Zito Kabwe amemtoa nje Waziri Chami aliyeongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Kukuza Mauzo nje (EPZ), Dk. Adelhelm Meru, na watendaji wa mamlaka hiyo kwa madai ya ufisadi wa sh bilioni 41 katika mradi wa Benjamin Mkapa ulioko Mabibo, jijini Dar es Salaam.
Dk. Chami na watendaji hao walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya mjumbe wa Kamati ya POAC kuhitaji ufafanuzi wa matumizi ya fedha katika mradi huo kwa kutofautiana na ripoti ya ukaguzi uliofanywa na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).
mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya (CCM), alisema kutokana na hali hiyo kamati inahitaji kupata maelezo ya kina kwani inaonyesha kuna matumizi yaliyofanywa na kuzidi gharama za ujenzi wa mradi huo ambazo ni sh bilioni 14 kama ilivyopangwa na serikali.
Kwa mujibu wa taarifa za CAG, kuna matumizi ya zaidi ya sh bilioni 41.
Tunahitaji ufafanuzi juu ya mradi huu sasa; inanyesha hata kuna malipo yalifanyika katika ununuzi wa vifaa hakunyesha stakabadhi za malipo, sasa hali hii inajenga shaka, kwa kuwa mwenyekiti wa baraza ambaye pia ni Waziri wa Viwanda unaweza kutupatia majibu ya kina kuhusu hili, alisema Bulaya.
Hata hivyo majibu hayo yalipingwa na mwenyekiti wa kamati hiyo alimtaka Waziri Chami na watendaji wake kutoka EPZ kuondoka kikaoni na mara watakapopata nyaraka hizo waje tena mbele ya kamati hiyo na kutoa maelezo yao ya kina.
Lengo letu ni kujenga kwa hili katika mradi huu wa Benjamin Mkapa, kuna kitu ambacho hakileti tafsiri nzuri kwenu hivyo tunawataka muondoke na pindi mtakapopata nyaraka hizo muhimu ndipo mje mbele ya kamati.
Lakini sasa inaoyesha kuna malipo yalikuwa yakifanywa bila hata kufuata utaratibu hadi kufikia sh bilioni 41; tunapata shaka na matumizi ya fedha za serikali kuchezewa na wajanja wachache, alisema Zitto.
Kutokana na maamuzi hayo wajumbe wa kamati hiyo waliunga mkono hatua hiyo hali iliyomlazimu Waziri Chami na timu yake kunyanyuka na kutoka nje ya ukumbi huo.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya EPZ, inaonyesha kuwa toka mradi huo ulipoanzishwa watendaji hao wa EPZ wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kufuja fedha za umma ikiwemo kujilipa mishahara mikubwa na hata kufanya matumizi ya ununuzi wa vifaa kinyume cha sheria.
Kamati pia imeomba ufafanuzi kuhusu matumizi makubwa ya fedha yaliyofanya na Mkurugenzi mkuu wa EPZA Adelhmer Mero Katika maandalizi ya warsha ya maonyesho ya EPZA Yaliyofanyika mwezi uliopita i
Dk. Chami na watendaji hao walijikuta kwenye wakati mgumu baada ya mjumbe wa Kamati ya POAC kuhitaji ufafanuzi wa matumizi ya fedha katika mradi huo kwa kutofautiana na ripoti ya ukaguzi uliofanywa na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG).
mbunge wa Viti Maalum, Esther Bulaya (CCM), alisema kutokana na hali hiyo kamati inahitaji kupata maelezo ya kina kwani inaonyesha kuna matumizi yaliyofanywa na kuzidi gharama za ujenzi wa mradi huo ambazo ni sh bilioni 14 kama ilivyopangwa na serikali.
Kwa mujibu wa taarifa za CAG, kuna matumizi ya zaidi ya sh bilioni 41.
Tunahitaji ufafanuzi juu ya mradi huu sasa; inanyesha hata kuna malipo yalifanyika katika ununuzi wa vifaa hakunyesha stakabadhi za malipo, sasa hali hii inajenga shaka, kwa kuwa mwenyekiti wa baraza ambaye pia ni Waziri wa Viwanda unaweza kutupatia majibu ya kina kuhusu hili, alisema Bulaya.
Hata hivyo majibu hayo yalipingwa na mwenyekiti wa kamati hiyo alimtaka Waziri Chami na watendaji wake kutoka EPZ kuondoka kikaoni na mara watakapopata nyaraka hizo waje tena mbele ya kamati hiyo na kutoa maelezo yao ya kina.
Lengo letu ni kujenga kwa hili katika mradi huu wa Benjamin Mkapa, kuna kitu ambacho hakileti tafsiri nzuri kwenu hivyo tunawataka muondoke na pindi mtakapopata nyaraka hizo muhimu ndipo mje mbele ya kamati.
Lakini sasa inaoyesha kuna malipo yalikuwa yakifanywa bila hata kufuata utaratibu hadi kufikia sh bilioni 41; tunapata shaka na matumizi ya fedha za serikali kuchezewa na wajanja wachache, alisema Zitto.
Kutokana na maamuzi hayo wajumbe wa kamati hiyo waliunga mkono hatua hiyo hali iliyomlazimu Waziri Chami na timu yake kunyanyuka na kutoka nje ya ukumbi huo.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari kutoka ndani ya EPZ, inaonyesha kuwa toka mradi huo ulipoanzishwa watendaji hao wa EPZ wamekuwa wakilalamikiwa kutokana na kufuja fedha za umma ikiwemo kujilipa mishahara mikubwa na hata kufanya matumizi ya ununuzi wa vifaa kinyume cha sheria.
Kamati pia imeomba ufafanuzi kuhusu matumizi makubwa ya fedha yaliyofanya na Mkurugenzi mkuu wa EPZA Adelhmer Mero Katika maandalizi ya warsha ya maonyesho ya EPZA Yaliyofanyika mwezi uliopita i