Uchaguzi 2020 Uchaguzi ujao wa 2020 hakuna mbunge wala Diwani kutoka vyama vya upinzani watakaopenya

jigoku

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
2,411
733
Nimemsikia makamu Mwenyekiti wa CCM ndugu Philip Mangula juzi akiwa ktk ziara zake sambamba na katibu mkuu wa CCM ndugu Bashiru wakijigamba kwamba,uchaguzi ujao wa 2020 hakuna mbunge wala Diwani kutoka vyama vya upinzani watapenya,kwamba hawawezi kushinda hata jimbo na kata yoyote.

Kauli hii imekuwa ikisisitizwa sana na viongozi hawa akiwamo hata Polepole hasa pale wanapokuwa wanawapokea wabunge au madiwani wanaohama vyama vya upinzani,na kwa mantiki hiyo inaonekana ni moja ya silaha wanayoitumia kuwarubuni na kufikia bei hata kuhama.

Nimetafakari kwa muda sana kuhusu kauli hiyo ya hakuna mbunge wala diwani wa upinzani atakaepenya...nawaza je CCM hii inapendwa sana? Je CCM hii imetekeleza vema ilani yake? Je CCM hii inawajali wanyonge? Je CCM hii inawavutia watu kwa sababu ya Itikadi yake?.

Maswali hayo yakanifanya nirejee kitabu cha Makwaia wa Kuhenga,kiitwacho CCM NA MSTAKABALI WA NCHI YETU.

Nimekutana na kauli ya Mzee Mangula ya mwaka 2007 ktk uchaguzi wa chama,ilinukuliwa na mwandishi nami nainukuu,
"Tusipoangalia udiwani na Ubunge utakuwa unapigwa mnada au kufanyiwa tenda na hivyo uongozi kununuliwa na wenye fedha"

Hili tumeliona,sasa CCM inawanunua wapinzani kwa kuwahonga vyeo na pesa kujaribu kuhalalisha kupendwa kwao,tena mtoa kauli hiyo ndio anasimamia mauzo na tenda.

Lakini kitabu hicho,mwandishi amemnukuu Dr Bashiru,wakati akihojiana nae,nami namnukuu.

Chama cha siasa sio mkusanyiko wa majini dume yenye tamaa...Majini ambayo yametanguliza tamaa kufa na kupona,tamaa ya kutengeneza pesa au kupata vyeo kwa gharama yoyote"

Sasa Leo Bashiru huyo huyo ndio anayatafuta majini dume,amekuwa dalali wa majini dume yanayosaka madaraka au pesa ayajaze kwenye Chama chake kionekane kinakubalika pamoja na mwenyekiti wake ndugu John Magufuli.
Mwandishi pia ukurasa wa 21 amenukuu barua ya Mzee Butiku kwenda kwa mwenyekiti wa CCM wakati huo Mzee Mkapa...
Anasema,

CCM haitaweza kuepuka kuvunjika kutoka na dhambi ya kukiuka maadili,ahadi na kiapo chake chenyewe.CCM ambayo inaliacha Bunge lake kutunga sheria ya kuhalalisha rushwa na kuiita takrima......haiwezi kuepuka hukumu ya dhambi ya kuruhusu kupitishwa na kutumia sheria ambayo ina udhalimu ndani yake.

Leo CCM wanahonga pesa na vyeo kununua wabunge na madiwani ili kuaminisha watu CCM inapendwa sana,kuaminisha mwenyekiti wao Magufuli anapendwa sana.

Kwa mtiririko huo wameanza kuaminisha umma,wabunge na madiwani,na wale wanaotaka kugombea uchaguzi ujao kupitia vyama vya upinzani kwamba hakuna atakaepenya,hakuna atakaechaguliwa,kauli hii inarudiwa sana, ili iwaingie wananchi NA waiamini....

Najiuliza kwa kipi? Hivi Leo CCM ni Chama cha Itikadi gani? Ni ujamaa au ubepari?yaani Chama kimebaki tu kama genge LA wapiga fedha za umma.Nisaidieni CCM kinafuata itikadi gani?

