Uelewa wa mambo kwa watanzania ni mdogo sana, Ujinga na upumbavu unaongezeka kila mwaka

tujadili content tuache kuleta mambo ya CDM na CCM wakati tunaona kabisa jamii ina tatizo..
 
Yanayoendelea kwa vijana wetu Wasomi na ambao sio Wasomi huwezi kutofautisha kitu Katika kundi hili. Hoja za matusi na kutukana ndio njia pekee ya hawa vijana, Wanaamini upande mmoja wa habari

Yawezekana ni makosa yetu wazazi kuwajaza watu ujinga na wao kuyaamini kama yalivyo bila kufikiria au kujiridhisha

Mambo yafuatayo yameonyesha aina ya watu na vijana tulionao hapa JF :

Mosi, Hoja za kuendeleza gesi na maamuzi ya kutafuta wanasheria wa nje kwa ushauri, Vijana wamejazwa upepo kuwa wao wanaweza kazi hii ya sheria za kimataifa kwa kusoma soma sheria za International law pale Udsm na Udom, Wamekaa wanakula popcorn hawaelewi kuwa serikali inalipa madeni mengi kwa kudharau sheria za kimataifa, Ushauri wa kipuuzi wa wanasheria wa ndani kuwa tunaweza serikali imeishia kulipa hasara na medeni

Pili, Hoja za Bandari ya Bagamoyo, Wengi wamejazwa upepo bandari haifai,Wachina wanatupiga. Ukiwauliza wewe unafahamu mkataba wake anajibu nilimsikia Rais na Waziri. Leo hii mtu anaweza sema tutaajiri vijana 100,000 serikalini na vijana wanapiga makofi, Ukiuliza ajira zitatoka wapi kwa pesa ipi hakuna majibu, Mtu haelewi hata maana ya kina cha bandari bali utasikia aaha kule Bagamoyo si kwa Mzee JK ndio maana wanajenga bandari, Ukimuuliza sasa ulitaka JK azaliwe Dodoma

Tatu, Hoja za Freeman Mbowe na kesi inayoendelea huko mahakamani, Utasikia Leo shahidi amegalagazwa vibaya sana, Tangu lini shahidi akagalagazwa? Shahidi anaeleza alichokiona Yeye na kukishuhudia, Maswali anayoulizwa nje ya yale aliyoyasema na kuyaandika hayamuhusu,Jaji anajenga msingi kwa alichokisema shahidi, Maswali ya kuwa una degree ngapi? Una wake wangapi? Unamfahamu Tundu Lisu? Uliona watu wakibeba petrol na magogo?. Haya yote inategemea kama shahidi aliyasema kama hakuyasema ni kupoteza muda kumuuliza, Maswali nje ya context ya alichokisema na kukiandika shahidi ndio vijana wanashabikia huku wakiwa na Tecno na itel za wachina wasiowataka kujenga bandari ya Bagamoyo

Hoja ya Ridhwani Kikwete kuwa naibu Waziri, Utasikia aaha yule Ridhwani hafai kabisa, Ukiuliza lini Ridhwani amewahi kuwa Waziri na akakosea hakuna Jibu lolote, Lipi baya alilofanya Ridhwani utasikia aahaa nchi sasa imerudishwa kwa wapigaji, amepiga pesa gani hakuna majibu, Kumbe wanaumia kwanini mtoto wa fulani kawa Waziri, Kwanini uumie mtoto wa Mo Dewji kuwa tajiri kama Baba yake ulitaka avae kandambili zilizoshonwa shonwa

Hoja za Spika Ndugai kujiudhuru na chama chake cha ccm, Utasikia Spika ameonewa na Rais ana nguvu zaidi. Je unafahamu taratibu za ndani za ccm kanuni na maadili ambayo chama kilimpendekeza Ndugai kuwa Spika, Utasikia sifahamu, Ndani ya ccm mtu anawajibika kwa chama chake kwanza halafu ndio anawajibika kwenye nafasi yako uliyopewa, Hata Rais Samia anawajibika kwenye chama kwanza halafu kama Rais, Chama ndio kimekupa nguvu na sio cheo, Ndugai alivunja maadili na kanuni za chama kilichompendekeza awe Spika kwa kushindwa kujizuia kutofautisha nafasi akiwa Bungeni na nje ya Bunge

Vijana ambao wanategemea akili za watu wengine wawafikirie kwa niaba yao, Hao ni vijana mfu
Mkuu itoshe tu kusema unamawazo mgando na yakizamani sana

Jambo lolote lile lina uzuri wake na kasoro zake na kila mtu ana UHURU wa kuchagua upande kwa mujibu wa maoni na dhamira yake

Sasa wewe ni nani wa kuwapangia watu upande wa kuchagua?
Kwamba watu wanaochagua maoni tofauti na yako ndio wajinga na wapumbavu na hajui kutumia elimu zao?
Kwamba wewe ndio Msaafu au Bibilia au Katiba unaotoa muongozo kipi ni sahihi kuchagua na kipi sio sahihi?

