Tutatue ubishi huu! Spika wa bungu ni lazima awe mbunge?

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Nchi hii imekuwa ya kisiasa zaidi. Kila kukicha, kila kona watu wanajadili siasa. Ndani ya basi umezuka ubishi huu. Je. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni lazima awe mbunge? Au hata mtu binafsi, raia wa kawaida anaruhusiwa kugombea? Nisaidieni ndugu zangu, wasafiri wametaka kuninyofoa roho baada ya kuweka msimamo kuwa hata raia asiye mbunge anaruhusiwa kugombea. Sijui, labda sheria hii imebadilishwa kwa bahati mbaya sikuwahi kusikia. Hebu tupeane elimu ya uraia ndugu zangu ili somo liwafikie wakulima hawa. Niko kimya sasa, basi linachanja mbuga, zogo bado linaendelea.
 
Spika siyo lazima awe Mbunge ndiyo maana kama nakumbuka vizuri Mabere Marando naye aligombea u-spika kupitia Chadema. Mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania mwenye sifa zinazotakiwa anaweza kugombea.
 
Waulize kama wanawajua waliokuwa wagombea wa uspika wa bunge hili? Wakishindwa kujibu waache? Wakiweza waulize Marando ni mbunge wa Jimbo gani?
 
ikiwa umeamua kuleta thread hii hapa, nadhani unahitaji mawazo ya wana JF.
Mkuu hoja yako iko sahihi kabisa, huitaji 'nondo' toka Jamiiforum;
mgombea binafsi nafasi ya Spika wa
bunge la Tz kikatiba anaruhusiwa kikatiba. Kama hao abiria wenzako wanazidi kuwa wabishi, achana nao.
 
Nchi hii imekuwa ya kisiasa zaidi. Kila kukicha, kila kona watu wanajadili siasa. Ndani ya basi umezuka ubishi huu. Je. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni lazima awe mbunge? Au hata mtu binafsi, raia wa kawaida anaruhusiwa kugombea? Nisaidieni ndugu zangu, wasafiri wametaka kuninyofoa roho baada ya kuweka msimamo kuwa hata raia asiye mbunge anaruhusiwa kugombea. Sijui, labda sheria hii imebadilishwa kwa bahati mbaya sikuwahi kusikia. Hebu tupeane elimu ya uraia ndugu zangu ili somo liwafikie wakulima hawa. Niko kimya sasa, basi linachanja mbuga, zogo bado linaendelea.
Ulikuwa na haraka ya kutafuta mada, Heading yako BUNGU NI NINI????? nadhani hii majibu yapo wazi hata wewe waweza kwenda ili mradi ukidhi haja ya katiba mbovu iliyopo kwa sasa
 
naona mchangiaji wa kwanza kashakujibu. Hata advocate mabere marando,raia na mwanaharakati ameshawai kugombea uspika akitokea nje ya bunge. cha muhimu uwe na sifa za kuwa mbunge basi.
 
Ulikuwa na haraka ya kutafuta mada, Heading yako BUNGU NI NINI????? nadhani hii majibu yapo wazi hata wewe waweza kwenda ili mradi ukidhi haja ya katiba mbovu iliyopo kwa sasa

Ha ha haaa, doh. BUNGU isikusumbue mkuu mladi umeelewa, si unajua ndani ya chombo alafu barabara zenyewe za vumbi huku vijijini. Badala ya kubofya A unaweza kuangukia kwenye Z.
 
Spika siyo lazima awe Mbunge ndiyo maana kama nakumbuka vizuri Mabere Marando naye aligombea u-spika kupitia Chadema. Mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania mwenye sifa zinazotakiwa anaweza kugombea.

Jibu ndiyo hilo,sheria inasema inaongeza kuwa lazima awe na sifa za kuchaguliwa kuwa mbunge,hii ina maana kuwa mara atakaposhinda uspika moja kwa moja anakuwa sehemu ya bunge,hivyo lazima awe na sifa za ubunge.
 
Jibu ndiyo hilo,sheria inasema inaongeza kuwa lazima awe na sifa za kuchaguliwa kuwa mbunge,hii ina maana kuwa mara atakaposhinda uspika moja kwa moja anakuwa sehemu ya bunge,hivyo lazima awe na sifa za ubunge.
Mkuu si lazima awe mbunge ila kama ulivyosema anatakiwa awe na sif za kuwa kuchaguliwa kuwa mbunge. Aina za wabunge ni wa kuchaguliwa, viti maalum, wawakilishi toka baraza la wawakilishi na ex officio kama AG. Rais ni sehemu ya bunge. Hapa tunapata tofauti kati ya Parliament na National Asembly.
 
Mkuu si lazima awe mbunge ila kama ulivyosema anatakiwa awe na sif za kuwa kuchaguliwa kuwa mbunge. Aina za wabunge ni wa kuchaguliwa, viti maalum, wawakilishi toka baraza la wawakilishi na ex officio kama AG. Rais ni sehemu ya bunge. Hapa tunapata tofauti kati ya Parliament na National Asembly.

sifa za kuchaguliwa ubunge zinafahamika,hizi za kuteuana sina maelezo nazo,mfano mwingine kumbuka pia waziri mkuu lazima awe mbunge wa kuchaguliwa rais hawezi kumteua mbunge na akampa uwaziri mkuu au mbunge wa viti maalum awezi kuwa waziri mkuu na wote wanaingia jengo moja na kuchangia sawa,so hii mikanganyiko ya sheria tuachie wanasheria,lakini sheria inasema lazima awe na sifa za kuchaguliwa kuwa mbunge,upungufu hapa naouona ni kuwa hata maji marefu au lameck airo naye anasifa,au kuna sifa za ziada ili uwe mgombea wa uspika?
 
Nchi hii imekuwa ya kisiasa zaidi. Kila kukicha, kila kona watu wanajadili siasa. Ndani ya basi umezuka ubishi huu. Je. Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni lazima awe mbunge? Au hata mtu binafsi, raia wa kawaida anaruhusiwa kugombea? Nisaidieni ndugu zangu, wasafiri wametaka kuninyofoa roho baada ya kuweka msimamo kuwa hata raia asiye mbunge anaruhusiwa kugombea. Sijui, labda sheria hii imebadilishwa kwa bahati mbaya sikuwahi kusikia. Hebu tupeane elimu ya uraia ndugu zangu ili somo liwafikie wakulima hawa. Niko kimya sasa, basi linachanja mbuga, zogo bado linaendelea.

Majibu yako yalikuwa sahihi, isipokuwa wasi wasi wako.
Ila katika swali lako hilo napenda na mimi niulize swali pacha. Je kwa mtu ambaye tayari ni mbunge wa Chama, anaweza kugombea nafasi ya Speaker bila kupitia Chama Chake, kwamba mimi ni mbungewa chama X, lakini nagombea nafasi hiyo pasi kukiwakilisha Chama, Je inaruhusiwa?
 
Majibu yako hayakuwasahihi, isipokuwa wasi wasi wako.
Ila katika swali lako hilo napenda na mimi niulize swali pacha. Je kwa mtu ambaye tayari ni mbunge wa Chama, anaweza kugombea nafasi ya Speaker bila kupitia Chama Chake, kwamba mimi ni mbungewa chama X, lakini nagombea nafasi hiyo pasi kukiwakilisha Chama, Je inaruhusiwa?

Mh! Hiyo nayo. Acha tusubiri wataalamu wa sheria watusaidie.
 
Back
Top Bottom