Ugawaji wa vitalu: Wazawa wanavyotumika kupotosha ukweli kwa maslahi ya wachache

Patriote

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
1,718
1,047
Suala la ugawaji wa vitalu vya uwindaji wa kitalii limekuwa likiisumbua serikali kwa miaka mingi sana na kufanya viongozi wetu mara kadhaa kutoana povu pale suala hili linapojadiliwa. Sio kwamba ugawaji wa vitalu kwa wawekezaji unatumia technolojia ya hali ya juu sana, la hasha, ukiingia kwenye undani wa suala hili utagundua kuwa kinachowafanya viongozi wetu kutoana povu ni kutaka wao/familia zao/jamaa zao wapate mgao wa vitalu hivi. Hili hasa ndilo tatizo la msingi ktk suala zima la ugawaji wa Vitalu. Ipo orodha ndefu ya vigogo, ndugu, jamaa na marafiki wa vigogo wa nchi hii waliomilikishwa maeneo ya mahoteli na au vitalu vya uwindaji wa kitalii ktk hifadhi zetu.

Kichefuchefu kilichopo katika upendeleo huu ni kwamba vigogo/ndugu/jamaa hao wanapopewa hayo maeneo kwa upendeleo wengi wao wanakuwa hawafwati sheria zilizopo kwa vile wanajua kuna anayewalinda na kuwakingia kifua, watu hawa hawana uwezo wa fedha wala utaalam, uzoefu, wala nyenzo za kufanya shughuli za utalii hivyo huishia kuuza/kukodisha maeneo hayo kwa wawekezaji wa kigeni kinyume na sheria/utaratibu. Hili ndilo hasa chimbuko lingine la ugomvi kati ya wawekezaji wa kigeni na serikali.

Serikali inatumia mgongo wa kujifanya inataka wazawa wamilikishwe Vitalu vya uwindaji wa kitalii kumbe kimsingi inalenga kuwanyang'anya wawekezaji wa kigeni waliokuwa wanamiliki maeneo hayo toka awali ili kuwapa "wazawa" ambao kimsingi ni vigogo wenyewe/watoto wao/ndugu, jamaa na marafiki zao tena wasio na sifa za kuendesha biashara hiyo. Hali hii inapelekea Serikali kupoteza mapato mengi sana. Kama kweli Serikali inapenda wazawa wamiliki rasilimali zao, Mbona Reginald Mengi hakupewa Kilimanjaro Hotel instead akapewa Muarabu wa Suti???Kama serikali inapenda wazawa, kwa nini wachimba madini wadogowadogo wanatimuliwa maeneo ya migodini???

Ugomvi huu sasa umevuka mipaka na kuingia kwenye anga za kimataifa ambapo Shirikisho la Kimataifa la Wawindaji ('Safari Club International-SCI) limeamua kuanika hadharani mvutano uliopo kati ya serikali na baadhi ya kampuni za uwindaji za kigeni huku likionya watalii wanaoingia nchini.Shirikisho hilo la Convention' ambalo huandaa maonyesho ya kimataifa ya kampuni za uwindaji kila mwaka, kupitia jarida lake la 'Hunting Report' toleo la Oktoba na Novemba mwaka huu, linaeleza kuwa kutokana na kuwepo mgogoro wa ugawaji vitalu nchini hivi sasa mazingira ya uwindaji sio mazuri. Tamko hilo au tahadhari hii inaweza ikapelekea kupungua kwa pato la Taifa linalotokana na Uwindaji wa kitalii.

HITIMISHO: Ndugu zangu suala la ugawaji vitalu na maeneo ya ujenzi wa mahoteli ndani ya hifadhi zetu kwa ujumla wake limegubikwa na utata unaosababishwa na ufisadi, uchu/ulafi wa viongozi wetu pamoja na upendeleo kwa ndugu, jamaa na marafiki zao. Ndugu zangu tusidanganywe kuwa Serikali inapenda sana wananchi wake na ndio maana imeamua kutoa vitalu hivyo wa wazawa, wazawa wanaoongelewa hapa kwa asilimia kubwa ni walewale wanaotuibia rasilimali zetu. Je katika hali hiii nini kifanyike?? Mana PCCB ndo hivyo kazi yake kubwa ni kusafisha na kutetea ufisadi!!!!???

Nashauri ili serikali ipate pato la kutosha na iondokane na lawama zisizokuwa na msingi, vitalu vigawiwe kwa mnada wa wazi kuliko huu utaratibu wa kugawa vitalu kwa kwa kujifungia na kwa kujuana. kwa kufanya hivi lawama, kujuana na ufisadi vitakuwa havina nafasi.


