Tutawaachia nini wanaotufuata?

Fundi Mchundo

Platinum Member
Nov 9, 2007
8,964
6,911
Jengo la kale Bagamoyo nusura limmalize Mchina

2008-10-17 22:22:34
Na Daniel Mkate, Bagamoyo

Mchina mmoja ambaye alikuwa msimamizi wa kampuni ya ujenzi ya CHICO inayobomoa jengo la kale lililokuwa Ofisi za Posta ya wakoloni kwa ajili ya ujenzi wa hoteli ya Sunrise, amenusurika kufa baada ya jengo hilo kuporomoka na kujeruhi watu watano.

Tukio hilo limetokea jana mishale ya saa 3.30 asubuhi, wakati mchina huyo, Bw. Tai Yang, akiwa anawasimamia mafundi waliokuwa wakiporomosha kuta za jengo hilo la kale.

Wakati wakiwa kazini, ndipo kuta za jengo hilo `zee`zikaporomoka hadi chini na kuwafunika wajenzi hao.

Majeruhi hao waliolazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo, wametajwa kuwa ni Cloud Nyenja, 25 mwenyeji wa Bagamoyo, Abdul Maulizo, 24 mkazi wa Dar es Salaam na Abdulrhaman Hamad, 24, mkazi wa Zanzibar.

Akizungumzia tukio hilo, fundi Nyenja amesema shughuli ya kubomoa kuta za jengo hilo walizianza hivi karibuni huku wakisimamiwa na Tai Yang, bila ya kuwa na hofu yoyote kuwa linaweza kuporomoka.

``Hatukutarajia kama lile jengo lingeweza kuporomoka, ingawa ni la siku nyingi... lakini tunamshukuru Mungu kwa kunusurika na kifo,`` amesema Bw. Nyenja.

Hata hivyo, Mchina huyo ambaye pia ni msimamizi wa ujenzi wa jengo jipya litakalojengwa, licha kuumia sana sehemu ya kichwa na miguuni, aligoma kuzungumza kabisa kuhusu jinsi jengo hilo zee lilivyopomoka.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Bagamoyo, Dk. Kussenah Lob, amethibitisha kuwapokea majeruhi hao na kueleza kuwa wanaendelea vizuri baada ya kuwapatia matibabu.

``Wanaendelea vizuri wote, kwani madaktari wamejaribu kuwashughulikia ipasavyo... tunashukuru Mungu hakuna aliyepoteza maisha,`` amesema Dk. Lob.

Aidha, Dk. Lob amesema kabla ya jengo halijaporomoka, waliwashauri wajenzi kutojisahau kwani kuna uwezekano wa kuweza kutokea madhara makubwa.

``Kauli yetu imethibitika leo (jana), kwani yale tuliyowaambia kupitia kwa msimamizi wao (Yang) yametokea, lakini tunashukuru hawakuweza kupoteza maisha,`` amesema.

Hiyo ni mara ya kwanza kwa magofu ya kale mjini Bagamoyo kuporomoka, na hivyo kuwatia wasiwasi wenyeji pamoja na wageni wanaotembelea magofu hayo.

Tutabaki na nini? Hivi hao watalii tunaotegemea kukaa kwenye hiyo Hoteli Sunrise watatoka wapi baada ya sisi kubomoa majengo yote ya kale?

Mji wa Dar es Salaam unasikitisha kwa kasi ya kubomea majengo ya zamani na kujenga maghorofa bila kuangalia infrastructure iliyokuwepo!

Lesser Flamingoes tunawapigia hesabu ya kuwamaliza kwa ajili ya virupia kutoka kiwanda tutakachojenga Lake Natron.

Serengeti tunajenga mahoteli na kiwanja cha ndege kuhudumia watalii watakaokuja kuangalia wanyama ambao hayo maendeleo ndiyo kiama chao!

Kweli tunajiuliza hao watoto na wajukuu wetu tutawaachia nini?

Mungu inusuru nchi yetu.
 
Tutabaki na nini? Hivi hao watalii tunaotegemea kukaa kwenye hiyo Hoteli Sunrise watatoka wapi baada ya sisi kubomoa majengo yote ya kale?

Mji wa Dar es Salaam unasikitisha kwa kasi ya kubomea majengo ya zamani na kujenga maghorofa bila kuangalia infrastructure iliyokuwepo!

Lesser Flamingoes tunawapigia hesabu ya kuwamaliza kwa ajili ya virupia kutoka kiwanda tutakachojenga Lake Natron.

Serengeti tunajenga mahoteli na kiwanja cha ndege kuhudumia watalii watakaokuja kuangalia wanyama ambao hayo maendeleo ndiyo kiama chao!

Kweli tunajiuliza hao watoto na wajukuu wetu tutawaachia nini?

Mungu inusuru nchi yetu.

Fundi Mchundo,

Hivi haya majengo si yalikuwa yamependekezwa na UNESCo kuwa yaachwe kama vitu vya kale na kihistoria? Kwa nini tumekimbilia kubomoa kumbukumbu nzuri kama hiyo? Mwandosya yuko wapi ambaye ni waziri wa Mazingira au yule wa Utamaduni?

Kwa nini tunakimbilia kufanya vitu kiholela tuu?

Kwa nini wasipeleke hawa wawekezaji kule Uswekeni ili maisha Bora yaanze kuwafikia Watanzania kama huyu Mwekezaji atajenga barabara na kuhakikisha kuna maji kufika hotelini kwake?

Ama kweli tunagidiwa kama mabwege!
 
