Uchaguzi 2020 Tundu Lissu: Kamati Kuu itakaa kutoa msimamo rasmi juu ya Mbunge wa Nkasi, Aida Khenan

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,194
4,116
Aida Khenan mbunge mteule wa Nkasi amesema, yeye ni mbunge pekee aliyetangazwa na katika mkoa wake amepata madiwani 10.

Lakini amesema amesikia kwenye mitandao kuhusu msimamo wa chama chake lakini yeye hajapewa taarifa rasmi eidha ya simu au barua, anadai anaamini chama chake ni taasisi kubwa hivyo anategemea atapewa taarifa rasmi.

Amesema jimboni kwake na mkoani kwake mpaka sasa kuna taharuki kubwa, wananchi wana taharuki kubwa.

Amesema mpaka sasa ametishiwa maisha na wananchi kwa kuwa wao waliamua kuvunja rekodi ya kutoa Mbunge mwanamke kwa mara ya kwanza hivyo wanadai yeye akifuata msimamo wa chama atakuwa kawasaliti wananchi ambao wapo walioumia ili yeye ashinde, pia amesema kuna kesi kama 18 za watu waliokamatwa walipokuwa wanapigania yeye ashinde.

Amedai wananchi wanamwambia kuwa machozi yao hayawezi kwenda bure asipokwenda kuwatumikia bora maisha yake wananchi wayamalize hapo.

Amedai kuwa anaomba chama chake warudie upya kutazama maamuzi yao, na kama waliyatoa kwa jazba kulingana na yaliyotekea kwenye uchaguzi basi waangalie upya na waelewe kuwa yeye hana amani anatishiwa maisha na amedai hawezi kuhama Rukwa na hawezi kuhama Nkasi.

Amedai kuwa kwa mara ya kwanza kwenye jimbo lao wamepata Mbunge mwanamke na Mbunge wa kutoka upinzani hivyo asipokwenda kuwawakilisha wananchi madhara yake ni makubwa sana kwake aidha hata kama viongozi wake hawatayaona.

Amesema alisharipoti Polisi kuhusu kutishiwa maisha na pia msimamo huo si wake peke yake bali ni wake na viongozi wa mkoa wa chama cha CHADEMA.

Amesema katika ngazi ya taifa hakuna kiongozi yeyote aliyemtafuta hata kwa simu aweze kujua amani yake au usalama wake.

Amedai kuwa alipoomba nafasi ya Ubunge aliomba peke yake na wala hawakuomba 2 wala 3 hivyo atakwenda bungeni kama yeye Aida na atakwenda kuwasilisha sauti yake yeye peke yake kwa niaba ya wananchi wa Nkasi japo atakuwa mpweke ndani ya bunge. Anasema alipokuwa mbunge wa viti maalum alijifunza kutoka kwa wabunge waliomtangulia lakini kama wabunge wa Viti Maalum watakwenda kipindi hiki atapata faraja lakini wasipokwenda itakuwa mpweke lakini faraja atapata kwa wananchi waliomchagua anaowawakilisha.

Tundu Lissu nae anena haya
Tundu Lissu anena kuwa, keshokutwa watakaa kamati kuu na ndio itatoa msimamo wa jumla wa chama, msimamo ambao waliusema wiki iliopita ni msimamo wa viongozi wakuu wa chama, lakini lazima kamati kuu itoe baraka zake au ikatae kutoa baraka zake.

Tundu Lissu amedai kuwa wao hawakua na wajibu wa kuuliza yeye Aida anafikiriaje kwa kuwa wao viongozi wakuu wana majukumu mengine ndani ya chama, amedai kuwa wao walitoa msimamo wao kuwa huo haukuwa uchaguzi.

Amedai kuwa kama chama kikisema kuwa huo ndio msimamo wa chama basi itabidi atafute utaratibu mwingine wa kuwatumikia wananchi wa Nkasi kwa kuwa Tanzania hakuna mbunge binafsi bali ni wabunge wa chama hivyo wabunge ni lazima wafuate utaratibu wa chama.
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
Huoni kuwa anaemuibia Masikini kila awamu ndio mbinafsi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse
Si mlitaka 100% kufuta CDM bungeni, mnalialia nini sasa?
 