Inaonekana bado mchanga sana kwenye haya mambo mkuu
Tofauti zetu ndio maendeleo yetu mkuu
Dunia hii tungekuwa wote tunawaza sawa sawa sijui ingekuwaje

Jifunze kuheshimu maoni ya wenzako pale mnapotofautiana na uyapinge kwa HOJA badala ya kuwatusi kejeli na dharau
 
Hujatoa suruhu ya hayo mambo yote,
kama umeona tatizo kipo bas tusaidiane namna ya kuleta utatuzi na watu wajitambue waweze kutoka kwenye hayo mazonge.
 
siku hizi jf kunazidi kujaa watu wa hovyohovyo yani mtu anakuwa na akili mgando kiasi ambacho unashanga kama huyu ni mtu alopita vidudu ama la.

Nianze tu na wale watu wa kupandikizana chuki dhidi ya mtu flani, kundi flani ama taasisi flan, Watanzania tuache hiyo mihemko ya kubeba chuki ndani ya mioyo yetu kisa flani kasema simpendi flani na nampenda flani unakuta mtanzania anachuki haswaa na tasisi flani ukimuuliza wamekufanyajee utasikia oooh sijui ilikuwa hivi mara vilee. kiufupi usimkumbatie adui wa mwenzako na kutembea nae,

Mtoa mada ka sijakuelewa kuhusu issue ya Bwagamoyo!
issue ya bwagamoyo binafsi sijawahi ielewa hata na sitokaa nielewe, sioni sababu ya kujenga bandari bwagamoyo wakati mtwara na tanga kuna bandari nzuri zenye kina kizuri tuu na hata kama tukizitengeneza hazita gharimu fedha nyingi kama kwenda kuchima huko bwagamoyo. Bandari ya Dar inagharama nyingi kutokana na utoaji wa mchanga wa mara kwa mara pili mji ushakuwa huu tunahitaji kukuza miji mingine.
binafsi napendekeza kama wanamalengo mazuri fedha za Bwagamoyo wazihamishie mtwara ambako kunabandari nzuri yenye kina kirefu kisichihitaji kuchimbwa tena pia itafanya mkoa wa mtwara kuinuka kiuchumi, ikumbukwe sina maslahi na Mtwara

tatizo lilipo bandari ya Dar es salaam la Sand deposit ndio tatizo linaloikuta Mtwara na Tanga... Bandari zote hizo zina mlango wa kuingilia meli sio an OPEN SEA matokeo yake ni Sand deposit za mara kwa mara na kizuizi kwa Mega Ships + Super tankers..

Bagamoyo ilichaguliwa na wawekezaji wenyewe baada ya research yao kwa bandari zote hizo, Bagamoyo ikaonekana ina kina kizuri, Open sea, na hakuna sand deposit, lakini pia kuna eneo kubwa lipo tupu tayari kwa ujenzi....(issue hapo ibaki kwenye mikataba tu)
 
tatizo lilipo bandari ya Dar es salaam la Sand deposit ndio tatizo linaloikuta Mtwara na Tanga... Bandari zote hizo zina mlango wa kuingilia meli sio an OPEN SEA matokeo yake ni Sand deposit za mara kwa mara na kizuizi kwa Mega Ships + Super tankers..

