Tundu Lissu ahojiwa kwa kumwita Rais Magufuli "Mtakatifu". Aachiwa...

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameachiwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam na pia polisi mkoa wa kipolisi Ilala.

Amehojiwa ni kwanini anamwita Mheshimiwa kuwa ni Mtakatifu.

Amehoji akiita "lile jina" ambalo limemfanya awe na kesi kadhaa mahakama ya Kisutu ni shida. Je, na hili la Mtakatifu ni shida?

Amehojiwa aeleze maana ya Mtakatifu akaeleza ni asiye na hatia mbele ya Mungu na wanadamu.

Amehojiwa pia kuhusu kikosi kazi kinachotesa watuhumiwa wanaokuwa chini ya polisi lakini huchukuliwa na kupelekwa kwenye chumba cha mateso na kurejeshwa alfajiri Central.

Amewaambia yeye ameongea na walioteswa na kuna wapo walio tayari kutoa ushahidi kuhusu ukatili wa kikosi kazi hicho.

RCO wa Ilala amekana na kusema kuwa watuhumiwa huwa hawateswi.

Lissu pia amehojiwa kuhusu sakata la kupotea Ben Saanane na polisi wanavyoweza kumtafuta amewaambia watafute mawasiliano yake ya mwisho waseme Saanane yuko wapi.

Lissu amekuwa polisi akiwa na Wakili Fred Kihwelo tangu saa nne hadi saa kumi na nusu.

Polisi wamefungua jalada la uchunguzi kuhusu maelezo hayo.
Hivi Think tank ya polisi ni nani ? Yaani yule anayewaelekeza polisi kwamba huyu akamatwe kwa kuwa kafanya hivi au vile , ni nani hasa ?
 
TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameachiwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Mapema leo asubuhi Lissu alikamatwa na kupelekwa kituoni hapo ambapo ilielezwa kuwa alichukuliwa kwa lengo la kuhojiwa kuhusiana na mkutano aliofanya na waandishi wa habari kuhusu wa kupotea kwa Bernard Saanane.

Ben Saanane alikuwa Msaidizi wa Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa – alipotea ghafla takribani mwezi mmoja sasa na hajulikani alipo huku Lissu akiitisha mkutano na wanahabari tarehe 14 Desemba, 2016 na kuitaka serikali ieleza kama inamshikilia kijana huo au la.

Fredrick Kihweru mmoja kati ya wanasheria wa Chadema akitoa maelezo baada ya mahojiano ya polisi na Lissu kumalizika amesema, “aliitwa kuhojiwa juu ya Press conference aliyofanya na kuzungumzia suala la Saanane lakini pia wamemuhoji anamaanisha nini kumwita Rais John Magufuli jina la “Mtukufu.”

Itakumbukwa kuwa Lissu amekuwa akimtaja Rais Magufuli kama “mtukufu” mara kadhaa tangu aliposhitakiwa kwa kutamka kuwa “Dikteta uchwara anapaswa kupingwa kwa nguvu zote” kesi ambayo bado inaendelea mahakamani.

Wakili Kihweru amesema Lissu amehojiwa pia kuhusu hatua yake ya kuitaka Serikali iseme kama haimshikilii Ben Saanane na pia ieleze juu ya mawasiliano yake ya mwisho ya Ben alifanya na nani, wapi na waliwasiliana nini.

Baada ya mahojiano hayo Lissu ameachiwa kwa dhamana na anaweza kuitwa wakati mwingine atakapohitajika.
 
Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ameachiwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam na pia polisi mkoa wa kipolisi Ilala.

Amehojiwa ni kwanini anamwita Mheshimiwa kuwa ni Mtakatifu.

Amehoji akiita "lile jina" ambalo limemfanya awe na kesi kadhaa mahakama ya Kisutu ni shida. Je, na hili la Mtakatifu ni shida?

Amehojiwa aeleze maana ya Mtakatifu akaeleza ni asiye na hatia mbele ya Mungu na wanadamu.

Amehojiwa pia kuhusu kikosi kazi kinachotesa watuhumiwa wanaokuwa chini ya polisi lakini huchukuliwa na kupelekwa kwenye chumba cha mateso na kurejeshwa alfajiri Central.

Amewaambia yeye ameongea na walioteswa na kuna wapo walio tayari kutoa ushahidi kuhusu ukatili wa kikosi kazi hicho.

RCO wa Ilala amekana na kusema kuwa watuhumiwa huwa hawateswi.

Lissu pia amehojiwa kuhusu sakata la kupotea Ben Saanane na polisi wanavyoweza kumtafuta amewaambia watafute mawasiliano yake ya mwisho waseme Saanane yuko wapi.

Lissu amekuwa polisi akiwa na Wakili Fred Kihwelo tangu saa nne hadi saa kumi na nusu.

Polisi wamefungua jalada la uchunguzi kuhusu maelezo hayo.
nimesoma ulicho kiandika hakika na wewe umeandika kichadema ....
Lissu na Mbowe wanajua Ben alipo
 
TUNDU Lissu, Mbunge wa Singida Mashariki kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ameachiwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa Jeshi la Polisi katika Kituo Kikuu cha Kanda Maalum ya Dar es Salaam.

Mapema leo asubuhi Lissu alikamatwa na kupelekwa kituoni hapo ambapo ilielezwa kuwa alichukuliwa kwa lengo la kuhojiwa kuhusiana na mkutano aliofanya na waandishi wa habari kuhusu wa kupotea kwa Bernard Saanane.

Ben Saanane alikuwa Msaidizi wa Freeman Mbowe Mwenyekiti wa Chadema Taifa – alipotea ghafla takribani mwezi mmoja sasa na hajulikani alipo huku Lissu akiitisha mkutano na wanahabari tarehe 14 Desemba, 2016 na kuitaka serikali ieleza kama inamshikilia kijana huo au la.

Fredrick Kihweru mmoja kati ya wanasheria wa Chadema akitoa maelezo baada ya mahojiano ya polisi na Lissu kumalizika amesema, “aliitwa kuhojiwa juu ya Press conference aliyofanya na kuzungumzia suala la Saanane lakini pia wamemuhoji anamaanisha nini kumwita Rais John Magufuli jina la “Mtukufu.”

Itakumbukwa kuwa Lissu amekuwa akimtaja Rais Magufuli kama “mtukufu” mara kadhaa tangu aliposhitakiwa kwa kutamka kuwa “Dikteta uchwara anapaswa kupingwa kwa nguvu zote” kesi ambayo bado inaendelea mahakamani.

Wakili Kihweru amesema Lissu amehojiwa pia kuhusu hatua yake ya kuitaka Serikali iseme kama haimshikilii Ben Saanane na pia ieleze juu ya mawasiliano yake ya mwisho ya Ben alifanya na nani, wapi na waliwasiliana nini.

Baada ya mahojiano hayo Lissu ameachiwa kwa dhamana na anaweza kuitwa wakati mwingine atakapohitajika.
Nadhani salutation ya mtukufu siyo kosa la jinai
 
Iteni majina yote lakini ikulu hamgusi milele.....2020 ni kuchinjwa tena
 
Back
Top Bottom