nderingosha
JF-Expert Member
- Mar 20, 2011
- 4,281
- 3,243
Imenibidi nilete changamoto hii kwa jukwaa la jamii forum ili ifanyiwe kazi haraka iwezekanavyo maana sisi kama watanzania tunaweza tukawa tumeingizwa mkenge uleule kama yalivyotokea mambo ya Richmund kwamba kampuni iligundulika feki kwa kujifanya mambo yao yamefanyika USA na kwingineko ulaya huku wakijua watanzania wana tatizo kubwa la kutafuta habari muhimu (kwa maana ya kutokutafiti mambo....yaani kutotaka kutafuta ukweli wa mambo haswa yale yafanyikayo nje ya mipaka ya Tz).Ili limekuwa tatizo hata kwa professionals wetu wa ndani (sijui ni kwanini kuna uvivu wa kujua issues haswa za nje zenye uhusiano na nchi yetu??....maana huku ndiko tunakoingizwa mikenge mikubwa....angalieni issue za rada...richmond na dowans na hata madini yetu yanavyouzwa nje...na hata ufisadi kwenye mabalozi yetu...huku ndiko tunakopigwa ipasavyo....maana hatufuatilii mambo yakishatoka nje ya TZ. Nimeanza hivyo nikitaka kuleta issue hii ya sakata la malipo ya hii tozo ya ICC kwa dowans. Nimefanya utafiti na kugundua yafuatayo kuhusu mchakato mzima wa jinsi dowans wanavyodai walipewa hii tozo...(tusijirizishe sana na documents zilizotumwa tz..kwani matapeli hawajulikani kwa documents). Hili linaweza likawa ni mkenge wa kufa mtu tumeingizwa kama nchi bila kujua(kwani mara ngapi hawa hawa professionals wetu wameingia mikenge???).Nianze kufafanua kama ifuatavyo alafu niwaachie mtafakari na mchukue hatua.....kila mtu kwa nafasi yake....
- Kwa kuanza tu nianze kwa huyu bwana anayeitwa...Gerald Aksen. Huyu ameripotiwa kwenye magazeti kama ndie jaji aliyetoa eti hukumu katika kesi ya ICC International court of arbitration...yaani kesi imefanyika chini yake kama mwenyekiti. Katika profile yake huyu bwana ni retired prof.wa sheria katika law firm ya Thelen LLP-USA. Profile yake ni pana na amefanya kazi nyingi mojawapo ikiwa arbitration.Hajaandikwa kuwa aliwahi kuajiriwa na ICC ila kwasasa anafanya kazi kama self employed mediator and ADR Neutral. Katika hukumu ya ICC kwa Tanesco haijuklikani huyu bwana alitumikaje kwa ICC. Pata attachment yenye profile yake jumla hapa chini.
- Katika ICC dispute resolutions...kazi ya ADR Neutral ni kama ifuatayo: kutumia busara,utaalamu na common sense katika dispute kati ya parties (pande husika).Pia kuonyesha imani kwa pande zote husika na kusaidia pande zote husika kufikia muafaka kwa manufaa ya pande zote mbili. Pia yeye ADR neutral kazi yake kubwa si jaji bali ni facilitator(mwezeshaji)kwa pande zote mbili kufikia muafaka.Yeye pia ndie anayeweza hata kuchagua ni lugha gani itumike katika shauri ili tu pawepo na muafaka na maelewano kwa manufaa ya pande zote mbili. Sasa kama hizi ndizo kazi za ADR Neutral wa ICC katika kutatua disputes...na kama huyu bwana alitumika na kwa experience yake ilivyo kubwa kwa maswala ya arbitration.....haiwezekani kabisa Tanesco washindwe kesi ile......haiwezekani hata kidogo.Sasa tujiulize nini kimefanyika?????.Nimeambatanisha document hapa yenye mchanganuo wa kazi za ICC ADR Neutral.Huyu bwana hawezi kuwa ametumiwa na ICC bila ya kuwa ADR Neutral na kama ametumiwa kama ADR Neutral na ICC basi haiwezekani Tanesco washindwe shauri lile.
