Mwanaharakati na Msomi maarufu nchini ameandika katika ukurasa wake wa mtandao:
Tarehe 11.09.2023) niliangalia na kusikiliza kwa makini, huzuni, mshangao na masikitiko makubwa sana Marudio ya Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan akifungua Baraza Maalum la Vyama vya Siasa.
2) Kuna siku ntapenda niandike Makala ya Maoni yangu kuhusu Hotuba hii. Insha Allah, Mungu Akipenda!
a) Mwenye text ya Hotuba hii naomba anitumie.
b) Leo ntaongea kidogo na kwa kifupi tu. Lakini naomba izingatiwe kwamba natoa Maoni yangu kwa Nia Njema kabisa, kwa Unyenyekevu mkubwa, Heshima na Taadhima.
c) Kwenye hiyo Makala ntakayoandika siku nyingine ndiyo ntaongea kwa kirefu kuhusu Mapungufu ya Hotuba hii ambayo ilitawaliwa na Matusi na kujichanganya. Mfano: Rais Samia kaona ni sawa kabisa kuwaita Bin Adam wenzie "Ng'ombe," "Mijitu," n.k.
d) Kwenye Utangulizi wa Makala hiyo ntaorodhesha Matusi yote aliyotumia Rais Samia kuwatukana Wapinzani wake wa kisiasa, Wananchi wenye Maoni tofauti (na kujidhalilisha).
3) Body Language!
a) Sijui Rais Samia alimuona Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Joseph Sinde Warioba alivyojikunyata huku akiwa amepigwa na butwaa?!
b) Sijui Samia alimuona Mpiga Debe wake, Mzee Stephen Wasira alivyojichekesha na kutaka kupiga Makofi, halafu akaangalia kulia kwake na kugundua wenzie wote wamemkaushia Rais... nae akasinyaa!
c) Sijui Samia alimuona Makamu wake, Kanali Mstaafu Mzee Abdulrahman Kinana ambaye alitumia mbinu ya kuhakikisha ameshika kijinotibuku mkono wa kushoto ambacho ndicho alitumia kama kisingizio chake cha kutompigia Makofi Bosi wake?!
d) Sijui Rais Samia aliyachukuliaje haya?! Au alijiona Mshindi tu?!
4) Rais Samia:
a) Kafoka huku akiwa amekasirika sana, tena sana. (Sina uhakika hasira zake zimesababishwa na nini?! Sijui ameishasahau kwamba aliwahi kutuahidi Wadanganyika kwamba yeye si Mtu wa kufokafoka na hatafokafoka...?!)
b) Kafoka sana kwa "gia" ya kuhubiri Maadili! Bahati mbaya, kapotea stepu kwa kutumia Hotuba yake nzima kutukana anaodai wamemtukana! (Sijui ni nani hao?!)
c) Kajisahau kwamba yeye ni Rais, na hivyo kuna Maneno hayastahili kutoka kinywani mwake, tena kinywa kilekile anacholia chakula na kumliwaza Mwenzi wake...! (Nimeazima Maneno ya Samia mwenyewe...!)
d) Kajisahau kwamba, kimsingi, katukana Watanzania wote (pamoja na wale marafiki zake Wazungu/Mabalozi waliokuwa Ukumbini wakimshangaa)!
e) Kajichanganya sana katika kila alilosema kuhusu Katiba. Rais Samia amethibitisha kwamba kumbe, labda, alikuwa Mwongo katika yote aliyofanya na kutamka huko nyuma kuhusu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
f) Anakumbuka Ombi na Ahadi yake kwetu Wadanganyikaaa?! "Naomba mnipe muda kidogo niweke Uchumi vizuri kwanza...!" Tukumbuke yeye ndiye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba kabla ya RC Paul Makonda kumpigia debe apewe Umakamu wa Rais! (Ingawa hakusema hivyo moja kwa moja, mimi BJC nilimsikia Rais Samia kama vile anaibeza Katiba yetu, Biblia na Quran Tukufu, kwa pamoja, mmhuuu...!)
g) Kachafua Hali ya Hewa kwa yote aliyosema (au kushindwa kusema) kuhusu Katiba Mpya na kuhusu DP World (i.e. ule Mkataba wa Hovyo wa Bandari).
5) Ushauri wa Bure!
a) Kama ambavyo Wasaidizi wa Rais (yeyote yule Duniani) hawatakiwi kumruhusu Rais wao ahutubie Taifa akiwa amelewa, Washauri wa Rais Samia hawatakiwi kumruhusu Rais Samia aongee na Wananchi akiwa amekasirika kupita kiasi.
b) Rais Samia ana zile 4R zake ambazo anadai ndio Msingi wa Urais wake (na ambazo, namhakikishia, hakuna Mwananchi anazielewa)! Namshauri Samia aongeze na 2H: "Hasira Hasara"!
c) Rais Samia atafute muda, Kichwa chake kikiwa kimetulia kabisa, aiangalie tena Hotuba yake na akijisikilize kwa makini.
d) Rais Samia ajiulize: Kwa nini hata "Chawa wake" walionekana kama kutatizika vile na kutojua wampigie Makofi kwa lipi?!
e) Kiapo cha Urais kiongezwe Maneno: "...naapa pia kuilinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isichezewe na/au kubezwa kwa namna yoyote ile na Mtu yeyote yule." (Wanasheria wanaweza kutusaidia kuiweka vizuri zaidi au kutuelimisha iwapo Maneno haya tayari yamo, by implication, kwenye Kiapo hikihiki cha sana!)
