Tuwache majungu katibu mkuu pekee yake haitoshi tunaomba ngeleja na malima wachie ofisi

tabu kuishi

JF-Expert Member
Apr 16, 2011
353
43
Tulichokisikia na kukiona ni muendelezo wa ujinga na umbumbu la baraza letu la mawaziri yaliyote yaliokosolewa na kurudishwakwa bajeti ya wizarani ya nishati na madini yalipita mbele ya baraza la mawaziri. Ina maana hawajaona upungufu na kasoro za bajeti ya hiyo wizara hadi kufika bungeni na kurudishwa tena.
 
Asante kwa Post yako, lakimi imepotea njia. Rudisha kwa jukwaa yake aisee.
Nachangia kidogo sasa. Kuna dhana ya kiutendaji katika
wizara, alter ego theory, kwamba maafisa wote wa wizara wanafanya kazi kama mkono wa Waziri husika. Kwa misingi hii, naona kwa kitendo cha Katibu Mkuu wizara ya madini kuhusika moja kwa moja na MEMO ya 50 million, William Ngereja hawezi akajiengua. Namuonea huruma waziri, duh!
 
Godbless Lema kaomba mwongozo kwa spika, naye kayeyusha kama kawa, kadai eti ile bajeti imeshazimwa tuwasubirie wahusika!! lema kadai mwongozo wa katibu lazima uwe na mkono na baraka kutoka kwa Waziri Ngeleja...ngoja tusubiri tuone coz akina Lema washaanza kulivalia njuga hili...Pole ngeleja
 
Na hao watu waliokula hiyo 1 bill. inabidi watajwe tuwafahamu kinaganaga.
 
Tulichokisikia na kukiona ni muendelezo wa ujinga na umbumbu la baraza letu la mawaziri yaliyote yaliokosolewa na kurudishwakwa bajeti ya wizarani ya nishati na madini yalipita mbele ya baraza la mawaziri. Ina maana hawajaona upungufu na kasoro za bajeti ya hiyo wizara hadi kufika bungeni na kurudishwa tena.
Unajua ndg yangu shida inabaki na ukweli kwamba mawaziri wote ni CCM na isotoshe wana vita vya wenyewe kwa wenyewe ili kuendelea kupotezeana dira katikta masuala ya kisiasa hulazimika kufanya mambo ndivyo sivyo hata jama anajua kua kuna kasoro katika hicho anachokubaliana nacho.Mfano mzur ni Mh. Sitta huyu ni waziri lakini si waziri mwaminifu hata kidogo katika baraza la mawaziri lililopo,amekwenda kwenye mandamano kule Mbeya akiwa anaongea na wanafunzi wa chuo kikuu akawambia serikali iwaombe radhi kwa tatizo la mgao wa umeme na kuongea hadharani kua tatizo ni mafisadi wachache wanaolingiza taifa katika tatizo la umeme kwa kusaini mikataba mibovu yenye maslahi binafsi.Sitta hakuona kwamba tatizo ni la mda mrefu tangu yeye yupo madarakani kama spika wa bunge je!Alishauri nini serikalini juu ya hilo,lakini tena je!Akiwa yeye ni mmoja wa mawaziri amewezaje kuipitisha bajeti hiyo katika vikao vyao vya mawaziri vya kupitia bajeti mbalimbali?Leo hii anatoa kauli na mambo ya siri ndani ya baraza la mawazari!CCM ijiandae kung'olewa madarakani.
 
Back
Top Bottom