Peter Mwaihola
JF-Expert Member
- Jun 23, 2022
- 227
- 333
Umewahi kusafiri umbali mrefu kwenye basi ukakaa na yule mtu kutoka mwanzo wa safari hadi mwisho kila chakula kinachopita dirishani kikiuzwa yeye husema nipe hicho, mpaka mnanafika ana rundo la vyakula anashindwa hata aweke wapi?
Au wewe ulikutana na yule ambae kila kituo cha kupumzika lazima aende kuchimba dawa arudi na vinywaji kwapani kama mwalimu wa hisabati na ubao wa lura?
Tuachane na hayo leo tujikite kwenye jamii zetu na utamaduni wa ulaji wa vyakula.
Bila shaka kila jamii ina utamaduni wake wa ulaji aina fulani ya vyakula kulingana na upatikanaji wake ingawaje watu wa mjini hula wao kinachopatikana sokoni.
Ukimuuliza mtu wa kigoma "ugali wa lowe" ni kitu gani ataacha shughuli anayoifanya akusimulie utamu wa ugali huo wenye mchanganyiko wa viazi.
Wanyamwezi hawaiti tena Lowe wao wana jina la kipekee huuita "Matoborwa" ingawaje ni aina ileile ya chakula kinacho lingana na lowe kiuandaaji na upishi.
Niseme nini kuhusu watu wa Tukuyu na kile chakula chao "kifughe"? hebu tuketi nikusimulie simulizi za vyakula vya asili.
Katika jamii hivi karibuni kula vyakula vya asili ni kama uganga wa kienyeji watu wanashika kichwa au kiuno wakikuona unakula bila hofu.
Jamii inaamini kwenye kukaangiza zaidi kuliko kuchemsha au kuchoma.
Nimethubutu kuwauliza watoto wa hapa Tukuyu, mkoani Mbeya walio zaliwa miaka ya 2000 waniambie kuna aina ngapi za ugali?
Wengi wakaniona mjinga ninae uliza swali jepesi wengi wao wakajibu zipo mbili tu Sembe na dona hakika nimecheka.
Hii inaonyesha dhahiri kuwa jamii imekuwa ya ki-mayai mayai mno watoto wanalishwa vitu vya dukani na viwandani.
Nimemkumbuka Mwalimu wangu nikiwa sekondari yeye aliyekuwa na utamaduni wa kufungasha kiporo cha dona na mikate ya kikinga akikisweka mdomoni pindi aendapo kazini.
Yako wapi sasa?
"Kipindi kile ukiwa na safari mama au bibi anakuandalia mkate wa mahindi mabichi maarufu kama Kisyesye, ili ule mpaka mwisho wa Safari" aliwahi kusema kusema Francis Mwalugaja mhenga mmoja wa Mwakaleli.
Utamaduni huu haupo kwa sasa badala yake wasafiri hupoteza maelfu ya fedha kununua miguu ya kuku na chipsi pale Comfort hotel wakeinda Dar es na mikoa ya pwani.
Nikajiuliza tena iwapo watoto hawa hawajui aina za ugali, itakuweje nikiwaambia kuna ugali unaotokana na ndizi si wataniona mshirikina.
Haya ni matokeo hasi ya maendeleo ya jamii, tumepoteza uhalisia sambamba na kuweka rehani afya zetu.
Mboga zetu za asili zimepotea tumehamia kula chainizi "Chinese" viazi havinogi tena tunakula chipsi hii ni ajabu sana.
Babu yangu hayati Kajubili alipanda mimea jamii ya viazi vikuu "Vitughu" nilimuona mtu mwenye kutulisha madudu kwakua havikua na radha na ukijaribu kuweka chumvi umeharibu.
Lakini hivi Sasa nimeanza kuamini kuwa wazee wa zamani walikuwa na maono juu ya afya zetu na walijaribu kutufundisha ili mbeleni tuishi vema.
Tudumishe utamaduni wa asili wa vyakula ili kuzilinda afya zetu.
Peter Mwaihola
Au wewe ulikutana na yule ambae kila kituo cha kupumzika lazima aende kuchimba dawa arudi na vinywaji kwapani kama mwalimu wa hisabati na ubao wa lura?
Tuachane na hayo leo tujikite kwenye jamii zetu na utamaduni wa ulaji wa vyakula.
Bila shaka kila jamii ina utamaduni wake wa ulaji aina fulani ya vyakula kulingana na upatikanaji wake ingawaje watu wa mjini hula wao kinachopatikana sokoni.
Ukimuuliza mtu wa kigoma "ugali wa lowe" ni kitu gani ataacha shughuli anayoifanya akusimulie utamu wa ugali huo wenye mchanganyiko wa viazi.
Wanyamwezi hawaiti tena Lowe wao wana jina la kipekee huuita "Matoborwa" ingawaje ni aina ileile ya chakula kinacho lingana na lowe kiuandaaji na upishi.
Niseme nini kuhusu watu wa Tukuyu na kile chakula chao "kifughe"? hebu tuketi nikusimulie simulizi za vyakula vya asili.
Katika jamii hivi karibuni kula vyakula vya asili ni kama uganga wa kienyeji watu wanashika kichwa au kiuno wakikuona unakula bila hofu.
Jamii inaamini kwenye kukaangiza zaidi kuliko kuchemsha au kuchoma.
Nimethubutu kuwauliza watoto wa hapa Tukuyu, mkoani Mbeya walio zaliwa miaka ya 2000 waniambie kuna aina ngapi za ugali?
Wengi wakaniona mjinga ninae uliza swali jepesi wengi wao wakajibu zipo mbili tu Sembe na dona hakika nimecheka.
Hii inaonyesha dhahiri kuwa jamii imekuwa ya ki-mayai mayai mno watoto wanalishwa vitu vya dukani na viwandani.
Nimemkumbuka Mwalimu wangu nikiwa sekondari yeye aliyekuwa na utamaduni wa kufungasha kiporo cha dona na mikate ya kikinga akikisweka mdomoni pindi aendapo kazini.
Yako wapi sasa?
"Kipindi kile ukiwa na safari mama au bibi anakuandalia mkate wa mahindi mabichi maarufu kama Kisyesye, ili ule mpaka mwisho wa Safari" aliwahi kusema kusema Francis Mwalugaja mhenga mmoja wa Mwakaleli.
Utamaduni huu haupo kwa sasa badala yake wasafiri hupoteza maelfu ya fedha kununua miguu ya kuku na chipsi pale Comfort hotel wakeinda Dar es na mikoa ya pwani.
Nikajiuliza tena iwapo watoto hawa hawajui aina za ugali, itakuweje nikiwaambia kuna ugali unaotokana na ndizi si wataniona mshirikina.
Haya ni matokeo hasi ya maendeleo ya jamii, tumepoteza uhalisia sambamba na kuweka rehani afya zetu.
Mboga zetu za asili zimepotea tumehamia kula chainizi "Chinese" viazi havinogi tena tunakula chipsi hii ni ajabu sana.
Babu yangu hayati Kajubili alipanda mimea jamii ya viazi vikuu "Vitughu" nilimuona mtu mwenye kutulisha madudu kwakua havikua na radha na ukijaribu kuweka chumvi umeharibu.
Lakini hivi Sasa nimeanza kuamini kuwa wazee wa zamani walikuwa na maono juu ya afya zetu na walijaribu kutufundisha ili mbeleni tuishi vema.
Tudumishe utamaduni wa asili wa vyakula ili kuzilinda afya zetu.
Peter Mwaihola