6) Swali la Kizushi!
a) Je, Rais Samia anapendekeza Watanzania wa Umri gani hawastahili kuangalia/kusikiliza Hotuba yake hii?!
b) Je, anaweza kukubaliana na mimi kwamba Hotuba kama hizi hazistahili kabisa kurushwa na/au kuonyeshwa na TBC (na Stesheni zingine za Runinga na Radio) kabla Watoto hawajalala (maana ni kinyume na Maadili)?!
7) Ngoja nitabasamu kidogo...!
8) Naamini Rais Samia anafahamu vizuri Matumizi ya Tahadhari kwenye Runinga (TV Content Warnings), na hasa DSTV:
a) S - Sex
b) N - Nudity
c) V - Violence
d) L - Language
e) PG - Parental Guidance
9) Naongelea Maadili yanayozingatiwa na hata hao Wazungu "waliopotea Njia" kwenye Mambo mengi.
10) Hakika Hotuba ya Rais kutawaliwa na Matusi na Mipasho:
a) Ni Ukosefu wa Maadili Kitaifa.
b) Si Malezi Bora.
c) Si Uongozi Bora.
11) Ingekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaruhusiwa kuomba radhi, ningemshauri Rais Samia awaombe radhi bila Masharti:
a) Watanzania wote.
b) Wapinzani wote.
c) Washiriki wote wa Mkutano aliouhutubia na kuufungua kwa Matusi, huku akitoa Amri badala ya Hoja!
12) Aidha, Rais Samia asisahau kuwaomba radhi Watoto na Vijana wote ambao, kuna Uwezekano mkubwa, baadhi yao wameathirika kwa ile Shock ya kumsikia Rais wao anatukana!
a) Watoto/Vijana hawa wanaweza kuwa wamepata "Psychological Trauma." Wataalam na Madaktari Bingwa watuongoze!
b) Rais ahakikishe Watoto/Vijana wetu hawa wanapimwa na kupatiwa Matibabu na/au Ushauri Nasaha.
13 That's how serious the whole mess is!
Tarehe 11.09.2023) niliangalia na kusikiliza kwa makini, huzuni, mshangao na masikitiko makubwa sana Marudio ya Hotuba ya Rais Samia Suluhu Hassan akifungua Baraza Maalum la Vyama vya Siasa.
2) Kuna siku ntapenda niandike Makala ya Maoni yangu kuhusu Hotuba hii. Insha Allah, Mungu Akipenda!
a) Mwenye text ya Hotuba hii naomba anitumie.
b) Leo ntaongea kidogo na kwa kifupi tu. Lakini naomba izingatiwe kwamba natoa Maoni yangu kwa Nia Njema kabisa, kwa Unyenyekevu mkubwa, Heshima na Taadhima.
c) Kwenye hiyo Makala ntakayoandika siku nyingine ndiyo ntaongea kwa kirefu kuhusu Mapungufu ya Hotuba hii ambayo ilitawaliwa na Matusi na kujichanganya. Mfano: Rais Samia kaona ni sawa kabisa kuwaita Bin Adam wenzie "Ng'ombe," "Mijitu," n.k.
d) Kwenye Utangulizi wa Makala hiyo ntaorodhesha Matusi yote aliyotumia Rais Samia kuwatukana Wapinzani wake wa kisiasa, Wananchi wenye Maoni tofauti (na kujidhalilisha).
3) Body Language!
a) Sijui Rais Samia alimuona Waziri Mkuu Mstaafu, Mzee Joseph Sinde Warioba alivyojikunyata huku akiwa amepigwa na butwaa?!
b) Sijui Samia alimuona Mpiga Debe wake, Mzee Stephen Wasira alivyojichekesha na kutaka kupiga Makofi, halafu akaangalia kulia kwake na kugundua wenzie wote wamemkaushia Rais... nae akasinyaa!
c) Sijui Samia alimuona Makamu wake, Kanali Mstaafu Mzee Abdulrahman Kinana ambaye alitumia mbinu ya kuhakikisha ameshika kijinotibuku mkono wa kushoto ambacho ndicho alitumia kama kisingizio chake cha kutompigia Makofi Bosi wake?!
d) Sijui Rais Samia aliyachukuliaje haya?! Au alijiona Mshindi tu?!
4) Rais Samia:
a) Kafoka huku akiwa amekasirika sana, tena sana. (Sina uhakika hasira zake zimesababishwa na nini?! Sijui ameishasahau kwamba aliwahi kutuahidi Wadanganyika kwamba yeye si Mtu wa kufokafoka na hatafokafoka...?!)
b) Kafoka sana kwa "gia" ya kuhubiri Maadili! Bahati mbaya, kapotea stepu kwa kutumia Hotuba yake nzima kutukana anaodai wamemtukana! (Sijui ni nani hao?!)
c) Kajisahau kwamba yeye ni Rais, na hivyo kuna Maneno hayastahili kutoka kinywani mwake, tena kinywa kilekile anacholia chakula na kumliwaza Mwenzi wake...! (Nimeazima Maneno ya Samia mwenyewe...!)
d) Kajisahau kwamba, kimsingi, katukana Watanzania wote (pamoja na wale marafiki zake Wazungu/Mabalozi waliokuwa Ukumbini wakimshangaa)!
e) Kajichanganya sana katika kila alilosema kuhusu Katiba. Rais Samia amethibitisha kwamba kumbe, labda, alikuwa Mwongo katika yote aliyofanya na kutamka huko nyuma kuhusu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
f) Anakumbuka Ombi na Ahadi yake kwetu Wadanganyikaaa?! "Naomba mnipe muda kidogo niweke Uchumi vizuri kwanza...!" Tukumbuke yeye ndiye alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba kabla ya RC Paul Makonda kumpigia debe apewe Umakamu wa Rais! (Ingawa hakusema hivyo moja kwa moja, mimi BJC nilimsikia Rais Samia kama vile anaibeza Katiba yetu, Biblia na Quran Tukufu, kwa pamoja, mmhuuu...!)
g) Kachafua Hali ya Hewa kwa yote aliyosema (au kushindwa kusema) kuhusu Katiba Mpya na kuhusu DP World (i.e. ule Mkataba wa Hovyo wa Bandari).
5) Ushauri wa Bure!
a) Kama ambavyo Wasaidizi wa Rais (yeyote yule Duniani) hawatakiwi kumruhusu Rais wao ahutubie Taifa akiwa amelewa, Washauri wa Rais Samia hawatakiwi kumruhusu Rais Samia aongee na Wananchi akiwa amekasirika kupita kiasi.
b) Rais Samia ana zile 4R zake ambazo anadai ndio Msingi wa Urais wake (na ambazo, namhakikishia, hakuna Mwananchi anazielewa)! Namshauri Samia aongeze na 2H: "Hasira Hasara"!
c) Rais Samia atafute muda, Kichwa chake kikiwa kimetulia kabisa, aiangalie tena Hotuba yake na akijisikilize kwa makini.
d) Rais Samia ajiulize: Kwa nini hata "Chawa wake" walionekana kama kutatizika vile na kutojua wampigie Makofi kwa lipi?!
e) Kiapo cha Urais kiongezwe Maneno: "...naapa pia kuilinda Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania isichezewe na/au kubezwa kwa namna yoyote ile na Mtu yeyote yule." (Wanasheria wanaweza kutusaidia kuiweka vizuri zaidi au kutuelimisha iwapo Maneno haya tayari yamo, by implication, kwenye Kiapo hikihiki cha sana!)
6) Swali la Kizushi!
a) Je, Rais Samia anapendekeza Watanzania wa Umri gani hawastahili kuangalia/kusikiliza Hotuba yake hii?!
b) Je, anaweza kukubaliana na mimi kwamba Hotuba kama hizi hazistahili kabisa kurushwa na/au kuonyeshwa na TBC (na Stesheni zingine za Runinga na Radio) kabla Watoto hawajalala (maana ni kinyume na Maadili)?!
7) Ngoja nitabasamu kidogo...!
8) Naamini Rais Samia anafahamu vizuri Matumizi ya Tahadhari kwenye Runinga (TV Content Warnings), na hasa DSTV:
a) S - Sex
b) N - Nudity
c) V - Violence
d) L - Language
e) PG - Parental Guidance
9) Naongelea Maadili yanayozingatiwa na hata hao Wazungu "waliopotea Njia" kwenye Mambo mengi.
10) Hakika Hotuba ya Rais kutawaliwa na Matusi na Mipasho:
a) Ni Ukosefu wa Maadili Kitaifa.
b) Si Malezi Bora.
c) Si Uongozi Bora.
11) Ingekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anaruhusiwa kuomba radhi, ningemshauri Rais Samia awaombe radhi bila Masharti:
a) Watanzania wote.
b) Wapinzani wote.
c) Washiriki wote wa Mkutano aliouhutubia na kuufungua kwa Matusi, huku akitoa Amri badala ya Hoja!
12) Aidha, Rais Samia asisahau kuwaomba radhi Watoto na Vijana wote ambao, kuna Uwezekano mkubwa, baadhi yao wameathirika kwa ile Shock ya kumsikia Rais wao anatukana!
a) Watoto/Vijana hawa wanaweza kuwa wamepata "Psychological Trauma." Wataalam na Madaktari Bingwa watuongoze!
b) Rais ahakikishe Watoto/Vijana wetu hawa wanapimwa na kupatiwa Matibabu na/au Ushauri Nasaha.
13 That's how serious the whole mess is!