Bagamoyo ilichaguliwa na wawekezaji wenyewe baada ya research yao kwa bandari zote hizo, Bagamoyo ikaonekana ina kina kizuri, Open sea, na hakuna sand deposit, lakini pia kuna eneo kubwa lipo tupu tayari kwa ujenzi....(issue hapo ibaki kwenye mikataba tu)
kama kweli ile kauli aliyozungumza mkuu aliyetangulia ni kweli basi hatuna haja ya kuwa na mikataba ya namna hiyo,
Pia wawekezaji wasitupangie sana maana tunakimbia foleni nao wanataka turudisha huko pia
 
Uzi wa kipumbavu kabisa. Mawazo yake ndio anataka yawe mawazo ya watu wote. Watu tumetofautiana kwenye kila kitu na ndio demokrasia hiyo....
Demokrasia ni pamoja na kutofautiana kwa facts sio kupinga tu eti democrasia ,
 
Tupe mkataba ambao ni wanserikali na uliwekwa wazi,tuanzie na mkataba wa SGR na JNHP
Ndio maana Tz mlijitoa kwenye nchi wa uendeshaji wa serikali Kwa uwazi (Open Government partnership,OGP) chini ya mwendazake!
Ndio mwendelezo wa upigaji tu!Mikataba kufanywa Siri!


 
Demokrasia ni pamoja na kutofautiana kwa facts sio kupinga tu eti democrasia ,
Shida kubwa ni mentality
Unazijua FACT Kwenye opinion?
Je unajua muktadha wa “kupinga” na kukosoa?

Tatizo huwa lipo hapa
Kiuna watu wanadhani wao ndio wana hodhi FACT ni nini
Na pia wana hodhi tafsida ya dhana jengefu kwamba ukiwaza tofauti basi UNAPINGA na kwakuwa wanadhani wana hodhi FACT basi unacho hoji kwa kukosoa unakua MPUMBAVU sababu ya kukutafsria FacT wanavyotaka wao

Wataamua jambo ukikosoa watakutusi huna FACT, baada ya muda upepo ukigoma wanabatilisha kwa tafsiri zao zao za FACT ...... imetokea mara nyingi sana

Kwani kuna matatizo gani watu kuhoji kitu au kuonyesha njia mbadala?
 
Mkuu pole Sana,ndio umegundua leo?

Ukishakuwa na jamii ambayo haina exposure, maskini,walalamishi na kulaumu na kukosoa kila jambo tegemea Hali hiyo..

Watu hawataki kutumia akili ila shortcut,kubebwa,kulelewa,miujiza na uganga usitegemee chochote cha maana a hapo zaidi ya wivu na majungu..
 
Kwenye bandari hapo vijana wengi wa bongo ni giza nene.
Utaskia Nchi imeuzwa,hata kwenye mikopo watu wanaelezwa kwamba Tzn ni himilivu Ili kuchochea maendeleo haraka lazima tukope tufanye kwa haraka tena tunakopa mikopo soft loan lakini daa ujinga umejaa kama pipa kichwani..

Uchumi hayajua kila kitu hawajui lakini Domo Domo kubwa ,ni shida tupu mara Nchi itauzwa na upuuzi mwingine.

Screenshot_20220102-191011.png
 
Hii ndio akili ya kuja kumtetea riziwani? Hivi mna account ngapi humu?
 
Mtindue Tena na tena
Mkuu hongera kwa kujaza madukuduku yako na kuyaleta katika hali ya kubeza walio kinyume na matamanio yako.

N ahapa ni sawa na kusema kwa kejeli kuwa unakuta mtu ni msomi au sio msomi analalamika hali ya hewa ya joto kali, wakati hajui mabadiliko ya tabia nchi. Ni sawa na kusema mtu analalamika mimea kuweka dawa wakati hajawahi kulima! Ulichokifanya ni kuweka mambo mengi kwa pamoja yanayokukera katika mfumo wa kubeza, lakini sioni kama una jipya kwenye bandiko lako. Inshort huna suluhisho lolote kwa uliyoyasema zaidi ya kuyaweka katika hali ya ujuaji.
 
Kuna wakati kujiona mjanja ndio huwa Ujinga wenyewe....

Mikataba ya hii nchi siku zote huwa haipo wazi,, Vijana wakitaka iwe wazi unaita wapuuzi,,..Walio na mikataba wakiweka wazi na Vijana wakahoji kutokana na waliypambiwa bado mnawaita wajinga kwa kuwahoji kuwa wana ukweli gani na wanachokisema na ukizingati nyie wenyewe ndio mliowapa hizo taarifa....

Kiukweli nchi ni ngumu sana na kwa maelezo yako inaonekana huamini uwezo wako binafsi na hio attitude umeipeleka kwa Vijana wenzako ukiamini wapo kama wewe....
 
Niliwahi kusema ukoo huu wa akina makamba sio watu wa kuaminiwa kabisa. Kumbukeni mzee makamba na mienendo yake akiwa katibu wa chama na RC Dsm, mtoto vilevile alipokuwa mazingira!
 
Back
Top Bottom