Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,150
SHUTUMA DHIDI YANGU (AFRICAR KAGEMA) KUTOKA SALES TEAM
Ni wajibu wetu sote kutambua kuwa biashara sio siasa na aihitaji mambo ya kisiasa badala yake inahitaji uwajibikaji na uzalendo kwa kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kwa kutumia elimu yake na upeo wa uelewa wake kuhakikisha kampuni inayofanya biashara ya faida iweze kufanya hivyo kwa manufaa yetu sote.
Kabla sijaeleza yaliyojiri siku ya jumamosi tarehe 26/09/09 kwenye mkutano wa wafanyakazi uliohusu kupunguza wafanyakazi, napenda kusema kuwa nimesikitishwa na nimefedheheshwa sana na majibu ya shutuma yaliyotolewa na sales team kujibu hoja ambazo sikuzitoa kwenye mkutano huo.
Hoja zangu kwenye mkutano huo wa tarehe 26/09/09 zilizogawanyika katika mada mbili ambazo nilizitoa kwa maadishi ambayo nakala yake wanayo COWTU zilikuwa ni;
i. Kutopunguza Wafanyakazi
ii. Kupunguza Wafanyakazi
Katika maelezo haya nitaijadili mada moja tu yaani Kutopunguza wafanyakazi ambayo sales Team wameijibu kama ifuatavyo;
KUTOPUNGUZA WAFANYAKAZI
1. MAPATO
Mimi nilipingana na zoezi la kupunguza wafanyakazi kama kigezo cha kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni badala yake niliomba kampuni kufanya yafuatayo ili kuongeza mapato na kupunguza gharama za kampuni;
a) Kuimarisha (Kuboresha) Vituo vyake vya Mauzo
Nilitoa rai kwa kampuni kurekebisha vituo vyake vya mauzo ili kukabiliana na ushindani uliopo katika soko. Nikitolea mfano wa vituo vya ATC House na Interline sales counters ambavyo mazingira yake yanakuwa kana kwamba Air Tanzania haina ushindani wowote katika soko hivyo kwa mazingira yoyote yale wateja watakuja tu kununua tiketi.
b) Kupunguza tiketi za bure yaani Liberty
Nilishauri kampuni kupunguza kutoa tiketi za liberty kwa wafanyakazi na management na watu wengine kwani tiketi hizi ndizo chanzo cha kupungua kwa mapato kwa kampuni. Niliendelea kusisitiza kuwa liberty hazina control yoyote na watu wa Fedha (Finance) hivyo hakuna mtu anayejua kuwa kampuni inapoteza kiasi gani kwa siku, Mwezi au Mwaka kutokana na tiketi hizi. Nilitolea mfano kuwa tiketi hizi zinatolewa na watu wa record na Commercial bila kuwahusisha watu wa Finance hivyo kutojua hasara inayopatikana.
c) Kuimarisha uhusiano mzuri kati ya Air Tanzania na Travel Agents ndani na nje ya nchi.
Nilikubushia kuweka uhusiano mzuri kati ya Air Tanzania na Travel Agents wa ndani na nje ya nchi kwani travel agents wanachukua nafasi kubwa katika mapato ya kampuni.
Uhusiano wa Ndani.
Nikielezea uhusiano wa ndani niliwakumbusha watu wa Commercial kuwa wanapaswa kutoa majibu yanayojitosheleza kwa travel agents kuhusu masuala yanayohusu uhasibu au BSP na kama wanaona hawana utaalam nayo wanapaswa kuniuliza ua kumuuliza mtu wa BSP kwa sasa AFRICAR ili wapate majibu sahihi badala ya kutoa shutuma kuwa mtu wa BSP ndiyo kikwazo cha matatizo yao.
Nikielezea kuhusu matatizo yanayojitokeza mara kwa mara ya refunds wakati mwingine zinachelewa kutokana na utaratibu niliojiwekea kwamba lazima zichunguzwe na watu wa Help desk au Mama Kikowe na kuzifunga kwanza ndipo nizifanyie kazi. Vilevile ifahamike kuwa wakati mwingine tiketi hazionekani kwenye system kwa hiyo mimi (Africar) na watu wa help Desk inabidi kuomba msaada kutoka SITA, ATLANTA AU MERCATOR ili kujua status zake.
Uhusiano wa nje.