 
Inaelekea unakaa sana nje ya nchi mpaka unajisahau

hujijui ulipo na unapokwenda

kwani inamaana hujui kama uozo ulipo leo ulisababishwa na yule jamaa ambaye maiti yake ilivimba na kupasuka uwanja wa taifa?

kawaleoa hawa watu tulionae leo halafu na wewe unaleta ngonjera
 
calmdowner you are sick to your stomach....

haijalishi jamaa anakaa wapi but there is a genuine concern mkuu.... many of these things spiraled out of control vitalu vilipoanza kugawiwa chini ya uangalizi wa rais mmojawapo na akagawa hadi nchi kabisaa
 
Bora wapewe hao hao Watanzania siyo kila kitu wapewe wageni. Tuanze na uwindaji kisha kwenye madini. Hao wageni si wakawinde kwao. Wakipewa wanaondoka na wanyama wetu wakiwa hai. Ndolanga aliwahi kusema wanyama ni wetu na sisi ndio tunawawinda. Kila kitu wageni wageni wageni aaaah! Hata kuwinda tu wageni, wacha wazawa wapewe na wageni wakija wapate toka kwa wazawa uchumi ubaki ndani.
 
Industry ya uwindaji ni very complex. Viongozi wengi wanaitolea macho. Ndo maana Ole Sendeka na kundi lake, wakiongozwa na Ndugai na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya ardhi maliasili na mazingira wanataka kumng`oa Waziri maige kwa sababu mambo yameenda kinyume na walivyotarajia. Hawa jamaa walijitungia sheria eti 75% ya vitalu wapewe wazawa na wageni wasipate zaidi ya 25% wakati wakijua 98% ya biashara hiyo imekua ikifanywa na wageni. Wao wanataka wapate vitalu halafu wawakodishe wageni kwa gharama za juu. Yaani watengeneze mamilion kwa kujaza makaratasi tu. Uzawa kwa nini kwenye vitalu tuuu. Bahati nzuri, wanasiasa machachari wamekosa
 
Inaelekea unakaa sana nje ya nchi mpaka unajisahau hujijui ulipo na unapokwenda

kwani inamaana hujui kama uozo ulipo leo ulisababishwa na yule jamaa ambaye maiti yake ilivimba na kupasuka uwanja wa taifa?

kawaleoa hawa watu tulionae leo halafu na wewe unaleta ngonjera
Vipi kiongozi mbona unaongea mengi, yasiyokuwepo na hata ya siyoeleweka?????hili jiwe limekupiga nini???samahan ckujua kama nalenga mtu mimi nimetupa tu jiwe gizani.Hoja yangu inataka ueleza nini kifanyike kurescue hii situation, hatuwezi kuendelea kuishi kwa kuangalia historia ya nani kalea au anaendekeza uozo. Msiotaka kuendekeza haya ndo wasaa wenu sasa mtoe ushauri wa nini kifanyike na sio tuanze kuvamiana mwilini badala ya kuivamia hoja.
 
Bora wapewe hao hao Watanzania siyo kila kitu wapewe wageni. Tuanze na uwindaji kisha kwenye madini. Hao wageni si wakawinde kwao. Wakipewa wanaondoka na wanyama wetu wakiwa hai. Ndolanga aliwahi kusema wanyama ni wetu na sisi ndio tunawawinda. Kila kitu wageni wageni wageni aaaah! Hata kuwinda tu wageni, wacha wazawa wapewe na wageni wakija wapate toka kwa wazawa uchumi ubaki ndani.
Nakubaliana na wewe kwenye hili suala la vitalu kumilikishwa wazawa, kinachosikitisha katika mpango huo, ni kuwakatalia wazawa wenye sifa na uwezo na kuwapa wasio na sifa wala uwezo ambao ni ndugu/jamaa na marafiki wa walio madarakani. Kama kweli lengo la nchi yetu ni kumuinua mzawa wa kawaida Mbona KIA hakupewa mzawa/wazawa kwa pango la $1000 tu kwa mwaka???kama waliona mzawa hana uwezo wa kuendesha KIA kwa gharama ya $1000 kwa mwaka (yaani $ 83.3 kwa mwezi) na wakaamua kumpa mwekezaj wa nje. Iweje leo wanaona mzawa huyo ana uwezo wa kuendesha biashara ya Uwindaji inayohitaji mamilion ya fedha katika uwekezaji wake????

Kinachofanyika kwenye ugawaji wa vitalu hakina tofauti sana na kilichofanyika kwenye mradi wa kuzalisha umeme KIWIRA, RICHMOND !!!Kama ya KIWIRA, RICHMOND tuliyaita ufisadi na uvunjifu wa maadili ya uongozi, basi kwenye vitalu ni zaidi ya yaliyotokea KIWIRA, RICHMOND. Sababu wengi wa wanaopewa vitalu kwa style hii ya kujuana hawana hata uwezo wa kulipia ada ya hivyo vitalu kwa mwaka. Wanasubiri wakabidhiwe vitalu ili wawauzie wawekezaji wa kigeni kuviendesha mana wao hawajui lolote na wala hawana uwezo wa kuendesha hiyo biashara, Sifa kubwa walionayo ni mtoto wa kiongozi, kaka ya kiongz, ukoo na kiongoz etc.