Nilishangaa sana niliposikia kuwa hayo majengo yanabomolewa. Mimi nilidhani kuwa kwa kuwa kuna maeneo mengi tu ya kujenga hoteli za kitalii, ingekuwa vema iwapo majengo haya ya kale yangewekwa katika hali nhzuri, ili watalii waje kuyaangalia na haapo hizo hoteli zinazojengwa zingepata wateja. Sasa ukibomoa vivutio vya kihistoria, watalii watakuwa kuanghalia nini?
 
Tunauongozi ambao ni dhaifu na unaofanya maamuzi kwa niaba ya wengi ili kujinufaisha.
Once we preserve the oldies we have history can be easily passed from a generation to another.But the government is not aware nor does it care.
Ningeomba kuuliza,Ina maana kwenye hii nchi hatuna mamlaka husika inayohusiana na vito vya kale?na kama ipo hawa watu ni wa kuhoji maana am sure they also have a hand in all these!
 
Sasa ukibomoa vivutio vya kihistoria, watalii watakuwa kuanghalia nini?

Hivi haya majengo si yalikuwa yamependekezwa na UNESCo kuwa yaachwe kama vitu vya kale na kihistoria?

Mwandosya yuko wapi ambaye ni waziri wa Mazingira au yule wa Utamaduni?

Kwa nini tunakimbilia kufanya vitu kiholela tuu?


Tutabaki na nini?

Hivi hao watalii tunaotegemea kukaa kwenye hiyo Hoteli Sunrise watatoka wapi baada ya sisi kubomoa majengo yote ya kale?

Ina maana kwenye hii nchi hatuna mamlaka husika inayohusiana na vito vya kale?

Itakuwa vigumu sana kupata, na inawezekana kamwe hatutapata, majibu ya maswali haya kama hamna vyombo vya habari kwa kusaidia kufikisha mambo haya kwa wanaotakiwa kuyajibu. Hatuna press!!!

Habari inasema "Jengo la kale Bagamoyo nusura limmalize Mchina" lakini kumbe ni watu kibao wamejeruhiwa. Mwandishi kaona Mchina tu!! Hii ni mbaya kuliko "Mtu mmoja na Wamakonde wanne wapata ajali," manake angalau katika ile classic epic, Wamakonde - japo wao sio watu - walikuwa recognized katika kichwa cha habari.

Na hata kama ingekuwa ni huyu Bw. Tai Yang peke yake ndio kaumia, hutakiwi kusema "Mchina" kaumia. Kabila/rangi/Utaifa wa majeruhi unatajwa kama tu unahusiki moja kwa moja na nyeti za habari. Kitu kimoja nimejifunza katika world class press ni kwamba the only time unaweza kuandika kitu kama "aliyesababisha ajali ni African American" ni kama labda dereva mmoja alikuwa ni African American ambae kakimbia eneo la ajali, hivyo anatajwa alivyo kwa sababu anatafutwa. Vinginevyo ukitaja race ya mtu bila sababu noma!!!!

Na nigekuwa mimi mwandishi ningembana mbavu (ningejitahidi nisimbane koo ) huyu daktari aliyehitimisha kwamba wagonjwa wake wamejeruhiwa kwa sababu hawakuwa waangalifu. Umesikia wapi emergency room doctor anatibu huku anatoa public statements kuhusu uzembe wa wagonjwa kuhusiana na construction site safety ??? Yeye daktari alitembelea construction site kabla ya ajali na kugundua hatari ? Serikali ilikuwa wapi ? Au kama alikuwa anapita tu njiani akaliona hili, kwa nini alienda ku complain kwa "Mchina" tu na sio kuliwakilisha hili kwa wahusika Serikalini ?

Hayo yote ni sehemu ya uvunjaji wa hili jengo na ajali hii. Lakini ukisoma habari kwenye gazeti letu lolote unaondoka na maswali tu, binafsi huwa najisikia nimeondoka mjinga kuliko nilivyokuja, maana gazeti lina ku treat kama mjinga. Nahakika inaweza kuchukuliwa kama nimeruka nje ya mada ya uvunjaji majengo ya Kihistoria, lakini kuna siku watu wataona kwamba the press is the weakest link katika mnyonyoro wa kuvuta gurudumu la maendeleo maana haitusaidii kujua yanaondelea. Huwezi kuendelea kama hujui kinachoendelea.
 
Kuhani,
'We need people like you in the editing room. Have you ever thought about going into journalism?
 
Fundi Mchundo,

Hivi haya majengo si yalikuwa yamependekezwa na UNESCo kuwa yaachwe kama vitu vya kale na kihistoria? Kwa nini tumekimbilia kubomoa kumbukumbu nzuri kama hiyo? Mwandosya yuko wapi ambaye ni waziri wa Mazingira au yule wa Utamaduni?

Kwa nini tunakimbilia kufanya vitu kiholela tuu?

Kwa nini wasipeleke hawa wawekezaji kule Uswekeni ili maisha Bora yaanze kuwafikia Watanzania kama huyu Mwekezaji atajenga barabara na kuhakikisha kuna maji kufika hotelini kwake?

Ama kweli tunagidiwa kama mabwege!


Mimi niliamini kuwa kwa sababu Rais wetu anatoka Bagamoyo basi huo mji utapata afueni! Kumbe ndiyo imekuwa kinyume. Miradi ya bandari, air-port, prawn fishing yote itaupeleka mji huo kuzimuni! Bora waende wakaupige picha na kutangaza kuwa ruksa kubomoa na kujenga kwenye mji mkongwe.

Hao mawaziri wapo tuu. Sidhani kama wana uchungu wowote na mazingira. Ingekuwa hivyo tungewasikia wakipinga kubomolewa kwa majengo Darisalama. Lakini wapi!

Naona hata Mkurugenzi wa Mambo ya Kale amenyanyua mikono!

Iko kazi.

Amandla................
 
Back
Top Bottom