Niliikumbusha kampuni kuangalia upya soko la South Africa kwani mpaka sasa Travel Agents wanadai ZAR 1,269,618@ 168 = TZS 213,295,824 credit card refunds ambazo zitaisumbua sana kampuni ikianza safari zake huko. Kampuni itambue kuwa deni hili halijalipwa kwa muda mrefu tangu December 2008.
d) Kulifanyia Matengenezo jingo la ATC House.
Nilitoa wito kwa kampuni kulifanyia matengenezo jengo la ATC House ili lipangishwe kwa kutangaza tenda na makampuni makubwa tu ndio yapewe nafasi yatakayoweza kupanga floor nzima ili kuweza kupata pesa nyingi kwa mkupuo kuliko hizi pesa ndogo ndogo tunazopata kwa sasa.
Nilipendekeza ukarabati ufanyike ili kubadilisha mabati juu ya paa ambayo yameoza na yanavuja hivyo kuleta usumbufu kwa wapangaji ikiwa ni pamoja na mabomba ya maji machafu.
Vilevile nilipendekeza wafanyakazi wa ATC House wahamie Mezzanine Floor kama ilivyokuwa zamani na kupangisha ghorofa ya kwanza,pili na Tatu.
e) Mikataba Mibovu
Nilitoa ushauri kwa kuirekebisha mikataba yote mibovu na inayopunguza mapato ya kampuni kama vile mikataba ya Miss Tanzania ambayo ni dhahiri kuwa haiinufaishi Air Tanzania badala yake inawanufaisha hawa Miss Tanzania na wenzao. Ni ukweli usiopingika kuwa Miss Tanzania inaitangaza Air Tanzania wakati wa mchakato wa kumpata Miss Tanzania tu lakini baada ya hapo hawaisaidii kampuni hii, hivyo wanapanda ndege bure tu. Niliomba mikataba hiyo iwe ya kipindi Fulani tu hasa wakati wa mchakato.
Vilevile mikataba ya Clouds FM ambayo nayo sio kila siku inaitangaza Air Tanzania, lakini wafanyakazi wake wanatumia liberty kila mara.
Hivyo ni wajibu wa kampuni kuangalia upya mikataba kama hii ili kuinusuru kampuni na kuongeza mapato yake.
f) Kuimarisha Kitengo cha mawasiliano.
Nilitoa wito kwa kampuni kuimarisha kitengo hiki ili wateja wetu wapewe maelezo au taarifa mapema inapotokea mabadiliko yoyote katika ndege zetu. Nilitolea mfano wa abiria ambao walijikuta wanasafiri hadi Kigoma wakati wao walikuwa wanaenda Tabora kwenye mkutano. Nikitolea mfano kama huu hapa chini,
Dear Rashida,
First of all may I take this opportunity to apologize for the inconveniences caused to our valuable customers due to unexpected schedule change of our flight to TBO.
Please convey our sincere apologies.
ATTN: Africar kindly processes ACM as requested and please waive all charges.
MBWETTE/TOLLYPROF (PNR# ZV6KGU, TKT# 197 3360837165)
VARISANGA/MODESTPROF (PNR# N62L3A, TKT# 197 336083716
MARGESON/DALOTTAPROF (PNR# N62L3A, TKT# 197 3360837167
2. MATUMIZI
Katika kipengele hiki niliiomba kampuni kupunguza matumizi katika mambo yafuatayo;
a) Kupunguza Duty Travel zisizokuwa za lazima kwa wafanyakazi na management.
b) Kupunguza matumizi mengine yoyote yasiyokuwa ya lazima ili kuinusuru kampuni na gharama zisizokuwa za lazima na kubana matumizi ikiwa ni pamoja na mikataba mibovu.
KUJIBU TUHUMA ZA SALES TEAM
Kwanza ni matumaini yangu kuwa kwa wale waliokuwepo kwenye mkutano huu watakubaliana na mimi kuwa hayo maneno na lugha iliyotumika haikuwepo kwenye mkutano ule. Vilevile ukisoma kwa umakini sana utagundua kuwa hawa watu wanageneralize tuhuma zao na hawako specific kwa kila kauli wanayodai kama vile
Quote Sales wamebweteka tu na hawafanyi kazi yoyote, hawana uhusiano mzuri na Ma-Ajenti wanao tuuza. Pia Sales hawajui wafanyalo wanaleta mkongamano na BSP/Agents, na kwamba tuje kwako utufundishe kazi. Hizi ni shutuma nzito na zinatia karaha, hasa kutoka kwa mtu kama wewe Afrika.