Wamefeli kutekeleza ilani wenyewe,wanatumia ujinga wa wananchi kuwalaghai,walichosema kuhusu Mazingira na mabadiliko ya tabia nchi ibara 152(e) kupunguza bei ya gesi na majiko ili kuokoa misitu nalo wameshindwa.

Walisema wataendeleza mamlaka za serikali za mtaa nako wamefeli,maana badala ya kuhamasisha Halmashauri kubuni vyanzo vipya vya mapato ili zijiendeshe vema,wakazipora vyanzo vya mapato,walisema watazifanyia mapitio sheria ili kuharakisha ugatuaji wa madaraka nako wamefeli.

Ibara 145(a) kuhusu utawala bora,demokrasia na uwajibikaji hili kili mtu anajua wameshindwa vibaya.

Ibara ya 145(g) ya ilani yao walisema watakamilisha mchakato wa katiba mpya,matokeo yake Mwenyekiti wao na Raid Magufuli alikataa kwamba haikuwa kipaumbele chake.

Hali ya uchumi na maisha ya watu yalivyo kila MTU anasoma namba.

Sasa huo mkazo wa kusema wagombea wa upinzani hawatachaguliwa utajwa sana based on what???

Nilichokigundua ni kwamba...

Jeshini kina kitu kinaitwa TARGET DAMAGE CRITERIA.

Kuna criteria NNE
1: Annihilation, upigaji target kwa kina hii ni wa kuingamiza target isiweze tena kuhama,kuondoka(Maneuver) hapa kinachokuwa huwa ni target ya platoon(Platoon strong points) au eneo lililohifadhiwa mizinga na vifaa vyake.

2:Demolition: Uboamoaji/Kuharibu.
Upigaji wa target kwa kina hii kinachokuwa komekusudiwa ni kubomoa majengo,madaraja,au njia na kusababisha kutokutumika tena.

3:Neutralization: Ni upigaji wa target na kufanya isiweze ku-maneuver kwa muda.

4:Harassment: Upigaji huu wa target hukusudiwa kuleta usumbufu kwa target iliyokusudiwa,hii ndio hutumika kwa ajili ya kushusha morali wa wapiganaji, maana ni pigo LA kisaikolojia,hutumika kwa ajili ya demoralization kwa adui.

Katika mapambano moja ya jambo muhimu sana ni Morali wa wapiganaji, kwa hiyo kauli ya CCM kupitia kwa makamu mwenyekiti Mzee Mangula na katibu wao Bashiru wanajaribu kutumia hii Target Damage Criteria namba 4 ya Harassment fire ili kuweka psychological pressure kwa wabunge walioko upinzani,madiwani na wanaotaka kugombea uchaguzi ujao ili wawe demoralised (washuke morali) kisha wajisalimishe CCM.

Ukweli ni kwamba CCM wameshashindwa,tena kadri siku zinavyosonga ndio wanachukiwa sana na RAIA,Upinzani unazidi kuimarika hususan CHADEMA... Na Kuna baadhi ya uimara huo umejengwa na CCM.

Wasitetereke kwa wachache wanao hangaika na vyama kuvitumia kama daraja la kupata madarka au pesa.

Tuendelee kudai Tume huru, wenye kuathiriwa na harassment fire waende,RAIA tupate Tume huru ndio watajua CCM inapendwa au La

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hili bara Mungu ameshaliacha, wewe haujiulizi maendeleo yapo sehemu nyingine duniani? Hata hapa Africa sehemu zilizopiga hatua kama North Africa, and south Africa walioleta maendeleo sio watu weusi?

Tuko busy na mambo ya kipumbavu kabisa, wakati vijana hawana ajira, hamna mitaji, umasikini unaongezeka,Uhuru unapungua but the main concern ya watawala niku consolidate POWER!

