Ngwananzengo
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 1,911
- 1,312
Mh. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete ameitumia sikukuu ya Mei Mosi kuwaaga wana-mwanza. Akiwa na bashasha na uchangamfu mkubwa alionyesha kufurahia uwepo wake Mwanza. Hakutaka kujikimbusha histori mbaya iliyomkuta hapa Mwanza. Kwanza ni pale alipovamiwa jukwaani mwaka 2005 akiwa kwenye kampeni. Pili ni pale alipoanguka kwenye mkutano na viongozi wa dini. Mh Dr. Jakaya Kikwete ametuaga wana-mwanza bila yaqkitimiza ahadi yake ya kuifanya Mwanza kuwa California ya Tanzania na Afrika Mashariki. Ni aibu lakini ndio ukweli wenyewe ndani ya utawala wake hata barabara ya njia mbili hatujajengewa. Ni karibu sana kutoka Mwanza kwenda kwenye miji mikubwa ya ukanda huu wa maziwa makuu (mfano Kampala, Bujumbura, Arusha, Nairobi, Lubumbashi, Kigali na Dar es salaam) lakini cha kushangaza ni hali ya uwanja wa ndege. Meli kwa ajili ya usafiri wa ziwa Victoria bado ni kitendawili.Treni bado haijawa usafiri wa uhakika kwa mizigo na abilia. Mh. Dr. Jakaya umeondoka bila kuigeuza Mwanza kuwa California. Ahadi ni deni lakini hii yetu itabidi tusamehe.