Napenda kusema kuwa hizi kauli hazikutolewa na mtu yeyote kwenye mkutano huo. Hivyo huku ni kupotosha jamii ya ATCL hasa ambao hawakuhudhuria mkutano huo waelewe hivyo. Hizi ni hadithi za kutunga kwani hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kutamka maneno haya.
Quote Sisi tunaichukulia kuwa hukutoa shutuma hizi kwa nia njema ya kujenga, bali kama kawaida yako, lazima ukosoe ili uonekane unajua, hata ikibidi kuwadhalilisha viongozi wa juu sana kwako.
Napenda kusema kuwa kwenye mkutano ule hapakuwa na kukosoa kwa mtindo huu unaoelezwa hapa juu kwenye quote na hakuna shutuma zozote zilizotolewa ingawaje kulikuwepo na kukumbusha wajibu wetu kama wafanyakazi na viongozi wetu. Mimi binafsi sijawahi kumdhalilisha kiongozi yeyote wa juu ndiyo maana Sales Team wameshindwa kutaja jina la huyo kiongozi hapa ili watu watafakali. Nina imani kuwa viongozi wa juu huwa tunashidana kwa nguvu za hoja zinazojenga kampuni hii na wala si kudhalilishana, wafanyakazi ni mashahidi kwa hili.
Quote Wengi wao akiwemo Four Ways Mwanza. wamekutaja kwa jina kuwa u msumbufu, una majibu ya jeuri, na hujali mchango wao katika shirika.
Napenda kusema kuwa ni dhambi mbele ya Mungu kumsingizia mtu bila makosa. Mimi siwezi nikaijibu 4ways majibu ya jeuri naomba mtajeni mtu (specific person) ambaye nilimjibu jeuri ili tumuulize.
Quote Ushauri wetu wa bure kwako nikuwa, jiulize, je ni miaka mingapi uko kazini na je umewahi kuvumbua lipi jipya katika kuboresha sehemu yako ya kazi. Kama ulivyojigamba kuwa wewe unajua sana mambo ya Sales, sasa, ukipenda kuhamia Sales itabidi uende shirika jingine kwa vile kauli zako kwa wafanyakazi wenzio, abiria na maajenti hazito endana na majukumu ya kazi za Sales za Shirika la Ndege Tanzania..
Kauli hii sales Team wanaitoa wakati mwafaka ili viongozi wangu wa juu wanichukie bila sababu za msingi. Wanaitoa kauli hii wakijua kilichopo mbele yetu na ikiwa ni kuwakumbusha tu viongozi wangu kuwa wasilisahau jina hii AFRICAR KAGEMA katika idadi ya wafanyakazi 125 wanaoodoka na kuwakumbuka wao katika ufalme wa kubaki. Napenda kuwahakikishia watu wa Sales Team kuwa mimi si mtu ninayetishika na zoezi la kupunguza wafanyakazi kwani uwezo wangu unahitajika kila kona ya nchi hii.
MWISHO
Nikiwa kama mwanajamii wa ATCL ni wajibu wangu kutoa ushauri wakati wowote na mahali popote panapofaa ili kuhakikisha kuwa kampuni yangu ATCL inasonga mbele kwa faida yangu na Watanzania wote na Taifa kwa ujumla.
Hata hivyo natoa wito kwa watu wenye tabia ya kujenga chuki miongoni mwetu waache mara moja ili kuijenga ATCL na sio kujijenga wenyewe binafsi kwa maslahi yetu binafsi mbele ya jamii. Hata hivyo mimi binafsi nawaheshimu sana wafanyakazi wenzangu na nitaendelea kushirikiana nao bila kinyongo hadi mwisho wa ajira yangu.