Sikubaliani na move ya kumpa mzawa-kiongozi/ndugu/jamaa ya kiongoz rasilimali zetu kwa kulighalimu pato la taifa kama ilivyotokea Kiwira.
 
Na vitalu vinavyoongoza kwa poaching ni hivi vya "wazawa". Wanatumia power in the excuse of "wazawa kwanza" kujifaidisha wao na si taifa.
Bora wewe umeliona hili, sio tu poaching kuwa juu, hawachangii maendeleo ya jamii zinazozunguka vitalu vyao wala kuboresha miundombinu km barabara etc as required by the law. Watu wasiofwatilia mambo wakiona hoja ya mzawa imewekwa mezani, wanadhan inawalenga wao, kumbe mzawa anayeongelewa hapa sio mzawa wa kawaida bali ni mzawa wa kikundi kile kile cha wafilisi mashirika yetu na mali za umma.
 
Bora wapewe hao hao Watanzania siyo kila kitu wapewe wageni. Tuanze na uwindaji kisha kwenye madini. Hao wageni si wakawinde kwao. Wakipewa wanaondoka na wanyama wetu wakiwa hai. Ndolanga aliwahi kusema wanyama ni wetu na sisi ndio tunawawinda. Kila kitu wageni wageni wageni aaaah! Hata kuwinda tu wageni, wacha wazawa wapewe na wageni wakija wapate toka kwa wazawa uchumi ubaki ndani.

Wazawa hawatakiwi kuwinda kwani wanyama watakwisha; ila wazungu wakiwinda wanyama hawaishi!! Zaidi ya hayo wazawa wakiwinda serikali yetu inwaita majangili!!
 
Wazawa hawatakiwi kuwinda kwani wanyama watakwisha; ila wazungu wakiwinda wanyama hawaishi!! Zaidi ya hayo wazawa wakiwinda serikali yetu inwaita majangili!!

Naenda kuomba kitalu na.mimi niwinde simba, vifaru na tembo.
Mbuga hizi wakabidhiwe wazawa yaani ziwe chini ya Halmashauri za Wilaya ziliko. Hivi mnafahamu kuwa mbuga ya Maasai mara huku Kenya ipo chini ya Narok Count Council na serikali kuu haitii mkono wake hata kidogo na ni mbuga ambayo ni maarufu sana (ni sehemu ya serengeti) na inaingiza kipato kikubwa. Mambo ya mbuga ipo Loliondo vitalu vinauziwa Keko ndio matokeo yake hayo.
 
Wandugu

Natafuta document juu ya Vitalu vya Uwindaji. Taarifa hiyo iliwahi kuwekwa hapa jukwaani lakini nimejaribu kutafuta sijafanikiwa. Mwenye nacho tafadhali tupia humu nami nifaidike.

Asanteni
 
Mkuu labda funguka zaidi, unatafuta taarifa ipi na kwa lengo gani ? Maana akina Maguluchemba pia wanatafuta sana taarifa hizi ili kuzichakachua, mambo ya loliondo yamewashika pabaya sana siajabu ndo maana siku hizi Vasco Dagama anapiga misele wilaya za DSM kukagua, maana kwingine hawataki kabisa kusikia blah blah na mauza uza ya uchumi kukua na nchi ya amani na mshikamano !!

Wandugu

Natafuta document juu ya Vitalu vya Uwindaji. Taarifa hiyo iliwahi kuwekwa hapa jukwaani lakini nimejaribu kutafuta sijafanikiwa. Mwenye nacho tafadhali tupia humu nami nifaidike.

Asanteni
 
Wandugu

Natafuta document juu ya Vitalu vya Uwindaji. Taarifa hiyo iliwahi kuwekwa hapa jukwaani lakini nimejaribu kutafuta sijafanikiwa. Mwenye nacho tafadhali tupia humu nami nifaidike.

Asanteni
Mkuu Ork, ni taarifa ipi unatafuta maana yawezekana kuna taarifa nyingi za vitalu vya uwindaji. Kwa mfano taarifa ya utekelezajia ya serikali ambayo kwa hakika inakuwa na mapungufu (si ya kweli) na ile ya wadau wanaoandika ukweli kuhusu wizi na ufisadi katika vitalu vya uwindaji. Ila mzee wa nyara za serikali lazima atakuwa nazo zote!!!
 
Natafuta juu ya idadi ya Vitalu, mmiliki, wapi ilipo na probably registration number ya kampuni
 
Back
Top Bottom