Tukio la kushambuliwa Lissu: Wahusika dhahania wa kufikirika

Mwaka 2009 ulikuwa uchaguzi ndani ya Chadema,lakini mwaka mmoja kabla, yaani August 2008 Chacha Zakayo Wangwe alifariki ktk ajali ya gari iliyogubikwa na utata mwingi.

Mwaka 2014 ulikuwa uchaguzi ndani ya Chadema,mwaka 2013 habari zilisambaa kuwa mmoja wa vijana wa Chadema (jina linajulikana) alituhumiwa hadharani kuwa akitumwa kumuwekea Sumu Zitto Kabwe.

Mwaka 2018 ni uchaguzi mkuu ndani ya Chadema, Septemba 2017 Tundu Lissu amepatwa na tukio la kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Haya matukio hayahusiani, ila yote yametokea mwaka mmoja kabla ya mwaka wa uchaguzi ndani ya Chadema. Inavyoonekana mwaka mmoja kabla ya uchaguzi huwa siyo mwaka mzuri sana kwa viongozi wa juu wa Chadema

[HASHTAG]#GetWellSoonTunduLissu[/HASHTAG] [HASHTAG]#LetUsAllPray4Lissu[/HASHTAG]

Magoiga SN
Damu ya mtu hajawahi kumwacha muuaji bila kuweweseka. Jificheni kwenye ID fake lakini Mungu anawajua mpaka kwa sura atawaumbua tu. Vipropaganda vya kipumbavupumbavu mnadhani vitamsafisha aliyeahidi kuwashughulikia wapinzani wakitoka bungeni? Na Lissu kapigwa risasi akiwa anatoka bungeni. Hakuna utakaso Wa kunawa maji kwenye mikono ya damu. Mikono yenye damu husafishwa kwa toba na ungamo. Mwambieni ajitokeze atubu vinginevyo damu ya Saanane, Roma na Lisu itaendelea kuchuruzika mikononi mwake maisha yake yote.

ACHA nikae KIMYA...!
 
Damu ya mtu hajawahi kumwacha muuaji bila kuweweseka. Jificheni kwenye ID fake lakini Mungu anawajua mpaka kwa sura atawaumbua tu. Vipropaganda vya kipumbavupumbavu mnadhani vitamsafisha aliyeahidi kuwashughulikia wapinzani wakitoka bungeni? Na Lissu kapigwa risasi akiwa anatoka bungeni. Hakuna utakaso Wa kunawa maji kwenye mikono ya damu. Mikono yenye damu husafishwa kwa toba na ungamo. Mwambieni ajitokeze atubu vinginevyo damu ya Saanane, Roma na Lisu itaendelea kuchuruzika mikononi mwake maisha yake yote.

ACHA nikae KIMYA...!
Kikulacho ki nguoni mwako.
 
wa somali kuna alshabaab, nigeria bokoharam Syria Is, Isl mara al-Qaeda lakini Tanzania tuna kikundi kinaitwa watu wasiojulikana sijui manayake nn? Kila linalotokea ni hao hao wasiojulikana ni aibu kuitwa mwana wa nchi hii!
tutegemee kusikia na wao ndo wahusika.. mimi naisi ni kikundi kinaitwa wasiojulikana ndo pakujiuliza wanatoa wapi motives za kushambulia watu unless wao na kiongozi wao asiyejulikana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii imebuma hii! Mlijiandaa na hii propaganda mkidhani Lissu atakufa. Sasa mmebaki kama kupe mnyonyaji asiyejuwa mabadiliko kwenye maisha ya ng'ombe...Hadi ngozi inawambwa yeye wamo tuu!

This time hakuna hiyo kitu maana Lissu ni mzima. Atarudi na atawatoa nishai. Atawataja tu, coz anawajuwa. Hakuna ambaye angechukulia more serious kama angewataja kabla ya jaribio hili.

Kwahiyo mkuu kwa kifupi single imebuma hii!