- Kama Gerald Aksen wanasema ametumika kama jaji wa ICC International court of arbitration.....pia haiwezekani kwani yeye si jaji na pia si mwanasheria tena kwani ameshastaafu.Profile yake inasema hajawahi kuwa jaji wa ICC court of arbitration.Soma attachment.
- Sheria za ICC zinasema ADR Neutral anachaguliwa kwa makubaliano ya pande mbili husika au ICC wenyewe kwa kukubaliana na pande husika.Swali: je Tanesco walishiriki vipi kumchagua Gerald Aksen kama alitumika kama ADR Neutral?
- ICC Dispute Board Centre inafanya kazi separate from the ICC International Court of Arbitration, the ICC International Centre for Expertise na pia ICC ADR Secretariat.Kama Tanesco hawakuridhika na maamuzi yaliyotolewa juu ya tuzo bado wangeweza kupeleka malalamiko kwenye ICC Dispute Board Centre au ICC ADR secretariat kama hawakuridhishwa na utendaji wa ADR Neutral. Swali: je Tanesco walifanya hivyo?????kwa mujibu wa ICC...tozo hutolewa baada ya makubaliano muafaka ya pande zote mbili.
- Types of ICC ADR techniques:
- Under the ICC ADR Rules, parties may freely choose the settlement technique they consider most appropriate to their situation.Je hili tozo lilikuwa appropriate kwa Tanesco kama mdau mmojawapo?????
- 1)Mediation: The Neutral may meet each of the parties separately to help them find common ground for resolving the dispute amicably. Je common grounds zilifikiwa na pande zote mbili???
- 2)Neutral evaluation: The parties seek the Neutral's non-binding opinion on such matters as:
- An issue of fact:-Did the maintenance teams do what was expected of them?
- A technical issue. Were the girders supplied in accordance with stress specifications? or did the generators produce emergence power to the country???(Tanzania)
- An issue of law. Did the floods that held up delivery of essential spare parts constitute force majeure?
- Then the panel either seeks a solution acceptable to all the parties or expresses an opinion on the positions of each side.
- Ukifatilia hizi techniques za ICC dispute resolution kwa vyovyote vile kama zingefuatwa kweli kweli kwa hakika Tanesco wasingeshindwa kesi. Nimeambatanisha hapa attachment yenye haya yote please read!!!!!!.Pia nimeambatanisha sheria....rules document ya ICC dispute resolution hapa.Someni muamue kama watanzania hatuingizwi technical mkenge hapa....na hawa wanasheria wetu haya mambo hawasomi?????hawa kina mwanasheria mkuu wanafanya nini jamani??????
- Kwa kumalizia tu nimtaje mshiriki mwingine katika shauri hili alikuwa huyu bwana Switilin Munyantwali.Huyu ni Mganda mwanasheria anayefanyia kazi marekani na alitumika nadhani kwa dowans. Yeye profile yake (attached) inaonyesha ni executive director wa African law institute in USA na pia ana majukumu chungu mzima....na ukiangalia huwezi amini alipata wapi muda wa kukaa kwenye shauri na kuwashinda Tanesco kwa hoja.Hawa jamaa wote wako nje ya nchi wakati Dowans walifanya kazi Tz.......na tatizo lilkuwepo tz, sasa vipi hawa jamaa washinde kesi???inaonyesha mapungufu makubwa yalikuwepo kwa upande wa Tanesco (walifanya kwa makusudi kabisa ili washindwe kesi...)kwani hakuna kigezo ambacho kingewazuia kushinda...
- Mjamaa mwingine aliyeshirikishwa na dowans kama inavyosemwa ni huyu.....Jonathan Parker....huyu bwana nimeshindwa kujua ni Jonathan yupi haswa maana wako wengi (unapo search). Nimejikuta nikifikiri kuwa ni labda mcheza cricket...maana yupo pia mcheza cricket mwenye hili jin...naomba mumtafute profile....now that you get the tip and food for thouth as Great thinkers....