Mungu ibariki ATCL, Mungu ibariki Tanzania
Imeandaliwa na;
AFRICAR TONONO KAGEMA
KWELI SHULE NI SHULE HATA UFANYE KAZI MIAKA MIA(100) KAMA HUNA SHULE YA KUKUSAIDIA LAZIMA UBAKI KULUMBUNA
Ni wajibu wetu sote kutambua kuwa biashara sio siasa na aihitaji mambo ya kisiasa badala yake inahitaji uwajibikaji na uzalendo kwa kila mmoja wetu kwa nafasi yake, kwa kutumia elimu yake na upeo wa uelewa wake kuhakikisha kampuni inayofanya biashara ya faida iweze kufanya hivyo kwa manufaa yetu sote.
Kabla sijaeleza yaliyojiri siku ya jumamosi tarehe 26/09/09 kwenye mkutano wa wafanyakazi uliohusu kupunguza wafanyakazi, napenda kusema kuwa nimesikitishwa na nimefedheheshwa sana na majibu ya shutuma yaliyotolewa na sales team kujibu hoja ambazo sikuzitoa kwenye mkutano huo.
Hoja zangu kwenye mkutano huo wa tarehe 26/09/09 zilizogawanyika katika mada mbili ambazo nilizitoa kwa maadishi ambayo nakala yake wanayo COWTU zilikuwa ni;
i. Kutopunguza Wafanyakazi
ii. Kupunguza Wafanyakazi
Katika maelezo haya nitaijadili mada moja tu yaani Kutopunguza wafanyakazi ambayo sales Team wameijibu kama ifuatavyo;
KUTOPUNGUZA WAFANYAKAZI
1. MAPATO
Mimi nilipingana na zoezi la kupunguza wafanyakazi kama kigezo cha kupunguza gharama za uendeshaji wa kampuni badala yake niliomba kampuni kufanya yafuatayo ili kuongeza mapato na kupunguza gharama za kampuni;
a) Kuimarisha (Kuboresha) Vituo vyake vya Mauzo
Nilitoa rai kwa kampuni kurekebisha vituo vyake vya mauzo ili kukabiliana na ushindani uliopo katika soko. Nikitolea mfano wa vituo vya ATC House na Interline sales counters ambavyo mazingira yake yanakuwa kana kwamba Air Tanzania haina ushindani wowote katika soko hivyo kwa mazingira yoyote yale wateja watakuja tu kununua tiketi.
b) Kupunguza tiketi za bure yaani Liberty
Nilishauri kampuni kupunguza kutoa tiketi za liberty kwa wafanyakazi na management na watu wengine kwani tiketi hizi ndizo chanzo cha kupungua kwa mapato kwa kampuni. Niliendelea kusisitiza kuwa liberty hazina control yoyote na watu wa Fedha (Finance) hivyo hakuna mtu anayejua kuwa kampuni inapoteza kiasi gani kwa siku, Mwezi au Mwaka kutokana na tiketi hizi. Nilitolea mfano kuwa tiketi hizi zinatolewa na watu wa record na Commercial bila kuwahusisha watu wa Finance hivyo kutojua hasara inayopatikana.
c) Kuimarisha uhusiano mzuri kati ya Air Tanzania na Travel Agents ndani na nje ya nchi.
Nilikubushia kuweka uhusiano mzuri kati ya Air Tanzania na Travel Agents wa ndani na nje ya nchi kwani travel agents wanachukua nafasi kubwa katika mapato ya kampuni.
Uhusiano wa Ndani.
Nikielezea uhusiano wa ndani niliwakumbusha watu wa Commercial kuwa wanapaswa kutoa majibu yanayojitosheleza kwa travel agents kuhusu masuala yanayohusu uhasibu au BSP na kama wanaona hawana utaalam nayo wanapaswa kuniuliza ua kumuuliza mtu wa BSP kwa sasa AFRICAR ili wapate majibu sahihi badala ya kutoa shutuma kuwa mtu wa BSP ndiyo kikwazo cha matatizo yao.
Nikielezea kuhusu matatizo yanayojitokeza mara kwa mara ya refunds wakati mwingine zinachelewa kutokana na utaratibu niliojiwekea kwamba lazima zichunguzwe na watu wa Help desk au Mama Kikowe na kuzifunga kwanza ndipo nizifanyie kazi. Vilevile ifahamike kuwa wakati mwingine tiketi hazionekani kwenye system kwa hiyo mimi (Africar) na watu wa help Desk inabidi kuomba msaada kutoka SITA, ATLANTA AU MERCATOR ili kujua status zake.
Uhusiano wa nje.