Pambaneni tu na hali zenu hakuna jinsi.
 
Km Unalindwa Na Mabwana Wakubw,ujue Laana Haitakuacha Vizazi Vyako Vyote Usijidanganye Kujificha Kwenye Id Fake.
 
Dk Slaa kaikimbia nchi kwa zaidi ya mwaka sababu kubwa ikiwa hofu kwa usalama wa uhai wake.

Unafikiri waliotishia uhai wake ni magufuli na serikali yake?! Think twice.

Dr. Slaa kakimbia nchi kuhofia usalama wake? Be serious!
 
Kinachohitajika bila kujali muuaji ni nani, na kwa nini aliua huyu ama yule kwa serkali na vyombo vyake vya usalama ni KUWAKAMATA WAUAJI NA KUWAFIKISHA MBELE YA SHERIA. Otherwise ni porojo tu!!
 
Mnaanza kuwahusisha nchi zinazotuzunguka na watu wa acacia aisee we wakutafute tu huna la maana unaloeleza hapa
 
According to my assumption hausiki. Namna najaribu kumfikiria. Labda nnachoweza kusema ni hicho kikundi cha watu either raia ama watu waliopo kwenye ndani ya serikali ambao wana mapenzi binafsi naye na ambao labda kwa tafsiri zao Tundu Lisu ni threat kwa taifa... Ila sioni kwamba Raisi anahusika.. japo watu almost wengi kwenye mitandao wanafikiri kama wewe.. ila mimi nasema hapana ndo mana sijamtaja.... Mengine Mungu atayafunua siku nyingine kwa namna ya kipekee.
1+1=2 Ongezea na swahiba zake wa jirani wanvyoshughulikia wasiowapenda jibu =3 najua unaujua ukweli ila unajifanya uonekane critical thinker my take umejificha peupeeee.
 
Aisee kama ndio basi asizuie Wote wanaomsaidia lisu
According to my assumption hausiki. Namna najaribu kumfikiria. Labda nnachoweza kusema ni hicho kikundi cha watu either raia ama watu waliopo kwenye ndani ya serikali ambao wana mapenzi binafsi naye na ambao labda kwa tafsiri zao Tundu Lisu ni threat kwa taifa... Ila sioni kwamba Raisi anahusika.. japo watu almost wengi kwenye mitandao wanafikiri kama wewe.. ila mimi nasema hapana ndo mana sijamtaja.... Mengine Mungu atayafunua siku nyingine kwa namna ya kipekee.
 
Nawasihi tuonyesheni picha zenu halisi. Je hamkusema Lissu ni msaliti wa taifa hili?, Je hamkusema ni mchochezi? Je hamkusema amenunuliwa na makampuni makubwa ya nje? Kama nyie wenye akili mlifikia hatua ya kusema maneno makali na ya chuki za wazi namna hii, mlitegemea wapumbavu watafanya nini??
 
Mtu wa usalama ni mtu mwenye utu kama mtu mwingine...naamini alitekeleza kazi aliyotunwa ila hakuwa na lengo la kumuondoa Lissu ndo maana alifanya Randomly attack...Lissu umetutoa watanzania machozi ipo siku Mungu atatulipia tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hii imebuma hii! Mlijiandaa na hii propaganda mkidhani Lissu atakufa. Sasa mmebaki kama kupe mnyonyaji asiyejuwa mabadiliko kwenye maisha ya ng'ombe...Hadi ngozi inawambwa yeye wamo tuu!

This time hakuna hiyo kitu maana Lissu ni mzima. Atarudi na atawatoa nishai. Atawataja tu, coz anawajuwa. Hakuna ambaye angechukulia more serious kama angewataja kabla ya jaribio hili.

Kwahiyo mkuu kwa kifupi single imebuma hii!

Pambaneni tu na hali zenu hakuna jinsi.
Jaribu kuelewa nilichokiandika mkuu.. Ulivo comment ni kama umeniweka kwenye uhusika wa tukio kitu ambacho sio kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom