Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Nchi hii imekuwa ya kisiasa zaidi. Kila kukicha, kila kona watu wanajadili siasa. Ndani ya basi umezuka ubishi huu. Je. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni lazima awe mbunge? Au hata mtu binafsi, raia wa kawaida anaruhusiwa kugombea? Nisaidieni ndugu zangu, wasafiri wametaka kuninyofoa roho baada ya kuweka msimamo kuwa hata raia asiye mbunge anaruhusiwa kugombea. Sijui, labda sheria hii imebadilishwa kwa bahati mbaya sikuwahi kusikia. Hebu tupeane elimu ya uraia ndugu zangu ili somo liwafikie wakulima hawa. Niko kimya sasa, basi linachanja mbuga, zogo bado linaendelea.