Uchambuzi umehalalishwa na ujumbe kufika au?

Kibunago

JF-Expert Member
Jan 11, 2008
300
122
Baada ya baadhi ya Wachambuzi wa JF kuanza kudadavua hapa siku ya kwanza wakieleza kuwa, ingawa ni Wakili wa kujitegemea, kuna utata wa Mh. Marando kumtetea Manji (aliyetuhumiwa na Mengi kuwa Fisadi Papa) wakati yeye Marando ‘atatakiwa kuonekana na jamii kutekeleza yale anayoyapigia kelele jukwaani’ likiwemo lile la kuwapinga na kupambana na Mafisadi kwa nguvu zote,

leo ni mara ya tatu nimegundua kuwa wakati kesi hiyo ya Manji Versus Mengi inaelezwa kupitia ITV NEWS, Jina la Marando sasa kama Wakili wa Manji halitajwi tena bali mwenzake ingawa katika picha unaweza kumwona Marando akiwa Mahakamani (ingawa inaweza kuwa ni kutoka Maktaba). Je,


  1. Marando kajitoa katika utetezi au
  2. Kuna katazo limetolewa asitajwe waziwazi kuwa ni (mmoja wa) (ma)Wakili kwa kudhani kuwa inachafua hali ya hewa? au
  3. Imetokea tu bahati kwamba Watangazaji sasa wanajikuta wanamtangaza Wakili mwenza bila kumtaja Marando kama siku ya kwanza?
 
Back
Top Bottom