wa gari, Wife akaniambia huyo jamaa anaondoka amka ukamzuie au ujue amemfanyia nini huyo Mwanamke, nikashtuka kidogo! Ile natafakari kwenye ile nyumba taa za ndani zikazimwa.
Wife akaniambia kuna mtu, huko ndani ila Kelele za yule Mwanamke na Jamaa hazikusikika tena. Wakati wote huo wife alikuwa anatamani niende nikaamulie huo ugomvi ambao sijui lolote.
Sasa gafla naona wife anachukua mto wake (pillow) anasema anaenda kulala chumba kingine, simply kwasababu nilishindwa kutoka na kuanza kunilaumu kwa mambo yasiyokuwa na kichwa wala miguu, ananiambia sina msaada wowote ule.
Wakuu kosa langu hapo ni lipi?
Unawezaje kuingilia ugomvi ambao hujui ulikotokea?
Naambiwa nina roho mbaya, kisa sikwenda na mimi dirishani kujaribu kuangalia kinachoendelea.
Ndoa ina miaka 6 hii ila bado sijamfahamu vizuri huyu wife wangu...Nahisi ana vichembe chembe vya u feminist.