Kuna bolt zimechomolewa kwenye kichwa cha MTU mweusi, ndio maana hawana mipango endelevu, for over 50 years matatizo yetu ni Yale yale over and over, more than 80% of people are living under poverty line! Hawana agenda za maendeleo, wabafanya miradi mikubwa kwa kukopa wala hawana mikakati ya kukuza uchumi. Wao ni kuongeza deni LA taifa mpaka lije litupasukie.

African leadership ni Shida sana...kwanini wazungu waendeleee kiasi hicho sisi tuwe masikini kwa kiwango hiki? Jiulizeni. Najua kuna watu watakuja na majibu mepesi kwamba hao wazungu wanatunyonya, kama wanawanyonya nchi ngapi wakati tunapata Uhuru na zenyewe zilikuwa zinapata Uhuru lakini zimetuzidi mbali sana kWa sasa?

Mbaya zaidi, wakitokea watu kuwa challenge hata tweeter tu wanawatafuta ili wawatoe roho! Kama sio laana ni nini? Wazungu na mapungufu yao they don't kill recklessly their own people, ndio maana hata Mungu anawabariki, kutwa Kucha unamwaga damu za watu wasiokuwa na hatia over useless things, huyu Mungu akubariki wa wapi? Na bado yalivyo empty-headed yanataka tuzidi kuzaliana!
 
Nimesoma mstari wa juu pekee.... Ila naomba niongee kitu sawa maendeleo hayana chama lakini ninachokiona kitakachotokea miaka ijayo nafikiri kama Taifa tunakwenda kuumia.....

Kama Bunge lina wabunge wa kijani zaidi ya 312 na Baadhi yao wanaingiza uvyama badala ya kujadili mustakabali wa Taifa bali ubishi tu.....

Mbunge Bwege (wanavyomuita au wanaomuita) nahisi ameliona na kuwaonya hao chama kijani kuwa wanakwenda kuliharibu hili Taifa

Mimi nafikiri kama Chama Kijani kina uhakika wa kushinda 100% ya wabunge wote, nafikiri busara itumike, fedha hizo kwàajili ya uchaguzi nahisi zitumike kwa maendeleo mengine tu nafikiri itapunguza hata deni la Taifa kuliko, kuitisha uchaguzi angali matokeo wanayo


NIMTAZAMO WANGU WA KIPUUZI TU MNISAMEHE

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Balvejmumt,
Kama shuleni mlikuwa mnafundishwa types of goverment mojawapo ni authoritarian government. Hiyo itaanza mwaka 2021. Hapo ndipo mtalia na kulimia meno kama alivyowahi kusema bwana yule
 
Kama shuleni mlikuwa mnafundishwa types of goverment mojawapo ni authoritarian government. Hiyo itaanza mwaka 2021. Hapo ndipo mtalia na kulimia meno kama alivyowahi kusema bwana yule
Mkuu uliwahi kwenda kwenye kikao halafu kumbe kilishakaliwa toka jana yake na walishatoa maamuzi Jana yake? Hivi wewe Leo hii unabadilije maamuzi yao kwa lipi labda.....

Kwasababu wameshatuona tunakaa kimya wameona wafanye wanachojisikia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Manelezu, Mawazo yako kama yangu, hakika Waafrika tumelaaniwa sana na Mwenyezi Mungu alisha tuacha zamani sana nahis kutokana na upumbavu wetu, kila nikiwaza naona sisi ngozi nyeusi ni laana tupu.

Miafrika tumekuwa wapumbavu kiasi cha kutoana roho tena kwa mambo ya kipuuzi ..Mungu alitupa rasilimali nyingi sana lakini hatuna hata akili ya kuzitumia. Hebu fikiria viongozi wanawaza matumbo yao tu..mipesa wanaenda kuficha kwa Wazungu huku kwetu wanatuachia vita na mauaji, hebu fikiria Yaifa kama Sudani Kusini, Tanzania, Uganda, Burundi nk.

Wazungu wanazidi kupiga hatua yaani mimi nahisi katika viumbe hai sisi ni toleo la mwisho baada ya Mungu kuumba wanadamu. Leo mtu anasimama anasema yule mpe umeme huyu usimpe maana ni chama fulani yule mpe maji yule usimpe.....inauma sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbinu iliyotumika kwenye uchaguzi wa serekali ya mitaa ndioitatumika kuwapitisha viongozi wa kuteuliwa kutoka CCM na kuwazuia wapinzani kupenya.
 