Niliikumbusha kampuni kuangalia upya soko la South Africa kwani mpaka sasa Travel Agents wanadai ZAR 1,269,618@ 168 = TZS 213,295,824 credit card refunds ambazo zitaisumbua sana kampuni ikianza safari zake huko. Kampuni itambue kuwa deni hili halijalipwa kwa muda mrefu tangu December 2008.
d) Kulifanyia Matengenezo jingo la ATC House.
Nilitoa wito kwa kampuni kulifanyia matengenezo jengo la ATC House ili lipangishwe kwa kutangaza tenda na makampuni makubwa tu ndio yapewe nafasi yatakayoweza kupanga floor nzima ili kuweza kupata pesa nyingi kwa mkupuo kuliko hizi pesa ndogo ndogo tunazopata kwa sasa.
Nilipendekeza ukarabati ufanyike ili kubadilisha mabati juu ya paa ambayo yameoza na yanavuja hivyo kuleta usumbufu kwa wapangaji ikiwa ni pamoja na mabomba ya maji machafu.
Vilevile nilipendekeza wafanyakazi wa ATC House wahamie Mezzanine Floor kama ilivyokuwa zamani na kupangisha ghorofa ya kwanza,pili na Tatu.
e) Mikataba Mibovu
Nilitoa ushauri kwa kuirekebisha mikataba yote mibovu na inayopunguza mapato ya kampuni kama vile mikataba ya Miss Tanzania ambayo ni dhahiri kuwa haiinufaishi Air Tanzania badala yake inawanufaisha hawa Miss Tanzania na wenzao. Ni ukweli usiopingika kuwa Miss Tanzania inaitangaza Air Tanzania wakati wa mchakato wa kumpata Miss Tanzania tu lakini baada ya hapo hawaisaidii kampuni hii, hivyo wanapanda ndege bure tu. Niliomba mikataba hiyo iwe ya kipindi Fulani tu hasa wakati wa mchakato.
Vilevile mikataba ya Clouds FM ambayo nayo sio kila siku inaitangaza Air Tanzania, lakini wafanyakazi wake wanatumia liberty kila mara.
Hivyo ni wajibu wa kampuni kuangalia upya mikataba kama hii ili kuinusuru kampuni na kuongeza mapato yake.
f) Kuimarisha Kitengo cha mawasiliano.
Nilitoa wito kwa kampuni kuimarisha kitengo hiki ili wateja wetu wapewe maelezo au taarifa mapema inapotokea mabadiliko yoyote katika ndege zetu. Nilitolea mfano wa abiria ambao walijikuta wanasafiri hadi Kigoma wakati wao walikuwa wanaenda Tabora kwenye mkutano. Nikitolea mfano kama huu hapa chini,
Dear Rashida,
First of all may I take this opportunity to apologize for the inconveniences caused to our valuable customers due to unexpected schedule change of our flight to TBO.
Please convey our sincere apologies.
ATTN: Africar kindly processes ACM as requested and please waive all charges.
MBWETTE/TOLLYPROF (PNR# ZV6KGU, TKT# 197 3360837165)
VARISANGA/MODESTPROF (PNR# N62L3A, TKT# 197 336083716
MARGESON/DALOTTAPROF (PNR# N62L3A, TKT# 197 3360837167
2. MATUMIZI
Katika kipengele hiki niliiomba kampuni kupunguza matumizi katika mambo yafuatayo;
a) Kupunguza Duty Travel zisizokuwa za lazima kwa wafanyakazi na management.
b) Kupunguza matumizi mengine yoyote yasiyokuwa ya lazima ili kuinusuru kampuni na gharama zisizokuwa za lazima na kubana matumizi ikiwa ni pamoja na mikataba mibovu.
KUJIBU TUHUMA ZA SALES TEAM
Kwanza ni matumaini yangu kuwa kwa wale waliokuwepo kwenye mkutano huu watakubaliana na mimi kuwa hayo maneno na lugha iliyotumika haikuwepo kwenye mkutano ule. Vilevile ukisoma kwa umakini sana utagundua kuwa hawa watu wanageneralize tuhuma zao na hawako specific kwa kila kauli wanayodai kama vile
Quote Sales wamebweteka tu na hawafanyi kazi yoyote, hawana uhusiano mzuri na Ma-Ajenti wanao tuuza. Pia Sales hawajui wafanyalo wanaleta mkongamano na BSP/Agents, na kwamba tuje kwako utufundishe kazi. Hizi ni shutuma nzito na zinatia karaha, hasa kutoka kwa mtu kama wewe Afrika.