Jamaa wabinafsi sana

Lowassa 'alipoibiwa'kura hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Slaa 'alipoibiwa' kura wao hawakususa kwenda Bungeni kwa kuwa wao walipata Ubunge

Safari hii kwa kuwa wao binafsi 'wameibiwa' wanataka hata 'wasioibiwa' wasuse

Mkuu bila kupinga maelezo wala mapendekezo yako, kwahiyo unaona ni sawa uchaguzi kwa sasa kufanyika kwa wizi na yoyote atakayepata katika mazingira ya wizi watu wasichukue hatua yoyote.

Mimi kwangu nadhani huyo dada aachwe aende bungeni kutafuta kipato maana maisha ni magumu. Lakini hakuna lolote linaenda kujadiliwa humo ndani zaidi ya kumsujudia Magufuli, na kutaka kumuongezea muda wa kukaa madarakani.
 
Trump anapolia lia kuibiwa kura kaambiwa weka ushahidi valid mezani sio blaa blaaa

Wekeni mezani mlipata majimbo mangapi na yepi CCM wameshinda kihalali

Tangu 1995 hakuna Uchaguzi ambao Wapinzani hawajadai kushinda lakini wakiulizwa Ushahidi wanatoa ushahidi mwepesi mwepesi kweli

Trump kaonesha Masanduku ya kura 53 ya njia ya posta yalicheleweshwa kuingizwa kwenye chumba cha kuhesabia kura kaambiwa ushahidi mwepesi sana

So wekeni ushahidi ili mjadala uwe kwenye kujadili ushahidi wenyewe kuepusha ubishi kimbunga wa ama ziliibiwa au laa
Mkuu bila kupinga maelezo wala mapendekezo yako, kwahiyo unaona ni sawa uchaguzi kwa sasa kufanyika kwa wizi, na yoyote atakayepata katika mazingira ya wizi watu wasichukue hatua yoyote.

Mimi kwangu nadhani huyo dada aachwe aende bungeni kutafuta kipato maana maisha ni magumu. Lakini hakuna lolote linaenda kujadiliwa humo ndani zaidi ya kumsujudia Magufuli, na kutaka kumuongezea muda wa kukaa madarakani.
 
Sie tunalia lia?

Wanaolia lia wameripoti Ostybay Police wakapigwa bench masaa kadhaa na mwingine kajipeleka Ukimbizini Ubalozin wakati wiki iliyopita walituambia saa hizi watakuwa Mmoja Rais mwingine PM
Sasa nchi mmepewa,bado mnahangaika nao,kunani?Bado mmefunga mitandao ya kijamii,hofu yenu nini?
Acheni maisha yaendelee,sisi wapenzi wa upinzani tumeshakubali mchukue kila kitu kwa 100%!Kwanini bado hamridhiki?
Mna matatizo,sio bure!
Acheni kulia lia,tekelezeni ahadi mlizowaahidi watanzania!
 
Ahadi moja wapo ni 'kulinda amani kwa gharama yeyote ile' kwa hiyo ukosefu wa internet ndio moja ya gharama yeyote ile
Sasa nchi mnepewa,bado mnahangaika nao,kunani?Bado mmefunga mitandao ya kijamii,hofu yenu nini?
Acheni maisha yaendelee,sisi wapenzi wa upinzani tumeshakubali mchukue kila kitu kwa 100%!Kwanini bado hamridhiki?
Mna matatizo,sio bure!
Acheni kulia lia,tekelezeni ahadi mlizowaahidi watanzania!!!
Shwain!!!!
 
Sie tunalia lia?

Wanaolia lia wameripoti Ostybay Police wakapigwa bench masaa kadhaa na mwingine kajipeleka Ukimbizini Ubalozin wakati wiki iliyopita walituambia saa hizi watakuwa Mmoja Rais mwingine PM
Sasa hivi wanaolia-lia ni wapinzani.

Hilo siyo jambo jema katika taifa.

..siyo jambo ambalo chama tawala kinatakiwa kujivunia.

..kwani kuna shida gani kuunda tume ya uchaguzi itakayokidhi matakwa ya wadau wengi zaidi wa siasa?
 
Back
Top Bottom