Naionea huruma Tanzania yangu juu ya kesho...kama kuna mtu anadhani kuwa Chama kimoja tu..ktakua na utengamano mbeleni..amejidanganya sana...kuna SERKALI nyingi cilishindwa katika hili...mfano..Cuba.na Venezuela .kweny siasa ubinafs ni pale unapoona wewe ndy unafaaa pekee yako...mfumo wa siasa wa Chama kimoja tu utaleta kutoelewana zaidi..!!mda utasema tu!!
Tengenezen Taifa lenye kujar kua uhuru wa kuamua mamlaka ya wananchi kuwa ni wananchi wenyewe,kupitia siasa Safi na uchaguz ulio huru na bora...!!
Mungu inua mioyo ya waliowanyonge na upofu juu ya kesho!na wape maono ya walionanguvu wajue hatar ya kesho ili watengeneze kesho nzur juu ya Taifa letu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kati ya uchaguzi wenye mtego wa hatari ni wa mwaka huu. Tusisahau kwamba kati ya observers ktk vituo ni: World Bank, European Union, USAID n.k a.k.a mabeberu.
Na njama za upinzani zaweza kuhusisha kususia uchaguzi kama matukio yatakuwa ya hatari. Hivyo Chama pendwa kisipige vigelegele maana baada ya uchaguzi twaweza kuingia mgogoro wa kiuchumi.
 
Yaani hii Nchi kunasiku itaongozwa na Chizi. Sasa kama kwa zaidi ya miaka 50 tunasumbuka na matatizo yale yale, bunge lisipokuwa na wapinzani ndio umasikini, ujinga, rushwa, ufisadi, maradhi, huduma mbaya za kijamii vitaondoka?.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni mwandishi mzuri sana haya nenda kamsaidie mbowe kuandika ilani ya chadema 2020!
Ilani ya uchaguzi haiandikwi na mtu mmoja,Chama chochote kikiandika ilani kutumia mtu mmoja hiyo sio ilani ya uchaguzi iliyowalenga wananchi.

Ilani ya uchaguzi inaandikwa na wananchi, Chama cha siasa kinatakiwa kufanya kitu kinaitwa Canvassing, lengo likiwa ni ku-identify issues zonazowahusu wananchi,baada ya hapo ndipo hupangwa na kuandikwa vizuri.
Nadhani umeelewa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya Wapinzani kudekekezwa sana Mzee Kikwete, sasa ni dhahiri bila mbeleko hawa watu hawawezi kupenya popote.

Ukiangalia wabunge wengi walioshinda Upinzani mwaka 2015 ni wale waliodhulumiwa CCM wakaamua kwenda upande wa pili kUchukua ubunge.

Kwasasa wote wamerejea nyumbani Upinzani wana hali mbaya hawaaminani wenyewe kwa wenyewe.

Wananchi wamewakataa wamebaki kusubiri mikutano ya Rais wetu mpendwa Magufuli wapate cha kutukana mitandaoni.

Wameishiwa kwisha kabisa. Huu mwaka wapinzani wakipata hata wabunge watano watambike. Target ya kwanza ni kuondoa wabunge wote wasaliti wa nchi bungeni.

Mwaka wa CCM kuvuna mazao bora

Ahsante Rais wetu mpendwa Magufuli kwa kuirejesha CCM kwenye makali yake.
 
upinzani usingekua na nguvu basi mwenyekiti wa CCM asingekua na hofu kuu aliyonayo. Anaujua ukweli, labda ni ninyi tu vichwa vya panzi wa lumumba ndio mnaishi kwenye dunia ya kufukirika.

Si mnamsikia 'graduate' mwenzenu wa lumumba ndugu bashite anavyoachia uharo kila akifungua domo lake? akili hamna.
 
Back
Top Bottom