Napenda kusema kuwa hizi kauli hazikutolewa na mtu yeyote kwenye mkutano huo. Hivyo huku ni kupotosha jamii ya ATCL hasa ambao hawakuhudhuria mkutano huo waelewe hivyo. Hizi ni hadithi za kutunga kwani hakuna binadamu mwenye akili timamu anaweza kutamka maneno haya.
Quote Sisi tunaichukulia kuwa hukutoa shutuma hizi kwa nia njema ya kujenga, bali kama kawaida yako, lazima ukosoe ili uonekane unajua, hata ikibidi kuwadhalilisha viongozi wa juu sana kwako.
Napenda kusema kuwa kwenye mkutano ule hapakuwa na kukosoa kwa mtindo huu unaoelezwa hapa juu kwenye quote na hakuna shutuma zozote zilizotolewa ingawaje kulikuwepo na kukumbusha wajibu wetu kama wafanyakazi na viongozi wetu. Mimi binafsi sijawahi kumdhalilisha kiongozi yeyote wa juu ndiyo maana Sales Team wameshindwa kutaja jina la huyo kiongozi hapa ili watu watafakali. Nina imani kuwa viongozi wa juu huwa tunashidana kwa nguvu za hoja zinazojenga kampuni hii na wala si kudhalilishana, wafanyakazi ni mashahidi kwa hili.
Quote Wengi wao akiwemo Four Ways Mwanza. wamekutaja kwa jina kuwa u msumbufu, una majibu ya jeuri, na hujali mchango wao katika shirika.
Napenda kusema kuwa ni dhambi mbele ya Mungu kumsingizia mtu bila makosa. Mimi siwezi nikaijibu 4ways majibu ya jeuri naomba mtajeni mtu (specific person) ambaye nilimjibu jeuri ili tumuulize.
Quote Ushauri wetu wa bure kwako nikuwa, jiulize, je ni miaka mingapi uko kazini na je umewahi kuvumbua lipi jipya katika kuboresha sehemu yako ya kazi. Kama ulivyojigamba kuwa wewe unajua sana mambo ya Sales, sasa, ukipenda kuhamia Sales itabidi uende shirika jingine kwa vile kauli zako kwa wafanyakazi wenzio, abiria na maajenti hazito endana na majukumu ya kazi za Sales za Shirika la Ndege Tanzania..
Kauli hii sales Team wanaitoa wakati mwafaka ili viongozi wangu wa juu wanichukie bila sababu za msingi. Wanaitoa kauli hii wakijua kilichopo mbele yetu na ikiwa ni kuwakumbusha tu viongozi wangu kuwa wasilisahau jina hii AFRICAR KAGEMA katika idadi ya wafanyakazi 125 wanaoodoka na kuwakumbuka wao katika ufalme wa kubaki. Napenda kuwahakikishia watu wa Sales Team kuwa mimi si mtu ninayetishika na zoezi la kupunguza wafanyakazi kwani uwezo wangu unahitajika kila kona ya nchi hii.
MWISHO
Nikiwa kama mwanajamii wa ATCL ni wajibu wangu kutoa ushauri wakati wowote na mahali popote panapofaa ili kuhakikisha kuwa kampuni yangu ATCL inasonga mbele kwa faida yangu na Watanzania wote na Taifa kwa ujumla.
Hata hivyo natoa wito kwa watu wenye tabia ya kujenga chuki miongoni mwetu waache mara moja ili kuijenga ATCL na sio kujijenga wenyewe binafsi kwa maslahi yetu binafsi mbele ya jamii. Hata hivyo mimi binafsi nawaheshimu sana wafanyakazi wenzangu na nitaendelea kushirikiana nao bila kinyongo hadi mwisho wa ajira yangu.
Mungu ibariki ATCL, Mungu ibariki Tanzania
Imeandaliwa na;
AFRICAR TONONO KAGEMA
KWELI SHULE NI SHULE HATA UFANYE KAZI MIAKA MIA(100) KAMA HUNA SHULE YA KUKUSAIDIA LAZIMA UBAKI KULUMBUNA